Rais, idhinisha malipo ya PSSSF toka Serikalini kwa ajili ya wastaafu ATCL

kisingi

JF-Expert Member
Apr 9, 2014
516
377
Kwa heshima na taadhima tunakuomba mheshimiwa Rais wa nchi yetu idhinisha malipo ya madai ya wastaafu wa ATCL. Kumekuwa na dana dana juu ya kulipwa hawa wastaafu toka Katibu Mkuu Kiongozi alipo iandikia wizara Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kushughulikia malipo ya madai ya wastaafu wa ATCL.

Wizara haijafanya lo lote kwa madai kuwa Hazina ndio wanatakiwa kupeleka pesa PSSSF. Mheshimiwa raisi, wastaafu hawa wanaelezwa na maafisa wa PSSSF kuwa pesa iliyolipwa toka serikalini kipindi chote kilicho pita hakuna malipo kwa ajili ya wastaafu wa ATCL.

Ombi maalum kwa mheshimiwa raisi, wasaidie wastaafu hawa wanyonge kulipwa mapungufu ya pension zao maana uhakiki ulifanyika zaidi ya mara mbili.

Tumeshuhudia wengine wakifariki bila kupata haki zao.
 
Inachouma wazee wametumikia kampuni kwa moyo mmoja na upendo wanakuja kuteseka uzeeni. Hii ni laana kubwa sana waangalie hili mara mbili mbili
 
Tusaidiane kupaza sauti ili waliokaribu ya mheshimiwa raisi wamfikishie kilio hiki maana yeye hupata taarifa nyingi moja kwa moja.
 
Hivi kweli PSSSF mko makini ama kunamnao shirikiana kuwadhulumu wastaafu wa ATCL. Mnajaza gaps ambazo wastaafu hawakulipwa na kuwaeleza waandike barua muqalipe.

Wastaafu wameandika barua mwisho wanapofuatilia malipo wanaambiwa serikali haijalipa kwenu na kukuta zile gaps mmeondoa sehemu mlizokuwa mmejaza. Huu ni uwizi au utapeli kwa wastaafu wa ATCL. Kwa nini mlifanya yote hayo kumbe hamjalipwa.

Mbona Rais kila siku anajinasibu kuwa kalipa madai yote ya PSSSF. Nani mkweli hapa.

RAIS HEBU OKOA JAHAZI WASTAAFU WA ATCL WALIPWE MADAI YAO AMBAYO HATA MAHAKAMA ILIAMURU WALIPWE LAKINI VIONGOZI WATEULE WAKO HAWATAKI KULIPA.
 
Alivyowafanyia watumishi hakika Mungu yupo.Miaka yote 5 ni kapa huku wakidhalilika kwa hali ngumu ya maisha huko mtaani.Poleni walimu,madaktari,wauguzi etc
 
Serikali yenyewe inajua na imewachukulia hatua wahusika na hukumu nyingine ishatoka. Wengine ni vigogo zaidi.
Hawa wastaafu walimaliza ajira zao salama walipwe haki zao. Hawakuwa na mamlaka ya kiutendaji.
 
Nchi hii ukitaka usife kwa presha ya pensheni..Basi kuwa mwanasiasa...wenyewe wanalipwa kabla ata hawajastaafu.
 
Hilo nalo neno. Ukiwa mbunge wewe umeondokana umasikini. Posho kibao, hakuna kiwango cha elimu ya juu ili ugombee. Tumeona juzi Lugola akigomea mapendekezo ya budget kwa kuwa yamegusa maslahi yao.
 
Ukifanyakazi kwa uadilifu adha yake ndio hiyo unastaafu serikali haikuthamini tena. Sheria za kukulinda ulipwe haki yako waliopo madarakani hawazijali wanazidharau. PSSSF wanadharua sheria namba 2 ya 2018 kuhusu mifuko ya jamii na serikali nayo imedharau amri / hukumu halali ilitaka wastaafu wa ATCL walipwe madai yao.
 
hivi mstaafu wa ATCL anataka alipwe hiyo pensheni kwa kipi hasa.Kwamba kuna kitu cha maana alichofanyia taifa na hilo shirika la ATCL.
 
Kwa heshima na taadhima tunakuomba mheshimiwa Rais wa nchi yetu idhinisha malipo ya madai ya wastaafu wa ATCL. Kumekuwa na dana dana juu ya kulipwa hawa wastaafu toka Katibu Mkuu Kiongozi alipo iandikia wizara Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kushughulikia malipo ya madai ya wastaafu wa ATCL.

Wizara haijafanya lo lote kwa madai kuwa Hazina ndio wanatakiwa kupeleka pesa PSSSF. Mheshimiwa raisi, wastaafu hawa wanaelezwa na maafisa wa PSSSF kuwa pesa iliyolipwa toka serikalini kipindi chote kilicho pita hakuna malipo kwa ajili ya wastaafu wa ATCL.

Ombi maalum kwa mheshimiwa raisi, wasaidie wastaafu hawa wanyonge kulipwa mapungufu ya pension zao maana uhakiki ulifanyika zaidi ya mara mbili.

Tumeshuhudia wengine wakifariki bila kupata haki zao.
Swichi za ndege mlikuwanazo kwanini hamkuikamata ndege moja?
 
Hata NSSF nako ni tabu tu, Watu wanateseka sana kupata mafao yao. Bahati mbaya hakuna mtetezi. Wabunge wetu ndio wanapitisha sheria za kumkandamiza mtumishi.

Wataalam wa sheria, hivi hakuna namna ya kuyashitaki haya mashirika yalipe haki za watu na faini juu, ili ifike mahali yaheshimu haki za watu na uwajibikaji kwa wanachama wao?
 
Back
Top Bottom