GE2025 Rais Dkt. Mwinyi atangaza Oktoba 29 ni siku ya mapumziko

GE2025 Rais Dkt. Mwinyi atangaza Oktoba 29 ni siku ya mapumziko

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

PAYE

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2025
Posts
354
Reaction score
395
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi ameitangaza kuwa Tarehe 29 Oktoba 2025 Siku ya Jumatano kuwa ni siku ya mapumziko kwa wananchi wote wa Zanzibar

Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu inaeleza kuwa sababu za Rais Mwinyi kufanya uamuzi huo ni kwaajili ya kutoa nafasi kwa wananchi wa Zanzibar kushiriki katika zoezi la kupiga kura ili kutekeleza haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka

Pamoja na hatua hiyo, Rais Dkt Mwinyi amewataka wananchi kufata miongozo na maelekezo yanayotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar ili kufanikisha zoezi hilo kwa salama na amani.

1761209100551.png
 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi ametangaza Oktoba 29, 2025 ambayo itakua ni siku ya Uchaguzi Mkuu kuwa itakuwa ni Siku ya Mapumziko kwa Wananchi wa Zanzibar.

Dkt Mwinyi ameyasema hayo hii leo Oktoba 23 kupitia taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Zanzibar ambapo ameeleza kuwa uamuzi huo unalenga kuwapa nafasi Wananchi wote wenye sifa kwenda kupiga Kura ili kutekeleza wajibu wao wa Kidemokrasia.

Aidha Dkt. Mwinyu amewasihi Wananchi wote kufuata maelekezo na miongozo iliyotolewa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ili kuhakikisha zoezi la upigaji kura linafanyika kwa amani, utulivu na nidhamu ka ilivyo desturi ya Taifa letu.
1761212260524.png
 
Kwa jins mama alivyovurugwa anaweza kutangaza ni siku ya maandamano
 
Back
Top Bottom