Wafanyabiashara na wenye mabenki ni wajanja kuliko mnavyofikiri. Unaweza kua unapeleka gari za serikali kufanyiwa service katika gereji flani na zikatozwa gharama za kawaida kabisa, lakini kile kitendo cha kupeleka tender pale tu tayari unakula commission yako ambayo haipo katika utaratibu rasmi na wala haitaonekana ktk muamala. Ikumbukwe fedha zote za TRA zinahifadhiwa benk kuu ila hawa wakapokea mgao kutoka serikalini kwa ajili ya shughuli za maendeleo kwao wao wakaamua kuziweka FD ili zizalishe wapate faida. Kitendo cha kuweka fedha pale tayari kimewanufaisha wenye benk ambao inawezekana walikua na hali ngumu ya kifedha wanazizungushia na kupata faida, fadhira ambayo ingerudishwa isingeonekana kwenye miamala. Swali la kujiuliza kama ni kawaida fedha zinazotengwa kwenye bajeti ya serikali ambazo zinapitishwa na bunge ni halali kuwekwa FD, Je bunge lilipitisha kua chanzo mojawapo cha mapato ya serikali ni faida itokanayo na FD ya fedha za serikali? Ili faida hiyo iingie katika mipango ya serikali. Kama ni halali basi na halmashauri pamoja taasisi zingine ziweke FD pesa za maendeleo ili zipate fedha za kutosha maana kila siku wanalalamika fedha zinafika lakin hazitoshi