Umewahi sikia serikali ina lala? Je wajuwa Rais ndio Amiri jeshi mkuu wa majeshi yote hivyo hana jp wala sikuku kila siku kazi ila ni uwamuzi wake kupumzika au kufanya kazi. Hivyo yuko sawa serikali ya wachapa kazi wewe lala.Imekuwa kawaida Sana kusikia Rais anateua na kutengua siku za weekend au
Hata usiku wa manane..
Taarifa zimekuwa kila mara zinapotoka hazijali kabisa ni saa ngapi na siku gani..
Hata siku za sikukuu watu wametenguliwa na kuteuliwa..
Rais anatakiwa awe mfano Kwa waajiri wote na wakuu wote wa kazi..
Katika Taifa ambalo waajiri hawaheshimu Sana masaa ya kazi na siku za kupumzika..Rasi no vizuri akawa mfano bora ..
Ili watu wa chini yake wasitumie hayo mazoea ya Rais kunyanyasa watu wa chini
Na kuwafanyisha kazi na kufukuza na kuajiri bila kujali sikukuu au weekend au ni usiku...
Kama Rais hajali nini kitamzuia waziri au mkurugenzi kupitiliza masaa ya kazi Kwa kujifanya ni kuna Jambo muhimu Rais kaagiza?..
Nini kitazuia hata watu wa chini kutoa maagizo Kwa kuwapigia simu watu usiku au siku za weekend au za sikukuu?
Hata kama Rais ana utaratibu wake kaweka WA kufanya kazi weekend na sikukuu ..Yeye Rais Hana mtu wa juu anaempa maagizo...yeye anaweza kuamua wakati gani gani apumzike au afanye kazi..ni vizuri na yeye akaweka utaratibu wa kuheshimu Kwa wengine wa chini yake..
Kingine utoaji wa maagizo hadi siku za sikukuu na weekend ya kufukuza na kuteua huleta picha ya kama kuna dharura au Jambo ambalo haliwezi kusubiri wakati hao hao wanaotumbuliwa wanakuja kuteuliwa tena
