Raia mwema na Raia Tanzania

Raia mwema na Raia Tanzania

Milindi

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2009
Posts
1,478
Reaction score
757
Namshukuru Mungu kuniwezesha kutambua ni kwanini magazeti haya sasa hivi yanamchafua sana Lowassa.

Hii ni hali ileile iliyompa ulaji Salva na Salva sasa ni mtu mwingine tofauti na mwandishi wa habari. Salim alichafuliwa vilivyo mpaka mukulu tukamuita chaguo la Mungu.

Kwa taarifa yenu watanzania wa sasa si wa miaka kumi iliyopita mtaandika na kuchafua sana lakini ukweli utabaki palepale.

Mabadilikoooooo....................
 
Ina maana Jenerali nae ananunulika siku hizi?

manake ni kama wameamua kupiga kampeni za wazi kabisa za kumsaidia Magufuli...

nimejiuliza why wanaogopa kuwa neutral...
 
Huwezi kuwa neutral
lazima uwe moto au baridi...
Hawawezi ujua ukweli afu wa pretend kutojua...
Yani uachie wananchi waamue? kwa akili zipi?
Lazima waonyeshwe njia..kuwa huku siko....

Mi nimefurai jinsi wasivyomung'unya maneno...
Hata CDM ukweli wanaujua....
Ila wana interests zao (wanatumiana)

Ina maana Jenerali nae ananunulika siku hizi?

manake ni kama wameamua kupiga kampeni za wazi kabisa za kumsaidia Magufuli...

nimejiuliza why wanaogopa kuwa neutral...
 
Namshukuru Mungu kuniwezesha kutambua ni kwanini magazeti haya sasa hivi yanamchafua sana Lowassa.Hii ni hali ileile iliyompa ulaji Salva na Salva sasa ni mtu mwingine tofauti na mwandishi wa habari.Salim alichafuliwa vilivyo mpaka mukulu tukamuita chaguo la Mungu.Kwa taarifa yenu watanzania wa sasa si wa miaka kumi iliyopita mtaandika na kuchafua sana lakini ukweli utabaki palepale.
Mabadilikoooooo....................

Haya magazeti yana wasomaji? Mimi sinunuagi tofauti na The Citizen, Mwananchi, Tanzania Daima, MwanaHALISI.
 
..huyo manyerere anazunguka na makufuli everywhere,hawezi kuacha kumpamba bosi wake wakati kila siku anapewa bahasha ya kaki.!
 
[U said:
The Boss;14155188]Ina maana Jenerali nae ananunulika siku hizi?[/U]

manake ni kama wameamua kupiga kampeni za wazi kabisa za kumsaidia Magufuli...

nimejiuliza why wanaogopa kuwa neutral...

Anunuliwe mara ngapi?
Magazeti anayomiliki Rostam yalikuwa ya Nani?. Kutoka Rai Hadi Raia na hatima ya Tanzania-2015

 
Huwezi kuwa neutral
lazima uwe moto au baridi...
Hawawezi ujua ukweli afu wa pretend kutojua...
Yani uachie wananchi waamue? kwa akili zipi?
Lazima waonyeshwe njia..kuwa huku siko....

Mi nimefurai jinsi wasivyomung'unya maneno...
Hata CDM ukweli wanaujua....
Ila wana interests zao (wanatumiana)


Jenerali alifanya hivi kwa Mkapa
walimsaidia mno kumshinda Mrema halafu Mkapa akaja kumvua uraia Jenerali
na kupiga stop matangazo ya serikali kwenye magazeti yake hadi kampuni ikafa
akaiuza...na aliapa kubaki neutral na kuto side na yeyote

sasa ndo najiuliza why now ana take side?
ni kweli Lowassa ni 'that big threat'?
Magufuli akija wageuka je?

Mimi binafsi sioni kama wanahitaji kumsaidia Magufuli...
wabaki katikati wawe balanced....sioni kama Magufuli atashindwa
 
Huwezi kuwa neutral
lazima uwe moto au baridi...
Hawawezi ujua ukweli afu wa pretend kutojua...
Yani uachie wananchi waamue? kwa akili zipi?
Lazima waonyeshwe njia..kuwa huku siko....

Mi nimefurai jinsi wasivyomung'unya maneno...
Hata CDM ukweli wanaujua....
Ila wana interests zao (wanatumiana)

Shida ni kujua ni nani anayemwonyesha mwingine njia. Ni yule anayeegemea upande mmoja au ni yule anayechambua kama ni watu - kuwachambua wote - na kama ni sera - kuzichambua zote - na kumwachia anayechagua achague kwa utashi wake. Au kumwonyesha mwingine njia ni kuwa kipofu sehemu moja na kuwa na macho zaidi ya mawili sehemu nyingine? What I see is just propaganda na huko kuegemea upande fulani ni kuonyesha wapi chombo fulani kina maslahi kitu ambacho ni tofauti kabisa na kuonyesha njia.
 
Anaogopa kuambiwa siyo raia watz,pia na umri umeenda anataka na yeye aenziwe kama Akina SALVA,MUHINGO na CHARLES CHARLES,kwa sasa hivi hayo magazeti siwezi hata kufungia vitumbua vitachafuka.

Ni zaidi ya hivyo mkuu! Saddam rais wa Kuwait ana undugu wa mbali na Ulimwengu. Kuna watu wawili nimewadharau sana kupita maelezo kipindi hiki cha uchaguzi kwani nimegundua hawayasimamii yale wanayoyasema, Ulimwengu ni mmojawapo. Huyu mzee kawasema sana Kikwete na Mkapa najiuliza tofauti yao ni nini na Magufuli? Kiukweli hakuna maana kama uchafu Magufuli naye anao wa kutosha. Conclusion yangu ni kwamba Ulimwengu ni fuata upepo kitu ambacho ni kibaya kuliko maelezo.
 
Inasikitisha magazeti tuliyoyapenda kwa kuwabana watawla yamegeuka kuwasifu watawala. sisi wanyonge nani atatutetea? Uchaguzi ukiisha ndio mwisho wa hayo magazeti! Mimi nilikuwa sikosi kununu gazeti la rai kila jumatano. Nikipitwa na nakala najisikia kama sijui nimekosa nini! lakini huwezi kuamini leo wametugeuka wanyonge kwa sababu ya peasa za kuhongwa! Bil. 150 kweli imefanya kazi!
 
Ina maana Jenerali nae ananunulika siku hizi?

manake ni kama wameamua kupiga kampeni za wazi kabisa za kumsaidia Magufuli...

nimejiuliza why wanaogopa kuwa neutral...
Kichwa cha habari cha Raia Tanzania leo kimemdhalilisha Generali na wenzake ! Hata kama ni kushabikia basi na taaluma ibaki kidogo! Pale juu wangeonesha kuwa maneneo yale yamesemwa na Na Mtoto wa Nje ya ndoa Nape Mnauye! Poor GENERALI NA WENZAKO MWAKA HUU NI SHIDA!
 
Ukweli hauna pande mbili...

Mimi nawshangaa wasio wazi kimsimamo...ndumila kuwili kuliko walio wazi....

Jenerali alifanya hivi kwa Mkapa
walimsaidia mno kumshinda Mrema halafu Mkapa akaja kumvua uraia Jenerali
na kupiga stop matangazo ya serikali kwenye magazeti yake hadi kampuni ikafa
akaiuza...na aliapa kubaki neutral na kuto side na yeyote

sasa ndo najiuliza why now ana take side?
ni kweli Lowassa ni 'that big threat'?
Magufuli akija wageuka je?

Mimi binafsi sioni kama wanahitaji kumsaidia Magufuli...
wabaki katikati wawe balanced....sioni kama Magufuli atashindwa
 
Ukweli hauna pande mbili...

Mimi nawshangaa wasio wazi kimsimamo...ndumila kuwili kuliko walio wazi....


Unasema waandishi wa habari lazima wa take side?
mimi naona watu binafsi ni sawa..but journalist wanawajibika kusema ukweli bila ku take side
shida ya ku take side ni kwamba hata ukiona jambo baya upande ule unaoutetea huwezi sema...
journalist alikuwa Sakina Datoo....

Kibaya zaidi ukimuunga mkono mgombea moja kwa moja
halazimiki kuaahidi chochote tena....
Sidhani kama Lowassa ni big threat hadi waandishi waamue wasiibane CCM kwa lolote
kwa kuhofia tu wakiibana CCM watamsaidia Lowassa....

Uchaguzi unakuja after only 5 years.....ni bora pia na CCM ibanwe ili iweze ku deliver
 
Huu ni upuuzi wa kutaka magazeti yote yaimbe wimbo wa Mwanahalisi, Tanzania Daima, Mawio, Mtanzania na hata nipashe.

Hilo gazeti linaandika ukweli ndio maana nyie mnalishupalia, maana linagonga kwenye mfupa.

Kwa nyie ambao mpo tayari kuchagua hata maiti au jiwe basi sio Saizi yenu, nyie someni hayo hapo juu ambayo ni vigumu kutofautisha Tanzania Daima, Mawio, Mtanzani na Uhuru.

Raia MWEMA ndipo Gazeti ambalo sikosi kulinunua, Nenda hata kwenye website yao angalia views, wakati mwingine makala moja inasomwa na watu Hadi elfu ishirini.

Wenye akili wanaelewa sio wote wanaweza kuburuzwa na Pesa za Lowassa.
 
Ina maana Jenerali nae ananunulika siku hizi?

manake ni kama wameamua kupiga kampeni za wazi kabisa za kumsaidia Magufuli...

nimejiuliza why wanaogopa kuwa neutral...

...JAMAA AME''GAMBLE''...labda baada ya uchaguzi awe tena dhidi ya serikali ndiyo biashara yake ya magazeti itaflourish,maana kwasasa anachofanya ni kazi ya Uhuru, Mzalendo na Habari Leo(Magazeti yanayoendeshwa kwa Ruzuku )..Kila wiki nilikuwa sikosi magazeti yake..ila kwa sasa yamekaa kipropaganda zaidi....Ndio maana nasema wakenya na Gazeti lao(MWANANCHI) wataendelea kuuza kuliko magazeti yote nchi hii mpaka tuwe serious.......
 
...JAMAA AME''GAMBLE''...labda baada ya uchaguzi awe tena dhidi ya serikali ndiyo biashara yake ya magazeti itaflourish,maana kwasasa anachofanya ni kazi ya Uhuru, Mzalendo na Habari Leo(Magazeti yanayoendeshwa kwa Ruzuku )..Kila wiki nilikuwa sikosi magazeti yake..ila kwa sasa yamekaa kipropaganda zaidi....Ndio maana nasema wakenya na Gazeti lao(MWANANCHI) wataendelea kuuza kuliko magazeti yote nchi hii mpaka tuwe serious.......

Mwananchi nalo linashabikia Ukawa silioni kama liko neutral.
 
Huu ni upuuzi wa kutaka magazeti yote yaimbe wimbo wa Mwanahalisi, Tanzania Daima, Mawio, Mtanzania na hata nipashe.

Hilo gazeti linaandika ukweli ndio maana nyie mnalishupalia, maana linagonga kwenye mfupa.

Kwa nyie ambao mpo tayari kuchagua hata maiti au jiwe basi sio Saizi yenu, nyie someni hayo hapo juu ambayo ni vigumu kutofautisha Tanzania Daima, Mawio, Mtanzani na Uhuru.

Raia MWEMA ndipo Gazeti ambalo sikosi kulinunua, Nenda hata kwenye website yao angalia views, wakati mwingine makala moja inasomwa na watu Hadi elfu ishirini.

Wenye akili wanaelewa sio wote wanaweza kuburuzwa na Pesa za Lowassa.

Shida ya hapa kwetu ukiwa na upande kwenye siasa uhakikishe 'predictability' ya siasa yenyewe. Ikitokea baada ya kuchukua upande na huo upande ukianza kuonyesha madudu wewe ambaye ulibeba huo upande na wewe una'share' blame/take responsibility. Vyombo vyetu vya habari vinakuwa na upande, lakini havikubali ku'share' blame au take responsibility.
 
Mwananchi nalo linashabikia Ukawa silioni kama liko neutral.

taja habari yoyote(kwa ushahidi) inayoonesha inashabikia/kuipendelea Chadema...
Yapo magazeti yanayo side na vyama yanajulikana....(mawio,mwanahalisi,tanzania daima nk-Ukawa)
(uhuru,habarileo,raia tz,raia mwema,jamba leo nk-CCM/Magufuli)..........
 
...JAMAA AME''GAMBLE''...labda baada ya uchaguzi awe tena dhidi ya serikali ndiyo biashara yake ya magazeti itaflourish,maana kwasasa anachofanya ni kazi ya Uhuru, Mzalendo na Habari Leo(Magazeti yanayoendeshwa kwa Ruzuku )..Kila wiki nilikuwa sikosi magazeti yake..ila kwa sasa yamekaa kipropaganda zaidi....Ndio maana nasema wakenya na Gazeti lao(MWANANCHI) wataendelea kuuza kuliko magazeti yote nchi hii mpaka tuwe serious.......



Jenerali labda kuna kitu anakijua...hatukijui
sababu hii 'fear ya Lowassa' mwisho watu wataipa CCM kura za bure bila hata
kuibana kidogo kujua kama wanastahili kweli kupewa nafasi....
 
ANakumbuka cha moto alichokipata alipoambiwa ni mnyarwanda. Anajitekenya akcheke aongeze dakika ya kuishi. Mwacheni ataumbuka mwenyewe. Hana lolote siku hizi, alikuwa mchambuzi mzuri wakati wa chama kimoja na amezeeka akili zake kwa sasa ndio maana hata hasikiki kama zamani
 
Back
Top Bottom