Elections 2010 Raia Mwema: Dk Slaa awataka Duni, Hamad wa CUF

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Raia Mwema: Slaa awataka Duni, Hamad wa CUF

Baada ya mgombvea urais kupitia Chadema, Dk W. Slaa kubadili upepo wa kisiasa nchini kuelekjea uchaguzi mkuu mwaka huu, chama hicho sasa kimo katika mkakati mahsusi wa kumpata mgombea mwenza mwenye ushawishi mkubwa kuroka kutoka CUF, Raia Mwema imethibitishiwa.

Habari za uhakika kutoka Chadema na CUF zimethibitisha kwamba mazungumzo yasiyo rasmi yamekwisha kuanza pamoja na kuwa tayari m,ajina mazito ya wanasiasa kutoka Zanzibar yameanza kutajwa kuombwa kuwa pamoja na Dk Slaa katika uchaguzi huo wa Oltoba 31.

Wanaotajwa ni pamoja na Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Juma Duni Haji na aliyekuwa Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed, ambao wote ni watu wenye ushawishi mkubwa katika siasa za Visiwani na Bara.

Duni ambaye tayari CUF imemteua kuwa mgombea mwenza wa Preof Ibrahim Lipumba, anayebeba kwa mara ya nne bendera ya chama hicho katika kuwania urais, anatajwa kutakiwa na Chadema kutokana na ushawishi wake ndani ya siasa za Zanzibar na hata Bara.

Kwa mujibu wa habari hizo, kukubali kwa Duni kutategemea zaidi msimamo wa chama chake katika kumuunga mkono Dl Slaa, hatua ambayo imeelezwa kuanza kujadiliwa katika vikao visivyo rasmi kabla ya kuingia katika vikao rasmi vya vyamna hivyo ili hatimaye kufikia uamuzi.

Mwaka 200 Chadema walimuunga mkono mgombea urais wa CUF, Prof Lipumba, ambako katika mikutano yake nchi nzima alisimama kuwapigia debe wagombea wa Chadema na CUF huku mitandao ya vyama hivyo ikitumika katika harakati za kampeni hizo, hali ambayo inaelezwa kupendekezwa kuwapo katika katika uchaguzi wa mwaka huu.

Kwa upande wa Hamad Rashid, anatajwa kama ni mtu aliye karibu na Dk Slaa wakiwa wamefanya kazi kwa muda mrefu bungeni katika ofisi ya Kambi ya Upinzani, na anatajwa kuwa mmoja wa wanasiasa waliomshawishi mwanasiasa huyo wa Chadema kuwania urais.

….Habari zaidi katika Raia Mwema ya leo – mwenye full soft copy yake atuwekee tafadhali.


My take:

This story is too good to be true, though it has certain convincing elements. Can that be possible?
 
Nianze na Malaria Sugu -- unao wimbo hapa? Nakushauri nawe ufikirie kuhamia Chadema -- ondokana na genge la mafisadi unaloliteteam kila kukicha pasipo hoja za msingi. Vuka mstari na uingie upande wa haki -- achana na kulamba m..... ya hao akina RA na wengine. Usichelewe, wakati ni huu.
 
Hizi ni habari njema pia,tumombee kwa mwenyenzi mungu atupe Mh Hamad Rashi - JEMBE,Toka Visiwa vya Unguja ili wamalize kazi ya kuangusha mbuyu Tanzania.
Go Dr Slaa,
Wellcome Hamad Rashid.

Ushauri kwa Mh Hamd Rashid-Wasilikize watanzania wanataka nini na wewe kama umepata nafasi ya kuombwa tekeleza ushauri wa walio wengi.umeshakuwa chaguo la wengi ndio chaguo la Mungu.Tuache ushabiki wa vyama na itkadi hizi tuziweke pembeni kwanza tutazungumza baada ya uchaguzi.
I salute you all JF's
 
tumaini hapo umeharibu yaani kumbe bado una siasa za kidini ndugu yangu usiwe hivyo pevuka akili toa mawazo ya kujenga.usipotoshe umma wa Watanzania ss tunataka mabadiliko sio siasa za kidini.
 
i would love to see the deal struck like that ingawa wana cuf cjui kama nia yao pekee ni kuiangusha ccm!
 
Binafsi ningefurahi sana kama CUF na CHADEMA wangeungana au Mhe. Duni na Rashid wakijiunga CHADEMA basi kwa % kubwa ushindi wa CHADEMA upo nje. Mungu atasikia kilio chetu na hawa wataona sababu ya kujiunga au CUF kumwunga mkono Dk Slaa. CUF inapaswa kuonyesha uzalendo wa kweli kwa maslahi ya nchi na watu wake kama CHADEMA walivyofanya mwaka 2000. God bless Dk Slaa
 
Watakuwa wanafanya kosa lile walilofanya wazee wa Dar enzi za mkoloni za kumkaribisha mchonga baada hapo wakatengwa na safari ya kubatiza nchi ikaanza rasmi. CUF nendeni mkajipendekezi kwa padre itakuwa ni kosa ambalo hamtalisahau... BIG NO kwa padre kuwa rais..
Huyu sasa amezidi kila threadi na kila posti anachafua. Sasa tafakuri nzuri za wengine tutazisoma muda gani? Hakuna sasa hiyo nafasi.
 
Hii ni swala ambalo tumekuwa tukilijadili kwenye thread nyingine kabla ya hizi habari. Kwa kweli ni habari nzuri inabidi Cuf watumie busara kama ambavyo walivyoonyesha Znz kwenye muafaka sasa baada ya Cuf kuwa na muafaka na Ccm imefika wakati kuwa na 'Mseto' na Chadema kwa uchaguzi wa 2010. Ajenda kuu ziwe;

Kumuunga mkono Dr Slaa na wao kuwatoa wagombea wao Lipumba na Duni.
Kukubali kuwa Hamad awe mgombea mwenza wa Dr Slaa kwenye uchaguzi mkuu

Hii itakuwa timu nzuri mbadala kwa wapiga kura wote wa Tz.

Kwa wewe Tumain swala kuwa Dr Slaa ni padre/mchungaji whatever si hoja kwa vile ni wazi katiba na nchi yetu ni sekula na hatujali dini ya mtu, labda kama wewe ni mfahidhina uliobobea.
 
Hadi sasa katika wachangiaji 12 waliochangia topic hii ni mmoja tu -- Tumain -- bila shaka nduguye MS -- ndiye mwenye mawazo tofauti. Hana aliyemuunga mkono. Mchafuzi tu huyu -- hata kama ni demokrasia -- kashindwa vibaya sana! Haoni hata aibu! Anatala kutuchafulia mpiganaji wetu kwa tuhuma za kidini! Bila shaka ametumwa na CCM ambao Dr Slaa amewasha moto ndani ya chupi zao!
 
Hizi ni habari njema pia,tumombee kwa mwenyenzi mungu atupe Mh Hamad Rashi - JEMBE,Toka Visiwa vya Unguja ili wamalize kazi ya kuangusha mbuyu Tanzania.
Go Dr Slaa,
Wellcome Hamad Rashid.

Ushauri kwa Mh Hamd Rashid-Wasilikize watanzania wanataka nini na wewe kama umepata nafasi ya kuombwa tekeleza ushauri wa walio wengi.umeshakuwa chaguo la wengi ndio chaguo la Mungu.Tuache ushabiki wa vyama na itkadi hizi tuziweke pembeni kwanza tutazungumza baada ya uchaguzi.
I salute you all JF's

Huu ndio wakati wa vyama kuunganisha nguvu.

CUF na wagombea wengine, wataelewa picha hii kubwa.... Kila la kheri katika ushirikiano.
 
Duni ni mgombea wa CUF tayari, mnategemea ataacha tiketi ya CUF kufuata CHADEMA ?

Hamad hana ushawishi kihivyo Zanzibar.

Regardless, tunarudi kule kule katika siasa zetu kuzunguka katika personalities badala ya policies, kama kuna hii meeting of minds kati ya CUF na CHADEMA, kama policies zinalingana si waungane tu ? This way CUF isiyo na nguvu sana kama CHADEMA bara itafaidika kwa kupata ufuasi zaidi bara na CHADEMA isiyo na ushawishi kama CUF visiwani itafaidika kupata ushawishi zaidi.

Ikumbukwe hata CCM imeweza kupata ushawishi Tanzania kwa kuunganisha TANU na ASP, kabla ya muunganisho huu kulikuwa hakuna chama cha siasa chenye ushawishi Tanzania nzima. Hii ndiyo nature ya politics za Tanzania, bila kuunganisha vyama tutabaki na vyama vya bara na vya visiwani tu, na CCM by virtue of being the eldest and a united front itakuwa na advantage ya kuwa the only national party.
 
Hii ni habari njema kuelekea ukombozi wa nchi yetu kutoka mikononi mwa wakoloni weusi (CCM). Tatizo ni kuwa tayari kuna mkono wa TISS kupitia hoja ya udini.Kwa mtazamo mwepesi tunaweza kuwaona hawa wenzetu kina hope na homa kama ni wadini tu, lakini nyuma yao ni mpango mahsusi wa UWT kuzigawa kura,ili kumpa ahueni kifa ulongo.Watanzania tuamke tusikubali kugawanywa ili tutawaliwe.UDINI NI SUMU MBAYA TUIKATAE.
 
Back
Top Bottom