Rai: Serikali isitishe uuzaji nafaka nje ya nchi: Hali siyo shwari, Gunia la mahindi limefikia 100,000/= kanda ya Ziwa.

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
Nimefanya utafiti mdogo ktk maeneo mbalimbali hapa nchini kuhusu bei za vyakula hasa nafaka aina ya mahindi na mchele.
1. Kanda ya Kaskazini, maeneo mengi ya Mkoa wa Kilimanjaro, Arusha na Manyara bei ya mahindi imefikia hadi 120,000/= kwa gunia la kg 100. Bei inaendelea kuongezeka.Hii ni kutokana na mvua za masika kukatika mapema.
2. Kanda ya Ziwa kwa mikoa ya Shinyanga na Mwanza, gunia la mahindi ni Tsh 100,000/= na bei inaongezeka kwa kasi. Bei ya mchele ni Tsh 1500/= hado 2000/= kwa kilo na bei inapanda kwa kasi.
Baadhi ya wafanyabiashara wamedai kuwa mazao hayo mawili mahindi na mpunga uzalishaji wake ulikuwa mdogo mwaka huu kwa baadhi ya maeneo.
Hivi karibuni, kupitia vyombo vya habari, taarifa zimetolewa na mamlaka husika kuwa mipaka iko wazi kupitisha mazao kuuza nje ya nchi. Hili ni jambo jema, lakini tuhakiki kiasi kilichopo maeneo mbalimbali kwanza. Lengo liwe ni kuhakikisha maeneo yenye upungufu kama niliyotaja,yanasambaziwa kwanza kabla ya kuruhusu mahindi hayo kwenda nje.
Sipingani na mipango ya Serikali kuruhusu mipaka kuwa wazi, lakini iwe ni baada ya kujiridhisha kuwa mikoa yote nchini haina uhaba, na bei yake inakuwa reasonable fair!
Mfano bei ya Mahindi Rukwa na Songea ni Tsh 50,000 hadi 55,000/= kulingana na utafiti wangu wa wiki hii.
Si ajabu kutokana na tamaa ya wafanyabiashara wetu kutaka faida kubwa yakapelekwa nje ya nchi na siyo kanda ya Ziwa au Kanda ya Kaskazini. Hivyo, udhibiti wa Serikali ni muhimu sana.
 
Nyie ni vigegeu, tafuta humu kuna thread kibao za kuilaumu serikali kwa kuzuia kuuza nafaka nje ya nchi hadi bei ya gunia ikafika 20,000/=, na mkasema wakulima wanaumizwa, sasa wameruhusu mnalalamika tena kwamba bei ya nafaka ipo juu. Nadhani wale wakulima walioumia kwa kuuza gunia 20,000/= waachwe sasa wajipoze vidonda na maumivu waliyoyapata, huu ni muda wao!
 
Muwe mnaishauri serikali i-regulate na bei ya pembejeo/dawa etc siyo watu wanapigika wenyewe halafu mnakuja kuwapangia pa kuuzia.

Mbolea fake, pesticides fake mfn viwavijeshi mpaka sasa taasis zote za utafiti hazijaja na suluhisho lkn hakuna aliyepaza sauti mnasubiri kupangia watu masoko.

Acha ipande na mipaka isifungwe tu.
 
Huwa nashangaa sana watu wanapotaka misiba yao watu wote walie,mkulima wa watu kapambana ajuavyo kupata mavuno halafu eti asiuze nje kisa we una njaa? Kama una njaa nunua kwa bei anayopewa kule nje uone kama atapeleka huko.
Nchi hii hatuna upungufu wa chakula ila watu wake wana uhaba wa hela ya kununulia chakula. Lini umewahi kwenda sokoni ukaambiwa hakuna mahindi? Kinachotokea bei hupanda kutokana na uhaba ambao husababishwa na soko duni hivyo wakulima hupeleka mazao kwny masoko bora yanayowalipa vizuri sasa kama mtu hana hela ya kumudu chakula asilaumu wakulima.
Muwe mnaishauri serikali i-regulate na bei ya pembejeo/dawa etc siyo watu wanapigika wenyewe halafu mnakuja kuwapangia pa kuuzia.

Mbolea fake, pesticides fake mfn viwavijeshi mpaka sasa taasis zote za utafiti hazijaja na suluhisho lkn hakuna aliyepaza sauti mnasubiri kupangia watu masoko.

Acha ipande na mipaka isifungwe tu.
 
Nimefanya utafiti mdogo ktk maeneo mbalimbali hapa nchini kuhusu bei za vyakula hasa nafaka aina ya mahindi na mchele.
1. Kanda ya Kaskazini, maeneo mengi ya Mkoa wa Kilimanjaro, Arusha na Manyara bei ya mahindi imefikia hadi 120,000/= kwa gunia la kg 100. Bei inaendelea kuongezeka.Hii ni kutokana na mvua za masika kukatika mapema.
2. Kanda ya Ziwa kwa mikoa ya Shinyanga na Mwanza, gunia la mahindi ni Tsh 100,000/= na bei inaongezeka kwa kasi. Bei ya mchele ni Tsh 1500/= hado 2000/= kwa kilo na bei inapanda kwa kasi.
Baadhi ya wafanyabiashara wamedai kuwa mazao hayo mawili mahindi na mpunga uzalishaji wake ulikuwa mdogo mwaka huu kwa baadhi ya maeneo.
Hivi karibuni, kupitia vyombo vya habari, taarifa zimetolewa na mamlaka husika kuwa mipaka iko wazi kupitisha mazao kuuza nje ya nchi. Hili ni jambo jema, lakini tuhakiki kiasi kilichopo maeneo mbalimbali kwanza. Lengo liwe ni kuhakikisha maeneo yenye upungufu kama niliyotaja,yanasambaziwa kwanza kabla ya kuruhusu mahindi hayo kwenda nje.
Sipingani na mipango ya Serikali kuruhusu mipaka kuwa wazi, lakini iwe ni baada ya kujiridhisha kuwa mikoa yote nchini haina uhaba, na bei yake inakuwa reasonable fair!
Mfano bei ya Mahindi Rukwa na Songea ni Tsh 50,000 hadi 55,000/= kulingana na utafiti wangu wa wiki hii.
Si ajabu kutokana na tamaa ya wafanyabiashara wetu kutaka faida kubwa yakapelekwa nje ya nchi na siyo kanda ya Ziwa au Kanda ya Kaskazini. Hivyo, udhibiti wa Serikali ni muhimu sana.
True!
 
wacha roho mbaya dhidi ya wakulima wetu! hiyo 100,000/= kama ni nyingi sana kwako nenda KALIME mahindi yako.
Hakuna mwenye roho mbaya labda hujaelewa vzr hii mada.
Serikali imeshusha bei ya pembejeo( mbolea), lengo ni ili kuwe na mlinganyo mzuri wa gharama za uzalishaji na bei ya mazao.
Ingekuwa ni roho mbaya isingeweka hizo ruzuku? Na pia siyo vibaya kuona kunakuwa na fairness kwenye bei za kuuza mazao. Mfano Pamba, Korosho, Kahawa nk serikali imefanya.
Kama ilivyo kuwa hatuwezi kuacha mkulima apunjwe bei, vivyo hivyo,tusiache mlaji alanguliwe!
 
Waendelee kuunga mkono na miguu,juhudi za utendaji wangu,nitawaletea mahindi.
 
wacha roho mbaya dhidi ya wakulima wetu! hiyo 100,000/= kama ni nyingi sana kwako nenda KALIME mahindi yako.
Hawa jamaa wanataka kuhujumu bei ya Mahindi

Ishuke hadi elfu 20 ili wafurahi bila kuangalia mkulima anaathirikaje na bei kuwa ndogo
 
Hapa naipongeza serikali ya awamu ya tano kwa hili kwa masikio yangu JNICC nilimsikia Waziri wa kilimo akihaidi kutoingilia biashara ya nafaka wala kufunga mipaka, kama unaona wakulima wanafaidi sana kalime ww au kanunue hayo mazao upeleke huko kwenye uhaba
 
Nimefanya utafiti mdogo ktk maeneo mbalimbali hapa nchini kuhusu bei za vyakula hasa nafaka aina ya mahindi na mchele.
1. Kanda ya Kaskazini, maeneo mengi ya Mkoa wa Kilimanjaro, Arusha na Manyara bei ya mahindi imefikia hadi 120,000/= kwa gunia la kg 100. Bei inaendelea kuongezeka.Hii ni kutokana na mvua za masika kukatika mapema.
2. Kanda ya Ziwa kwa mikoa ya Shinyanga na Mwanza, gunia la mahindi ni Tsh 100,000/= na bei inaongezeka kwa kasi. Bei ya mchele ni Tsh 1500/= hado 2000/= kwa kilo na bei inapanda kwa kasi.
Baadhi ya wafanyabiashara wamedai kuwa mazao hayo mawili mahindi na mpunga uzalishaji wake ulikuwa mdogo mwaka huu kwa baadhi ya maeneo.
Hivi karibuni, kupitia vyombo vya habari, taarifa zimetolewa na mamlaka husika kuwa mipaka iko wazi kupitisha mazao kuuza nje ya nchi. Hili ni jambo jema, lakini tuhakiki kiasi kilichopo maeneo mbalimbali kwanza. Lengo liwe ni kuhakikisha maeneo yenye upungufu kama niliyotaja,yanasambaziwa kwanza kabla ya kuruhusu mahindi hayo kwenda nje.
Sipingani na mipango ya Serikali kuruhusu mipaka kuwa wazi, lakini iwe ni baada ya kujiridhisha kuwa mikoa yote nchini haina uhaba, na bei yake inakuwa reasonable fair!
Mfano bei ya Mahindi Rukwa na Songea ni Tsh 50,000 hadi 55,000/= kulingana na utafiti wangu wa wiki hii.
Si ajabu kutokana na tamaa ya wafanyabiashara wetu kutaka faida kubwa yakapelekwa nje ya nchi na siyo kanda ya Ziwa au Kanda ya Kaskazini. Hivyo, udhibiti wa Serikali ni muhimu sana.
Naunga mkono hoja hili la kutofautina bei kiasi kikubwa hivyo ndani ya nchi moja sidhani kama ni fair. Pengine mipaka ifungwe kwa muda kupunguza makali kwa hawa wananchi au wafanyabiashara waruhusiwe kwenda kununua huko nyanda za juu kusini peke yake la sivyo inaweza ibuka njaa kwa baadhi ya mikoa.
 
Acheni wakulima wanemeeke
Nimefanya utafiti mdogo ktk maeneo mbalimbali hapa nchini kuhusu bei za vyakula hasa nafaka aina ya mahindi na mchele.
1. Kanda ya Kaskazini, maeneo mengi ya Mkoa wa Kilimanjaro, Arusha na Manyara bei ya mahindi imefikia hadi 120,000/= kwa gunia la kg 100. Bei inaendelea kuongezeka.Hii ni kutokana na mvua za masika kukatika mapema.
2. Kanda ya Ziwa kwa mikoa ya Shinyanga na Mwanza, gunia la mahindi ni Tsh 100,000/= na bei inaongezeka kwa kasi. Bei ya mchele ni Tsh 1500/= hado 2000/= kwa kilo na bei inapanda kwa kasi.
Baadhi ya wafanyabiashara wamedai kuwa mazao hayo mawili mahindi na mpunga uzalishaji wake ulikuwa mdogo mwaka huu kwa baadhi ya maeneo.
Hivi karibuni, kupitia vyombo vya habari, taarifa zimetolewa na mamlaka husika kuwa mipaka iko wazi kupitisha mazao kuuza nje ya nchi. Hili ni jambo jema, lakini tuhakiki kiasi kilichopo maeneo mbalimbali kwanza. Lengo liwe ni kuhakikisha maeneo yenye upungufu kama niliyotaja,yanasambaziwa kwanza kabla ya kuruhusu mahindi hayo kwenda nje.
Sipingani na mipango ya Serikali kuruhusu mipaka kuwa wazi, lakini iwe ni baada ya kujiridhisha kuwa mikoa yote nchini haina uhaba, na bei yake inakuwa reasonable fair!
Mfano bei ya Mahindi Rukwa na Songea ni Tsh 50,000 hadi 55,000/= kulingana na utafiti wangu wa wiki hii.
Si ajabu kutokana na tamaa ya wafanyabiashara wetu kutaka faida kubwa yakapelekwa nje ya nchi na siyo kanda ya Ziwa au Kanda ya Kaskazini. Hivyo, udhibiti wa Serikali ni muhimu sana.
 
Kwa taarifa yako kama kuna wakulima wanaouza nafaka nje ya nchi ni wachache sana. Wafanya biashara ndio wananunua kwa wakulima, tena tu baada ya kuvuna na kuhifadhi. Sasa hivi wao ndio wanauza nje ya nchi na soko la ndani, mkulima hafaidiki kwa lolote kwa hii ruhusa ya kuuza nje. Sasa hivi kwa kweli hali imeshaanza kuwa tishio hasa kanda ya ziwa.
Nyie ni vigegeu, tafuta humu kuna thread kibao za kuilaumu serikali kwa kuzuia kuuza nafaka nje ya nchi hadi bei ya gunia ikafika 20,000/=, na mkasema wakulima wanaumizwa, sasa wameruhusu mnalalamika tena kwamba bei ya nafaka ipo juu. Nadhani wale wakulima walioumia kwa kuuza gunia 20,000/= waachwe sasa wajipoze vidonda na maumivu waliyoyapata, huu ni muda wao!
 
Back
Top Bottom