Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Salam Wana JF
Kuna rafiki yangu wa karibu ambaye tumeshibana sana, toka ameoa sasa ni mwezi wa 5 , Jana nilikuwa naye akanieleza matatizo anayoyapata toka kwa mkewe. Aliniambia kuwa anajitahdi sana kumridhisha mkewe kwa tendo la ndoa, lakini huyu mke wake amekuwa akitaka sana mchezo kuzidi uwezo wake.
Kila mara mkewe anataka. Akikaa kuangalia tv sitting room mkewe huwa anamvutia chumbani na kumtaka ampe raha, Akimwambia amechoka, mkewe huwa analalamika sana, mara nyingine hulalamika kwa sauti kubwa mpaka rafiki yangu anahofia majirani wasije kusikia. Sasa hili jambo limekuwa kero mpaka siku hizi amebuni safari za mikoani na kumdanganya mkewe anasafiri kikazi ili aepukane na balaa la nyumbani. Kiukweli huwa haendi mikoani bali anakwenda gest kulala mpaka akijisikia ndio anarudi nyumbani na kuzuga anatoka mkoani.
Ameniomba nimpe ushauri afanye nini ili aweze kusolve hili tatizo, Wana Jf nimekuja kwenu kupata ushauri wenu ili niweze kumsaidia
Kuna rafiki yangu wa karibu ambaye tumeshibana sana, toka ameoa sasa ni mwezi wa 5 , Jana nilikuwa naye akanieleza matatizo anayoyapata toka kwa mkewe. Aliniambia kuwa anajitahdi sana kumridhisha mkewe kwa tendo la ndoa, lakini huyu mke wake amekuwa akitaka sana mchezo kuzidi uwezo wake.
Kila mara mkewe anataka. Akikaa kuangalia tv sitting room mkewe huwa anamvutia chumbani na kumtaka ampe raha, Akimwambia amechoka, mkewe huwa analalamika sana, mara nyingine hulalamika kwa sauti kubwa mpaka rafiki yangu anahofia majirani wasije kusikia. Sasa hili jambo limekuwa kero mpaka siku hizi amebuni safari za mikoani na kumdanganya mkewe anasafiri kikazi ili aepukane na balaa la nyumbani. Kiukweli huwa haendi mikoani bali anakwenda gest kulala mpaka akijisikia ndio anarudi nyumbani na kuzuga anatoka mkoani.
Ameniomba nimpe ushauri afanye nini ili aweze kusolve hili tatizo, Wana Jf nimekuja kwenu kupata ushauri wenu ili niweze kumsaidia