Radio Tumaini fanyeni 'review' vipindi vya kijamii

MTAZAMO

JF-Expert Member
Feb 8, 2011
19,643
33,439
Wakuu,

Kama mnavyojua JF ni kisemeo chetu na imesaidia kuleta mabadiliko mengi. Niliwahi kuanzisha uzi hapa kushauri radio za Kikatoliki na kupitia uzi ule kuna mabadiliko yamefanyika na moja wapo ni kurasa za mitandao ya kijamii ya radio Tumaini ku improve! Kasi bado ni ndogo kulinganisha na Radio Maria lakini kuna mwendo.

Leo nimeona nishauri mambo mengine kuboresha radio Tumaini. Kwasasa kuna kampeni ya kuchangia radio/TV Tumaini na nimesikiliza father Massenge akifafanua changamoto za uendeshaji hadi nikajisikia vibaya! Tujitahidi kuchangia kurahisisha uinjilishaji.

Lakini ni muhimu radio Tumaini wabadilike pamoja na vipindi vingi vizuri lakini bado wanafanya vipindi kama radio Tanzania! Hivi nani zama hizi anasikiliza vipindi vya salamu tena usiku? Nani anasikiliza ngoma za asili zama hizi? Hayo achieni idhaa ya Taifa wanaoishi kwa ruzuku.

Radio Tumaini kuna asilimia ya vipindi vya kijamii sio dini tu lakini kwa hizo asilimia ndogo fanyeni vipindi ambavyo hata idara yenu ya marketing wanaweza kutafuta sponsors.

Usiku watu wamelala kama hakuna mahubiri basi wekeni hata nyimbo za dini kuliko kutuma salamu mambo ambayo hata radio zingine walishaacha!Karistimatiki chini ya utume wa walei mnaweza kuwapa wafanye night shift itaongeza wasikilizaji.

Vipindi vya kijamii visivyo na tija ni mzigo tu bora iwe radio ya dini fully kuliko hivi! Sponsors zimejaa shule na vyuo vya ufundi sababu ya jinsi mnavyoendesha vipindi kizamani na hambadiliki.

Ushauri, Kanisa limejaa manguli wa kuendesha radio na social media kwa mafanikio mf Millard Ayo, Sebastian Maganga, Francis Chiza n.k. Waiteni muwape kazi ya kusikiliza na kuwashauri hasa uendeshaji wa vipindi vya kijamii na mitandao ya kijamii ili vivutie sponsors otherwise mtakuwa mnalipia leseni bure!

Nimemsikia Basil Mbakile kwenye habari, mtumieni vizuri kwenye maboresho ni fundi aliyefanya kwenye radio za kisasa ikiwemo East Radio na Tv.

Mwisho kwa waamini Wakatoliki, tujitahidi kuchangia media zetu kazi ya injili isonge mbele! Ni wajibu wetu.

Mwenye access na father Massenge Mkurugenzi wa Radio Tumaini amfikishie hii.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
RC always ni consevative.
Mambo mengine Ina bidi ku change kdgo,TV Tumaini nayo Bado sana wajifunze kwa Upendo TV
Mfano tuna vyama vya kitume moto sana kama Moyo Mtakatifu wa Yesu, Damu Takatifu ya Yesu, Karistimatiki Katoliki wote hawa wangetumika kuhubiri. Watu wana kiu na kuhubiriwa neno la Mungu kwa kina! Ila wanaendesha vipindi vya kijamii kizamani sana bora wangefanya vya dini tu maana havina tija.

Mimi ni msikilizaji mkubwa wa radio Tumaini lakini usiku zikianza salamu inabidi ubadili stations au uzime kabisa. Mtu unatamani ulale na mambo ya kiroho lakini watu wanakesha na salamu! Haina tija hata kidogo na watuma salamu ni walewale usiku kucha kila siku.

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Ila watafute pesa walipe wanazodaiwa nimesikia kuna deni la million 160+. Waache kutafuta huruma na sadaka.

Wabuni vyanzo na vipindi vitakavyokuza mapato na redio kujiendesha yenye.

Waombe jimbo kuu liwape pesa ya kulipa kupitia sadaka tunazotoa
 
Binafsi Radio na TV tumaini ikitokea nimesikiliza ni kwa bahati mbaya,kuna siku nimetoa maoni abt maboresho nilijibiwa kwa jibu la kutimuliwa ka nyau wa mjumbe!

TV limejaa marudio, rangi mbovu, nyimbo nyingi hazieleweki. Katoliki mlivyo tajiri wa lot of songs Tumaini wamekomaa na nyimbo za low quality?

Mbona Radio Maria wapo vzr sana na now wapo mikoa yote??

Wabadilike, wanapoteza muda as watazamaji wengi wapo Upendo kwa Walutheli uko
 
Binafsi Radio na TV tumaini ikitokea nimesikiliza ni kwa bahati mbaya,kuna siku nimetoa maoni abt maboresho nilijibiwa kwa jibu la kutimuliwa ka nyau wa mjumbe!

TV limejaa marudio, rangi mbovu, nyimbo nyingi hazieleweki. Katoliki mlivyo tajiri wa lot of songs Tumaini wamekomaa na nyimbo za low quality?

Mbona Radio Maria wapo vzr sana na now wapo mikoa yote??

Wabadilike, wanapoteza muda as watazamaji wengi wapo Upendo kwa Walutheli uko
Kwakweli ni aibu, hadi akina Sunguye wana TV why Kanisa kubwa kama Katoliki tusuesue. Sometimes tutalaumu waamini bure wakati vyombo vyenyewe vinaendeshwa kimazoea.

Sasa hivi hata magazeti ya Tumaini yanauzwa jumuiya kama sadaka tena kila wiki unatumiwa tu gazeti uchangie, hii haiwezi kudumu namna hii. Ni kweli ni muhimu kuchangia lakini bado media za Kikatoliki haziko vibrant na hazibebi maudhui yanayovutia.

Hutusemi wawe na vipindi kama Clouds fm ila watimize kiu za watu hasa mahubiri! Watu wana kiu na mambo ya kiroho. Tuna walei, vyama vya kitume, na mapadri wenye kiu ya kuhubiri wapewe nafasi za kutosha tusikie habari za Mungu!

Watu wakimsikia Mungu vya kutosha hata michango watapata hadi kutoka madhehebu mengine kwa kuguswa! Kanisa limejaa utajiri wa historia, shuhuda, miujiza, na umisionari mkubwa lakini hazisikiki kwenye hizo media! Vipindi vinarudiwa, wakati mwingine quality mbovu n.k

Hebu shirikisheni walei waliobobea huko wawasaidie kuboresha uendeshaji wa vipindi badala ya kutobadilika! Hata RTD wanabadilika siku hizi.



Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom