Radio Free Africa mna shida gani??

Radio Free Africa mna shida gani??

Madeni madeni Kiongozi..Si CCM wala Viongozi wake waandamizi(majority) hawawezi kuendesha wala kusimamia chochote
1.Sukita chali
2.Shule za CCM chini ya Jumuiya ya Wazazi chalii
3.Mradi wa mabasi ya Wanafunzi DSM chali
4.TAZARA chalii
5..BRT chali
6..Hivyo vyombo vya Habari vya Chama dhoofu lihali
 
Ni wiki sasa nikifungulia radio yenu kusikiliza vipindi vya asubuhi vya magazeti na matukio nakutana na miziki na matangazo ya biashara tu. Kulikoni???
Radio Free Africa na Azam Tv ni mapacha wenye aleji na mvua, hivi vituo viwili havipatani na mvua kwani kukiwa na mvua matangazo yake hukatika. RFA magazeti husomwa toka Dar es Salaam Kinondoni huku wakiunganishwa na kituo kikuu cha kurusha matangazo kilichoko Mwanza lakini kukiwa na mvua mawasiliano hukatika na tatizo hili lipo tangu RFA ilipoanzishwa na kwa miaka yote wameshindwa kulitatua tatizo hilo vivyo hivyo na Azam Tv nayo mvua ikinyesha matangazo husikia baridi na kutetemeka! Nao tangu kituo kianze wameshindwa kulitatua tatizo hilo kutokana na vifaa wanavyotuuzia kuwa ni vya hali ya chini sana kiasi inawalazimu watumie gharama kuvifanyia matengenezo bure! Hii si bure kwani mwisho wa siku mteja unaambiwa ununue kingine ambacho nacho hakitadumu huku TBS( Mamlaka ya Viwango) ikiwagwaya.
 
Hii ndo Redio yangu bora kwa vipindi vya asubuhi hasa DW na Magazeti lakini hata mimi nashangaa wiki nzima wanaweka muziki tu mara matangazo yakate inakua kimya.

Dialo kama kashijdwa bora aiuze kwa Jambo.
 
Ni wiki sasa nikifungulia radio yenu kusikiliza vipindi vya asubuhi vya magazeti na matukio nakutana na miziki na matangazo ya biashara tu. Kulikoni???
hii redio inayumba sana, mara wapotee hewani kwenye masafa yao
 
Ni wiki sasa nikifungulia radio yenu kusikiliza vipindi vya asubuhi vya magazeti na matukio nakutana na miziki na matangazo ya biashara tu. Kulikoni???
Leo wamenikumbusha mbali kweli. Wamepiga ule wimbo wa "Kinshasa Malembe....! wa Zaiko Langa Langa! Magazeti na matukio hamne! Nisingelikuwa mstaarabu, ningelisema RFA wamefanya makusudi tusisikie mambo ya G55 ya Chadema! Ahahahahaha!!
 
Hii ndo Redio yangu bora kwa vipindi vya asubuhi hasa DW na Magazeti lakini hata mimi nashangaa wiki nzima wanaweka muziki tu mara matangazo yakate inakua kimya.

Dialo kama kashijdwa bora aiuze kwa Jambo.
Jambo 106.9 fm Mwanza
Mapinduzi ya tasnia ya radio nchini Tanzania, kwa mwanzo huu naimani kubwa ya kuwarudisha watu katika kisikiliza redio kama ilivyokuwa miaka ya 90-2000 kupitia Jambo fm,, wamejipanga vizuri sana,, nawatakia kila lenye kheri kwao,,
 
Jambo 106.9 fm Mwanza
Mapinduzi ya tasnia ya radio nchini Tanzania, kwa mwanzo huu naimani kubwa ya kuwarudisha watu katika kisikiliza redio kama ilivyokuwa miaka ya 90-2000 kupitia Jambo fm,, wamejipanga vizuri sana,, nawatakia kila lenye kheri kwao,,
hii jambo fm ni yule mtengeneza juisi za jambo? Redio inapiga muziki tu, naona iko kwenye majaribio, inapasua anga mpaka ukanda wa kati
 
Back
Top Bottom