Rada kuu ya Tanzania ni mbovu.

Wamalawi wameiharibu hatuwawezi wameshaanza

inteli-jinsia ya (ke) ya Joyce B inaonekana kufanya kazi vema, hatutakuwa na uwezo wa kumzuia yule mmalawi ku-hit magogoni na viunga vyake i.e ilala migomigo, upanga kwa mama jeni*** kurasini, gomz, lugalo***

waliotununulisha hii kitu napendekeza wapimwe kubaini kama ni waumini itikadi ya D. Cameroon.
 
Mi natamani hata dege likosee njia li ingie magogoni pale kwenye pango la wanyang'anyi halafu eti tuna taka vita na malawi wakati hata kirada chenyewe ma gumashi!.....
Mimi acha nilie tu uwiiiii dhaifu wotate naneeeeee!!!!!....
 
Nyie Pro-Chadema JF ebu acheni ushabiki mbona mtanaitakia nchi mabaya.
 
rada.jpg




Hii wiki ya pili

nadhani mnajua kama BAE SYSTEMS wanataka ma bilioni kuja kuifanyia marekebisho

uzuri rada tuliuziwa na wawekezaji ambao tunawapenda na tunawaona sio matapeli (wazungu)

Ingekuwa tumeuziwa na Waarabu naona kungekuwa kunawaka moto sasa

Kazi kwenu na nchi yenu ya kufikirika. Of course waziri husika hawezi kulaumiwa for obvious reasons ( mtu wenu).

Najua uwanja wa ndege umebadilishwa jina lakini silipendi kulitumia hiyo jina kipya linantia kichefu chefu na naomba uamuzi wangu uheshimiwe

Nani kasema anapendwa mtu hapa? Tanzania si ya watanzania? Kwani wanaoiba wanyama hai nao ni wazungu? Kuna watu mnataka dunia iwe kama mnavyofikiria nyinyi... Ukiona waarabu ni watu wema sana nakushauri uhamie uarabuni maana kwangu awe mzungu au mwarabu mambo yao wote ni yale yale.
 
CCM oyeeeeee......
Mkapa oyeeee.........
Kikwete oyeee.......
Chenge oyyeeeee.......
Mna bahati hampitagi mtaani kwetu. Ningewamwagia maji niliyosafishia samaki..... Mngekomaje?
Tunajua mahakama mmezizidi nguvu, lakini kaeni mkijua kuwa, haya mateso mnayompa maskini yanawakosesheni baraka

unapikaga kwani?.
Hili jina limekaa kianaumeanaume.au we bachelor?
 
Asante kunistua. Sikujua nabishana na GT. Huyu jamaa kabadilisha majina kibao humu JF. But we know his true colours. Hebu mwangalie kule kwenye thread ya Muhongo kumkatalia Mwarabu "mwekezaji." Udini mtupu.
mtu kama huyu ni hatari sana, usione mtu akateka ndege na kuibamiza kwene jengo, dalili ni kama hizi..ni kwamba tu kungekua na remote control ya kuua makafiri wote angegombea kubonyeza kitufe..
 
RADA.jpg


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini
(TCAA), Fadhili Manongi



Rada yaharibika


Ni ile iliyomhusisha Chenge
Kifaa kilichokufa kugharimu Mil.40/-

Rada ya kuongozea ndege kwenye Uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere imeharibika na sasa itailazimu Serikali kutumia Sh.milioni 40/- kwa ajili ya kuagiza kifaa cha mfumo wa kusambaza umeme kilichopata hitilafu.


Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini (TCAA), Fadhili Manongi, alithibitisha rada hiyo kutokufanya kazi na kueleza kuwa kifaa kinachoitwa Power Supply Unit kimeharibika.
Kifaa hicho ambacho ni sehemu ya vifaa vinavyosaidia shughuli za kuongoza ndege ,kimezimwa kutokana na hitilafu zilizojitokeza.


Rada hiyo ni ile ambayo ilinunuliwa kwa Dola za kimarekani milioni 40 na Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Silaha ya BAE Systems ya Uingereza na imekuwa haifanyi kazi tangu Agosti 3, mwaka huu baada ya kutokea hitilafu katika kifaa cha kuingizia umeme katika rada hiyo.

Ununuzi wa Rada hiyo ulizua mjadala mkali na kusababisha wabunge mara kwa mara kuhoji gharama kubwa za ununuzi wake.

Sakata hilo lilimfanya aliyekuwa Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza, Clare Short wakati wa Serikali ya Waziri Mkuu Tony Blair, kujiuzulu akipinga Uingereza kuiuzia nchi maskini kama Tanzania rada hiyo kwa bei kubwa.
Kashfa hiyo kwa muda mrefu pia imekuwa ikitajwa kumhusisha aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Andrew Chenge, ambaye pia aliwahi kukutwa na kiasi cha Sh. 1.2 bilioni, kisiwani Jersey, ambazo Taasisi ya Makosa Makubwa ya Jinai (SFO) ya Uingereza, ilikuwa ikichunguza kama zilikuwa na uhusiano na biashara hiyo.


Manongi aliwaambia waandishi wa habari kuwa ni wiki ya tatu sasa kifaa hicho hakifanyi kazi ambapo wahandisi na wataalamu walibaini tatizo hilo wakati wakifanya ukaguzi wao.
Hata hivyo, Manongi alisema hakuna madhara yoyote yaliyotokea kutokana na kifaa hicho kuharibika kwani marubani hawajaeleza matatizo yaliyotokea tangu kuharibika kwa kifaa hicho. Alisema baada ya kutokea kwa tatizo hilo waliamua kuzima mtambo huo na kuwasiliana na Kampuni ya Uingereza ili kuwapa kifaa hicho.


Manongi alisema kifaa hicho kitagharimu Sh milioni 40 na kinaagizwa kwa oda maalumu, kitendo kitakachosababisha kutumia muda kidogo kukipata. "Sio kwamba ukiagiza unakikuta kipo tayari wanapokea oda kwenye kampuni ambayo iliyotuuzia rada hiyo hatujajua kitatumia muda gani kuwasili nchini," alisema.

Alisema badala ya kusubiri kifaa hicho kitoke Uingereza, Jumatatu watakipeleka kifaa kilichoharibika nchini Afrika Kusini ili kifanyiwe matengenezo kwa ajili ya kuendelea na shughuli zake.

Alisema uamuzi wa kukipeleka Afrika Kusini ni njia mbadala ya kusubiri kifaa kipya kwa kuwa Uingereza wanatoa kifaa kipya.
Alisema kampuni hiyo ya BAE tayari imeshaanza mchakato wa kukitafuta kipuri hicho. Alisema kuzimwa kwa mtambo kama huo ni kawaida kwani wahandishi hulazimika kupanda katika antena kwa ajili ya kuweka mafuta mazito.


Manongi alisema pamoja na kuharibika kwa kifaa hicho ambacho ni muhimu bado huduma za usafiri wa anga zinaendelea vizuri na waongoza ndege wanaendelea kutumia taratibu nyingine.
Alisema wamejipanga kuhakikisha hakuna madhara yoyote yatakayotokea kwa kuwa njia mbadala ya mawasiliano katika kuendesha ndege hizo pamoja na redio call zinatumika.


Akizungumzia kuhusu usalama wa anga alisema tangu kuharibika kwa kifaa hicho usalama wa watu unaangaliwa ndio maana mpaka sasa hakuna matatizo yaliyotokea.
"Sio mara ya kwanza kuharibika tumekuwa tukibadilisha vipuri katika mtambo huo kwani ni mara nyingi hivyo ni jambo la kawaida kufanya matengenezo na isitoshe rada hiyo kwa sasa inafikisha miaka 12 tangu iliponunuliwa mwaka 2000," alisema.


Alisema suala la huduma ya anga halitegemei rada peke yake na kwamba kuna njia mbalimbali ambazo zinawezesha huduma hiyo kuendelea.
Aidha alisema hatua nyingine walioifanya ni kutoa taarifa kwa wadau wa usafiri wa anga kote duniani juu ya kuzimwa kwa mtambo huo. Alisema suala la usafiri wa anga nchini linapewa kipaumbele cha pekee kulingana na taratibu za Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga Duniani (ICOA).


Tayari Serikali imeshapokea Pauni milioni 29 za malipo ya fidia kwa Serikali ya Tanzania na imekubaliwa fedha hizo zitumike kununua vitabu na madawati kwa shule za msingi na sekondari nchini.

 
Wakati Tanzania ikiwa tayari kutaka kuingia vitani dhidi ya Malawi, Ile rada kuu inayotegemewa kwa mambo ya anga, mawasiliano, kijeshi na kutua kwa ndege iliyopoko Dar kwenye uwanja wa zamani wa ndege imeharibika kwa karibu mwezi mzima sasa.

Sababu kuu ya kuharibika kwake ni matatizo ya kukatikakatika umeme nchini.

Matengenezo yake yatahitaji vifaa na wataalam kutoka kwenye kampuni ileile ya uingereza uliyotuuzia rada hiyo.

Hii ndio rada iliyonunuliwa kutoka uingereza na kuzaa kashfa ya ufisadi.



SOURCE: BBC

Rada si mbovu, ila wajanja wamefanya mbinu kuiharibu kwa makusudi ili kuvuja pesa za serikali kwa masilahi yao, lazima wawe na pa kusimamia. Chombo kidogo kama hicho kina bei ya kununua rada mpya? Swali la kujiuliza vandugu sangu.
 
Back
Top Bottom