Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,232
- 113,610
R. Kelly ni mwimbaji aliye gwiji. Ana kipaji kikubwa sana. Binafsi nazipenda sana nyimbo zake.
Ila, huyu jamaa huenda akawa ana matatizo ya kingono. Tuhuma za yeye kujihusisha na visichana vidogo hazijaanza leo wala jana.
Kwa kumbukumbu zangu, tuhuma hizo nilianza kuzisikia tokea 1994 pindi Aaliyah alipoibuka.
Baadaye akaja kutuhumiwa kujirekodi kwenye video akifanya ngono na kasichana kengine kadogo 'teenager' mwaka 2003 kama sijakosea.
Hiyo ilipelekea hadi yeye kushitakiwa kwa kutengeneza video za ngono na mtoto aliye chini ya umri wa miaka 18. Hiyo kesi alishinda ingawa ilimgharimu sifa yake kwenye jamii.
Sasa jana kukaibuka na tuhuma zingine tena za yeye kuwanyanyasa wanawake wenye umri mdogo kwenye nyumba zake za Atlanta na Chicago.
Mwenyewe kazikanusha hizo tuhuma. Hilo ni suala la kutegemewa maana sidhani kama anaweza tu kukiri bila mshikemshike kuwa hizo tuhuma ni za kweli.
Kiunganishi cha hiyo habari ya jana hiki hapa: R. Kelly accused of abusing women, running 'cult' in Johns Creek
Jana, familia ya mmoja wa hao wasichana [Joycelyn Savage] wanaodaiwa kuwa ndo wamewekwa ndani na R. Kelly huko Johns Creek, GA, waliitisha mkutano na waandishi wa habari.
Na hivi ndivyo walivyosema.
Baba wa huyo Joycelyn ndo huyo jamaa anayezungumza. Anaitwa Timothy Savage.
Fast forward mpaka leo [tarehe 18 July], binti mtu, Joycelyn kajibu mapigo kwa kurusha hii video huko YouTube.
Joycelyn anadai baba'ake kamuaibisha na pia kaiaibisha familia nzima kwa kufanya mkutano na waandishi wa habari hiyo jana.
Polisi wa Johns Creek nao wamesema hawana la kufanya kama hao wadada wanaishi hapo nyumbani kwa R. Kelly kwa ridhaa yao wenyewe hususan kama wapo na umri zaidi ya miaka 18.
This thing is so bizarre. And R. Kelly has been dogged by these allegations of him liking young girls for decades now.
With him I definitely think there is fire behind or underneath the smoke!
http://www.ajc.com/news/local/kelly...ning-cult-johns-creek/ZejyB7KbyykVWptYuw5ZNP/
Ila, huyu jamaa huenda akawa ana matatizo ya kingono. Tuhuma za yeye kujihusisha na visichana vidogo hazijaanza leo wala jana.
Kwa kumbukumbu zangu, tuhuma hizo nilianza kuzisikia tokea 1994 pindi Aaliyah alipoibuka.
Baadaye akaja kutuhumiwa kujirekodi kwenye video akifanya ngono na kasichana kengine kadogo 'teenager' mwaka 2003 kama sijakosea.
Hiyo ilipelekea hadi yeye kushitakiwa kwa kutengeneza video za ngono na mtoto aliye chini ya umri wa miaka 18. Hiyo kesi alishinda ingawa ilimgharimu sifa yake kwenye jamii.
Sasa jana kukaibuka na tuhuma zingine tena za yeye kuwanyanyasa wanawake wenye umri mdogo kwenye nyumba zake za Atlanta na Chicago.
Mwenyewe kazikanusha hizo tuhuma. Hilo ni suala la kutegemewa maana sidhani kama anaweza tu kukiri bila mshikemshike kuwa hizo tuhuma ni za kweli.
Kiunganishi cha hiyo habari ya jana hiki hapa: R. Kelly accused of abusing women, running 'cult' in Johns Creek
Jana, familia ya mmoja wa hao wasichana [Joycelyn Savage] wanaodaiwa kuwa ndo wamewekwa ndani na R. Kelly huko Johns Creek, GA, waliitisha mkutano na waandishi wa habari.
Na hivi ndivyo walivyosema.
Baba wa huyo Joycelyn ndo huyo jamaa anayezungumza. Anaitwa Timothy Savage.
Fast forward mpaka leo [tarehe 18 July], binti mtu, Joycelyn kajibu mapigo kwa kurusha hii video huko YouTube.
Joycelyn anadai baba'ake kamuaibisha na pia kaiaibisha familia nzima kwa kufanya mkutano na waandishi wa habari hiyo jana.
Polisi wa Johns Creek nao wamesema hawana la kufanya kama hao wadada wanaishi hapo nyumbani kwa R. Kelly kwa ridhaa yao wenyewe hususan kama wapo na umri zaidi ya miaka 18.
This thing is so bizarre. And R. Kelly has been dogged by these allegations of him liking young girls for decades now.
With him I definitely think there is fire behind or underneath the smoke!
http://www.ajc.com/news/local/kelly...ning-cult-johns-creek/ZejyB7KbyykVWptYuw5ZNP/