Putin aridhia kuinga mkono Iran

Putin aridhia kuinga mkono Iran

Labani og

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2020
Posts
22,854
Reaction score
32,657
Rais wa Urusi Vladimir Putin ameahidi kuiunga mkono Iran, kufuatia mashambulizi dhidi ya taifa hilo yanayofanywa na Marekani na Israel.

Itakumbukwa kuwa, Iran imekuwa ikiipa silaha Moscow katika vita vyake vinavyoendelea na Ukraine na mataifa hayo mawili ni washirika wakubwa wa kimkakati.

#DWKiswahili
1750693363945.jpg


Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Si ndiyo huyu aliyeiomba Israel iangalie usalama wa wataalam wake 200 walioko Iran na Israel akasema atazingatia Hilo. Tusubiri maana Kama msaada alitakiwa kuutoa Kama mambo hayajaharibika. Na ndiyo yeye alisema Iran walikataa ulinzi wa anga aliyotaka kuuweka
 
It's called BLOGGING or VILOGING not JOURNALISM.
blogging is someone keeping their personal diary. however it been monitored today.

if you need journalism go to VANGUARD,NATIONAL GUARD,NEW YORK TIMES OR THE GUARDIAN.
 
Na yeye alitafutwa sana ajiunge kijinga, sasa siyo Ukrain wala Iran ataambulia

Aliyeniaminisha niione Iran inauwezo, nitamlaani maisha yangu yote,

Yaani Israel iliyo na vita karibu nchi nne zaidi, wakati huo huo Iran anasulubishwa....?

Siwaamini tena Mashekhe zangu, mtaniwia radhi tu
 
Na yeye alitafutwa sana ajiunge kijinga, sasa siyo Ukrain wala Iran ataambulia

Aliyeniaminisha niione Iran inauwezo, nitamlaani maisha yangu yote,

Yaani Israel iliyo na vita karibu nchi nne zaidi, wakati huo huo Iran anasulubishwa....?

Siwaamini tena Mashekhe zangu, mtaniwia radhi tu
Wewe kweli akili imejaa machichaa ya pombe
Hivi Kuna Israel bila marekani? Akili Gani hii?
 
Si ndiyo huyu aliyeiomba Israel iangalie usalama wa wataalam wake 200 walioko Iran na Israel akasema atazingatia Hilo. Tusubiri maana Kama msaada alitakiwa kuutoa Kama mambo hayajaharibika. Na ndiyo yeye alisema Iran walikataa ulinzi wa anga aliyotaka kuuweka
Ndo wameenda kuomba msaada sasa

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Putin sio jawabu la kumaliza vita. Na akiingia Iran atakuwa so exposed maana Ukraine ni kaa la moto.
Hizi vita zote zina maslahi ya kiuchumi. Europe wanamsaidia Ukraine sababu Russia anawasaidia nchi ambazo Europe zinakula bure.
Waafrika tuzinduke tuamue kuwa serious.
 
Kwanza Iran haikumpa silaha urusi ila urusi alinunua toka Iran

Pili urusi urusi imesema inatarajia kumpatia Iran silaha, Kwa kauli hii urusi inathibitisha kuwa Iran imepungukiwa na silaha ndiyo maana anaomba Msaada

Tatu anachofanya Israel sasa hivi NI kumiliki anga na kuhakikisha hampi nafasi ya Irani kurusha makombora, Irani inaweza ikarusha kombora ila Israel inahakikisha hiyo launcher inaangamizwa

Sasa Kwa Hali ya sasa ama makombora yameangamizwa Kwa Kiasi kikubwa au launcher zimeangamizwa au vyote viwili

Wasiwasi wangu NI Iran inaweza ikapewa silaha lakini kipengele cha kuzifikisha battlefield hizo silaha ndiyo kigumu zaidi hasa ukizingatia Israel ana mamluki wengi ndani ya iran
 
Back
Top Bottom