Pumzika kwa Amani Ka' Abdallah. Tusipende kuchukua sheria mkononi tutaua watu wasio na hatia bure tTu

NDUKI

JF-Expert Member
Jan 19, 2013
3,423
2,414
Habari wandugu.

Natumai mu-wazima kabisa, naandika andiko hili kwa masikitiko makubwa sana kwa kweli.

Jana mnamo majira ya asubuhi nilipata taarifa ya kifo cha ndugu yetu mmoja amezoeleka kwa jina la Ka' Abdallah. Huyu jamaa bwana alikuwa ni dereva wa Prof. Mtulia aliyekuwa Mbunge wa Rufiji, amefanya kazi kwake tangu mwaka 1974 kamuendesha mzee na watoto mpaka watoto wamekuwa wakazaa akawaendesha mpaka na wajukuu.

Sasa bwana jana alikuwa anaenda Masaki kwa boss wake Dr. Ali Mtulia kuchukua gari ili awapeleke watoto shule, akatokea jamaa akampigia kelele za mwizi, basi wakanipiga hapo mpaka akafa.

Na wakati wanampiga walifika raia wakamueleza huyo jamaa aliyemuitia mwizi kuwa huyu jamaa ni dereva wa Dr. Mtulia sio mwizi tunamfahamu lakini bado jamaa wakawa wanazidi kumpiga mpaka akafa.

Katika hali kama hiyo inasikitisha sana kumuua mtu ambaye hana hatia kwa kujichukulia sheria mkononi. Ila mpaka dakika ya mwisho raia walimshikilia yule jamaa ambaye alimuitia kelele za wizi mpaka polisi walipofika wakamchukua yule jamaa na mwili wa marehemu wakaondoka nao.

Jamani tusiwe wepesi kuchukua sheria mkononi pasina kuwa na uhakika wa tukio alilofanya, kuwa na uhakika thabiti kuwa kweli unayemshuku amehusika na tukio na baada ya hapo mpeleke polisi sheria ikachukue mkondo wake kuliko kujichukulia sheria mkononi mtawadhulumu watu nafsi zao bure kabisa.

MUNGU AKULAZE MAHALI PEMA KA' ABDALLAH. POLENI WAFIWA, NDUGU NA JAMAA.


NAWASILISHA.
 
Alienda kuchukua Gari kwa miguu Akitokea wapi? Kweli muendesha Gari la mbunge aende kufata Gari kwa miguu?
Loh, ngumu kumeza

Toka 74, kupata leseni I believe jamaa wa 50 huko, na uzee huo waliokuja kumpiga hapo masaki walitokea wapi?
Hata kuuliza ameiba nn?

Kifo kishapita, ila sababu ya kifo nahisi n utata mtupu,

Maswali mengi hayajibiki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mna roho za shetani
Watu gani ambao wenyewe ni wizi wakubwa halafu mnauwa kwa kusingizia
Yaani serikali imeshindwa hili jambo kulimaliza kabisa na liwe historia?
Eti sheria mkononi na wao wanalitamka bila aibu
Shame on you
Kutwa tunaongelea mauwaji ya nje wakati yetu yanatuahinda tena vifo vya ajabu na aibu mno



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
R.I.P

Umenikumbusha mbali sana kuna watu wanyama ndugu yangu.

2011 pale mtaani kwetu kulikua na jamaa mmoja mpole mstaarabu sana,rastafari tulimzoea kwa jina la Ngosha ,ila alikua mtu wa bangi sana alikua ametoka dodoma na kufika soko la mbagala rang 3 kwa nia ya kuanza maisha.

Alikua mtu wa kubeba mizigo kwenye lile soko na ukifika muda wa kulala alilala popote hata sokoni hakuwa na pakulala.Baada ya kuzoeana na watu akajuana na jamaa mmoja ambaye alikua anaishi mtaa mmoja na sisi hivyo alimchukua kwa ajili ya kuishi wote lakini walishindwana baada ya yule jamaa kuwa anamfanyia vituko rasta hasa alikua anaweza kuingiza demu usiku na kulala naye huku akimwambia rasta akatafute pa kulalal.Mwishowe rasta alishindwa akahama akwa analala mtaani pale baraza lolote na kwakuwa alizoeleka basi watu hawakua na shida nae.

Mtaani pale kulikua na watoto wa 5(4 wanaume na 1 wa kike) waliachiwa nyumba na baba yao aliyefariki wale watu walikua watu wa pombe na wakorofi sana na hata marehemu baba yao aliwahi watabiria kuwa wataishi maisha mabaya akifariki.Kuna siku ile nyumba iliibwa TV na Deki basi wale jamaa wakawa wanasema wameibiwa na yule Ngosha kiasi cha kutaka kumpiga kwa upole na ustaarabu ngosha akawaeleza hana huo uwezo wa kuiba akawasihi sana kwa msaada wa watu wakamuacha hawakumpiga.

Baada ya mwezi siku moja kulikua na mvua sana kama kawaida yake Ngosha hana makazi ya kulala kula kwenye anaunga unga akaona akajistiri kwenye lile baraza la wale jamaa.Usiku kaka yao mkubwa alipotoka alimkuta Ngosha amelala pale huku amejifunika magunia dah wakaamshana wakaanza kumpiga na kumuitia kelele za mwizi,watu tulitoka nje na kila aliyetoka na silaha alirudisha mwenyewe ndani baada ya kumuona Ngosha tuliwasihi sana wamuache wakakubali kishingo upande kwa makubaliano kuwa wampeleke polisi..kosa tulilolifanya kuwaacha wenyewe wampeleke polisi walipofika uwanja wa shule ya msingi walianza tena kumpiga mpaka wakamuua kijana wa watu na ni kazi iliyofanywa na watu wa 4 tu.

Asubuhi tunaamka tunaambiwa kuna mwizi kauawa kwenda tunamuona Ngosha hiyo siku sitaisahau jinsi nilivyoona mwili wa mtu ninayemfahamu alivyouliwa kinyama na watoto waliokosa utu..tulijilaumu mtaa mzima mjumbe akaamua kwenda kuwashtaki lakini baada ya muda ikafutwa ile kesi sijajua nini kilifanyika.

Wahuni wa ule mtaa waliwatenga wale watu ila wakajiapiza watalipa kisasi na kweli bwana kuna siku yule kaka yao alilewa mpaka kuzima wahuni wakamla TiGo saafi kabisa.

Kujichukulia sheria mkononi haifai.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
From no where aseme tu mwizi.???

Wana ugomvi before au niaje.???

Msafwa,
Uporoto, Mbeya..

Yaaaaani kila mtu ana shangaa na sidhani kama wana ugomvi viz mzee wa watu ni mpole, mkimya, mtaratibu wala hana tatizo na mtu na pia hakai eneo moja na huyo jamaa aliyemuitia mwizi.

Na mpaka watu wanafika eneo la tukio wanamwambia huyu mzee tunamfahamu ni dereva wa Dr. Mtulia lakini bado wakawa wanampiga tu.
 
Habari ya kusikitisha sana hii. Yaani huko Dar itabidi kutembea na kitabu kitakatifu mkononi maana hiyo hali ya ikishamiri watu wasio na hatia watapukutia.

Kabisa aisee inasikitisha sana mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom