PSPF na mikopo ya kujikimu

PSPF na mikopo ya kujikimu

Robot la Matope

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2015
Posts
8,584
Reaction score
17,528
Ndugu zangu kipindi naajiriwa pspf walinishawishi kwamba nikichangia Mara 6 wananipa mkopo ambao ni mshahara wangu X3 (basic)
Baada ya kuchangia X6 nimefata wakaanza ahadi kama za wagombea.
Kusema ukweli sijawaelewa.
Hivi kuna possibility ya kuhama mfuko?
 
Wewe hama tu kwani hamna namna. Hao PSSF NI MZIGO kwa watumishi,leo hii kuna watu wamestaafu tangu mwezi wa February 2015 (Miezi 9) lakini hawajalipwa mafao yao, Shame on PSPF!
 
Hawana jipya hao siku flani nilipita hapo baada ya kusikia habari zao za kukopesha nilichoka kuambiwa eti ukachukue benki kwa riba ya benki wao ni km wanakugarantii tu!! Hawa ni majambawazi waliovaa suti.
 
Ndugu zangu kipindi naajiriwa pspf walinishawishi kwamba nikichangia Mara 6 wananipa mkopo ambao ni mshahara wangu X3 (basic)
Baada ya kuchangia X6 nimefata wakaanza ahadi kama za wagombea.
Kusema ukweli sijawaelewa.
Hivi kuna possibility ya kuhama mfuko?

umefanya makosa kuchagua pspf, ni wasanii kwelikweli.mikopo ya elimu wanayotoa riba yao ni 7.5% kwa mwaka chaa ajabu makato yao kwa hela hiyo hiyo ukichukua NMB wenye riba ya 18% makato ya kila mwezi yako sawa ni wasanii balaa
 
Duu Mmenitia Hofu, Mi Mwanachama Ninakaribia Kusitafu Baada Ya Muda Mfupi!
 
Ppf ndio mfuko bora yani huwa ppf mafao yao yakichelewa sana ni 1 week wana DG/MD Smart sana Mr. Erio jamaa ni kichwa sana ambacho serikali haitakiwi kukipoteza
 
Mimi nimehama juzi juzi kutoka PSPF Znipo LAPF kama hujapata kitambulisho mfuate afisa utumishi kwamba unataka kuhama.
 
Viongozi wa PSPF hayo yanayosemwa ni kweli? maana yamenitia hofu na kunipandisha presha sababu juma lijalo nastaafu jee ni kweli waliostaafu wa Aprili hawajalipwa mafao yao?kama ni kweli hamuwatendei haki wanachama wenu kumbukeni hizo ni hela zao walizokuwa wanakatwa kutoka kwenye mishahara yao
 
Kuhusu kuhama mfuko fika kwa afisa utumishi wa halmashauri husika watakupa taratibu.
 
Back
Top Bottom