Propaganda zinasukwa Simba Day isihudhuriwe na watu wengi ili uongozi wa Simba uonekane haufai

Mfa maji haachi kutapatapa. Halafu mbona muda mwingi nikiangalia Azam Tv naona promo ya Siku ya Wananchi pekee kwenye kisimbuzi chao!!

Kulikoni sioni promo ya Mbumbumbu Day!!! Azam Media ndiyo Baba Lao!! Mkimuendekeza Moo atawapeleka shimoni! Shauri zenu. Usikute amewadanganya mrushe matangazo yenu kupitia Dstv isiyo angaliwa na Watanzania walio wengi, kama ilivyo kwa Azam.

Ndicho mlichobakiza “promo” tu.Mambo ya msingi kama Pre season kwenu siyo ya muhimu.Uzuri tukiwa tunacheza ngao ya jamii nyie CL mtakuwa mlishatolewa
 
Hizo ndio mbinu zenu UTOPOLO kutuvuruga ila ubingwa msahau nyie wacheza Ndombolo.
Kwa misimu minne mfululizo wao wanapiga blaablaaa porojo fitna,majungu na propaganda dhidi ya ,lakini huwa anaibuka kidedea mwishoni mwa msimu , UtOPoLo mnafeli Sana,wamewekeza nguvu kubwa kwenye propaganda kuliko uwanjani.
 
Natamani Simba ifikie hatua ya kutomtegemea yeyote.
Yaani ni sawa na kutamani kuona siku moja ccm ikisimama yenyewe pasipo kuwategemea polisi na tume ya uchaguzi! Itaangukia pua bila shaka!

Simba ni Moo na Barbra! Ukitofaitiana kwa namma yoyote ile na hao watu wawili, basi ujiandae kufukuzwa kwenye hiyo klabu kama paka mwizi.
 
Watajua wenyewee sisi mashabiki wa simba tunataka burudan tu na makombe
Na ndiyo maana Ismail Aden Rage, Mwenyekiti wenu Mstaafu aliwaita mbumbumbu! Vipi mkikosa hiyo burudani na hayo makombe! Bila shaka mtapiga tena kelele za kumkataa huyo Moo wenu!!
 
Mfa maji haachi kutapatapa. Halafu mbona muda mwingi nikiangalia Azam Tv naona promo ya Siku ya Wananchi pekee kwenye kisimbuzi chao!!

Kulikoni sioni promo ya Mbumbumbu Day!!! Azam Media ndiyo Baba Lao!! Mkimuendekeza Moo atawapeleka shimoni! Shauri zenu. Usikute amewadanganya mrushe matangazo yenu kupitia Dstv isiyo angaliwa na Watanzania walio wengi, kama ilivyo kwa Azam.
Wewe Utopolo huijui biashara ya mpira.Nyamaza tu.
 
Wana Simba wenzangu kumbukeni mafanikio ya Simba kwa miaka 5 yametokana na kazi nzuri aliyoifanya aliyekuwa RC wa DSM Paul Makonda, bila yeye ubingwa tungekuwa tunausikia tu kwa jirani.

Dhambi inamsumbua kwa alichokifanya kwa hakina Manji kwa maslahi yake na ya Simba.
 
Acha uongo, Manara japo Mimi binafsi sijawahi penda namna anavyo zungumza ila alikua anaushawishi binafsi ku ujaza uwanja. Ata usipo ujaza Ila watu uwa wakutosha.

Mashabiki wa Simba ni watu wazima japo u mbumbumbu ni sehemu ya DNA yao wanajua mchango wa Manara katika hamasa, Ule ni uwezo wake Haji.

Kwasasa amesha ondoka mliobaki onyesheni uwezo wenu katika kuhamasisha msitafute huruma na kumfitinisha Haji na Wanasimba.

Kama mnafikiri Haji hakua na mchango wowote katika kuhamasisha mashabiki nyinyi mliobaki tumieni ushawishi au acheni kwakua mashabiki watajaa bila hamasa.
Kabla ya uwepo wa manara Simba haikuwah kujaza uwanja?

Unataka kuniambia watu walikuwa wanamfuata manara uwanjani na sio soccer Safi la Simba?

Unataka kuniambia Leo hii manara akiwa msemaji wa club ya kmc anaweza kuongea na kushawishi cku ya kmc day akaujaza uwanja?

Je huon kuwa manara kapata umarufu kupitia Simba ?

Je unaamini manara ndie huwapatia ubingwa Simba ? Kama ni hivyo Basi Safari hii yupo upande wa yanga nadhan majibu yatapatikana tu soon
 
Ligi ikianza Haji ataonekana kama Mzee Mpili tu huko Yanga
IMG-20210826-WA0015.jpg
 
Back
Top Bottom