Project ya UDART imeshakufa

Project ya UDART imeshakufa

Kipaumbele chetu ni watanzania masikini, ndio maana tunawanunulia -400, ndotolaini, tunajenga sgr ya kwenda kwetu. Nyinyi matajiri mnaopanda mwendo ukakasi sio kipaumbele chetu, hadi muwe mashetani.
 
aletwe mbia mwingine period hizi siasa zenu hatutaki we need service and it is not frèe we are paying
Hawataki ushindani UDART wameshafungua kesi dhidi ya serikali kumleta muwekezaji mwingine
 
Nadhani lianzishwe somo entrepreneur skills kwenye mtaala kuanzia la kwanza hadi chuo. Huenda ikasaidia.
 
hahahaa hata waliongia mkataba na hii kampuni si wazalendo , serikali inalipwa sh 10M kila siku , wakati huo huo sirikali imeivest shs 300 Bil, kwa hiyo payback period ni miaka mia , sasa siulize je hiyo miundo mbinu itadumu kwa miaka mia ? Wakati hiyo kampuni kila siku wanaingiza zaidi ya shs 100.
mkuu miradi mingi serikali inafanya kama huduma kwa wananchi hiyo ya miaka mia ya payaback period isikupe shida hata kidogo.
 
Watanzania mna manung'uniko na lawama zisizoisha as if kwenye maisha yenu binafsi mpo timilifu.

Wengi mmeshindwa manejimenti hata ya familia zenu lakini mnavyojitutumua kutoa lawama kwa wengine!!! Ovyo kabisa!!!
 
Yaani sijui hawa waendeshaji wa huu mradi hua wanafikiria kwa kutumia nini,
Anyway, RIP Dkt Didas Masaburi
 
Kwa mtaji huohuo Na vitendea kazi hivyo hivyo akiletwa CEO Mkenya UDART itakuwa imara. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, sisi tuna laana ya kutokuwa serious.
Kila jambo tunaloanzisha Lina mwisho mbaya kwa sababu ya laana ya mwenge.
Isaya : Mlango 50

11 Tazama, ninyi nyote mwashao moto, mjifungiao hiyo mienge; endeni ninyi katika mwali wa moto wenu, na katikati ya mienge mliyoiwasha. Mtayapata haya kwa mkono wangu; mtalala kwa huzuni.
Kulala kwa huzuni maana yake hamtafanikiwa.
leo umenifumbua macho..kumbe Nyerere alituletea laana
 
Naiangalia project ya UDART kwa jicho la tatu naona inakufa. Pamoja na support kubwa ya Serikali bado hawa jamaa (management ) wameshindwa kujiongeza kabisaa.

Imagine if were you unaondolewa washindani wako katika biashara unabaki peke yako harafu unashindwa kufanya huduma unategemea nini?

Wateja ( pamoja na mimi) wanalalamika kukaa muda mrefu vituoni lakini utawala hauna ufumbuzi.

Wametoa namba za customers care hazipokelewi kabisa(nadhani kwenye hili wanamlizisha mheshimiwa kama vile wafanyabiashara wanavyobandika siku ya TRA kuwa yeye analipa kodi while not)

Hawa jamaa hawajui;
1.Muda gani ni peak/rush hours magari yawepo barabarani
2.Madereva kuanza kazi muda tofauti tofauti kutasaidia kumaliza kazi muda tofauti
3.Hawapo systematic katika kuyaondoa magari kwenye main port zao yanaweza yakaongozana magari hadi sita yanayoelekea upande mmoja
4.Overtime, motisha nahisi kwao wanaogopa kufanya.

Nimeona nchi za wengine walioanza kufanya hizi projects kwenye miji yao mikubwa;
1.Magari yanafanya kazi masaa 24/7 ila yanapungua barabarani jinsi muda unavyozidi kuyoyoma na siku za weekends
2.Sio lazima magari yote yaanzie mwanzo kupakia abiria kunakuwa na mawasiliano kati ya head office/port na vituoni kuangalia wingi wa abiria na kutuma gari
3.Dereva anaye fanya vizuri mfano kuwahi, attendance, ukarimu/costomer care anakuwa rewarded
Taifa la wajinga mnatakiwa kuburuzwa tuu hakuna namna
 
Wakuu Mnashindwa Kutambua kwamba Miradi Mingi ya Tanzania ni WHITE_ELEPHANT PROJECTS,Lengo ni Kupiga DEAL tu na sio kumsaidia mtanzania,ndio maana umeona watu wameenda kujenga kwenye BWAWA la maji Jangwani they dont care ili mradi washapiga 50% nyie mtajijua....Miradi Mingi ya Maji hela imetoka yote 100% lakini hakuna hata tone la maji yanayotoka,Hii ndio Tanzania...Hiyo UDART/UDA /KISENA/RIZMOKO yote wizi mtupu.

Bongo hakuna customer's care bali ni Customer's KERO.
 
Back
Top Bottom