Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,974
- 6,721
Profesa wa Uchumi, Samuel Wangwe, amesema nchi za Afrika zinapaswa kuweka kipaumbele katika kuongeza thamani ya rasilimali zake ili kunufaika ipasavyo na utajiri uliopo barani humo. Amesema miongoni mwa njia muhimu ni kuwekeza kwa vijana kwa kuwapeleka kujifunza katika mataifa yaliyopiga hatua kiteknolojia, ili warudi na kutumia ujuzi huo kuendeleza nchi zao.
Ameeleza hayo leo Januari 21, 2026, kupitia kipindi cha Mizani cha TBC 1, wakati akichangia mada inayohusu nafasi ya Afrika katika muktadha wa siasa za kikanda na maendeleo ya kiuchumi.
Ameeleza hayo leo Januari 21, 2026, kupitia kipindi cha Mizani cha TBC 1, wakati akichangia mada inayohusu nafasi ya Afrika katika muktadha wa siasa za kikanda na maendeleo ya kiuchumi.