Profesa Maghembe, Sasa imetosha tuwape wanyama silaha wajilinde wenyewe

JAMII-ASM

JF-Expert Member
Jul 30, 2015
1,305
524
you-get1.jpg

Tumeshuhudia siku chache zilizopita mauaji ya kinyama ya rubani Capt. Roger yaliyofanywa na majangili .Ujangili nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla badala ya kupungua ndio kwanza unashika kasi,na kufikia hatua ya kutungua hata vyombo vya anga.
Raven-II-for-sale.jpg

Kitu kibaya zaidi majangili wameungana na magaidi.Ushauri wangu kwa Mh. Maghembe..kama tumeshindwa Kupambana na majangili basi ni wakati muafaka Tanzania ianze kuwapa mafunzo wanyama pori ,wajilinde wenyewe. Hii haitakuwa mara ya kwanza kwa Tanzania kufundisha wanyama .Wengi tunaufahamu mradi wa panya wa kutegua mabomu.Mradi huu umesaidia sana katika nchi zilizo tumbukia katika vita na kubaki na maelfu ya mabomu ardhini.
Kama inavyoonekana katika picha ya nyani hapo juu aliepewa mafunzo ya kuwalinda nyani wenzie pamoja na faru dhidi ya maadui .. hususan binadamu..Tunaweza tukaanza na battalion moja ya nyani wenye IQ ya kushika mafunzo...kama nyani huyu wa South Africa aliepewa kazi ya kulinda faru na kampuni iliyompa mafunzo na kumuajiri... na sasa kampuni hii inalipwa fedha nyingi.
 
Kw nn wasitumie JW?ninauhakika siku JW likipiga kambi kwenye hizo hifadhi hutasikia hata mbu kaguswa!
 
anafundishwa kumtabua jangili sio kwamba akiona mtu yeyote anakatiza bas ni shaba tu!Ss hata anyemfundisha tutamuona naye ni nyani tu
 
Kw nn wasitumie JW?ninauhakika siku JW likipiga kambi kwenye hizo hifadhi hutasikia hata mbu kaguswa!
Na ndio maana Rais Magufuli kamteua katibu mkuu wa maliasali kutoka JWTZ Meja Jenerali Gaudence Milanzi.Hili jukumu analiweza.
Ila ni wakati muafaka wa kubuni mbinu mpya.Kama hii..ya wanyama kutumia silaha na kujilinda wenyewe sehemu zisizofikika kwenye mbuga.
 
Eeeeh.......mkuu......hii sasa si itakuwa vita......wacha tuwalinde tu maana hakuna namna nyingine........nyani hakawii kukutungua.......tena hawa wa kwetu ukimuangalia kwa mbali ana jazba.........mi nadhani......watu wafanye kazi zao na waache mzaha........kuna mzaha mkubwa sana unaendelea..........
 
Sasa naanza kuhisi operation tokomeza iligus watu wakaamua kuizika kwa hila
 
Njia ni moja tu hii wizara ikopewe kwenye wizara ya Ulinzi na JKT kwa mda alafu hawa jamaa waweke Deti huko Mbugani tuone kama kutakua na ujangili.
 
anafundishwa kumtabua jangili sio kwamba akiona mtu yeyote anakatiza bas ni shaba tu!Ss hata anyemfundisha tutamuona naye ni nyani tu
Nyani huyu kafundishwa ishara tatu tu.. LOAD, SHOOT na CEASE FIRE .Ila kama ilivyo kwa viumbe wengine nyani nae huwa ana ndoto mbaya ''nightmares''..anaweza akaamka vibaya. Siku hiyo inabidi asipewe silaha..maana hakuna atakaebaki.
 
Njia ni moja tu hii wizara ikopewe kwenye wizara ya Ulinzi na JKT kwa mda alafu hawa jamaa waweke Deti huko Mbugani tuone kama kutakua na ujangili.
Hicho ni kilio cha wengi..Maliasili iwe idara chini ya Wizara ya Ulinzi kama ilivyo JKT.
 
Eeeeh.......mkuu......hii sasa si itakuwa vita......wacha tuwalinde tu maana hakuna namna nyingine........nyani hakawii kukutungua.......tena hawa wa kwetu ukimuangalia kwa mbali ana jazba.........mi nadhani......watu wafanye kazi zao na waache mzaha........kuna mzaha mkubwa sana unaendelea..........
Katika viumbe wenye akili sana mmojawapo ni nyani.Ukweli ni kwamba uhusiano wetu na nyani si mzuri. Siku wakijijengea uwezo kama nyani huyu nafikiri ndio utakuwa mwisho wetu.
 
Kweli kabisa. ....

But tuanze kwanza na ulinzi shirikishi ... Kuwe na mahusiano mazuri kati ya wananchi wanaoishi maeneo karibu na pori na hao walinzi wa pori. .
 
TOKOMEZA ilihujumiwa na wanufaika wa ujangili wa meno ya tembo na maadui wa kisiasa wa Dr. Kagasheki.
Mkuu unaongea point sana tatizo kubwa la nchi yetu mambo kupekeka kisiasa ile operation ilikua ina maana sana ila watu wakataka umaarufu wa kisiasa na Jeshi haliwezi kufanya kazi na wanasiasa Dawa ni moja tu tuwaruhusu Wanajeshi watulindie Mbuga zetu baas!
 
kama soko la pembe za ndovu lataendelea kuwepo basi ujangiri hautaisha leo wala kesho.
 
Back
Top Bottom