Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), profesa Ibrahim Lipumba, amemshambulia Rais Jakaya Kikwete kuwa hajali matatizo ya wananchi pindi yanapojitokeza mazito ya Kitaifa.
Akihutubia mkutano wa hadhara uwanja wa Mwanga Centre mkoani Kigoma juzi, Profesa Lipumba alisema rais anapaswa kuwa makini na kuonyesha misingi bora ya uongozi.
Rais wetu amekuwa akichezewa ovyo na watu na kutukanwa bila sababu za msingi, hali hii inasababishwa na rais kutokuwa makini. kwa bahati mbaya sana, ana udhaifu wa kutokuwa makini, jambo linalofanya baadhi ya watu kupoteza imani naye na kumuona kama mfano mbaya wa kiongozi wa nchi.
Rais amekuwa hajali matatizo ya wananchi na kutoa mfano wa milipuko ya makombora ya Gongo la Mboto.
Baada ya kutokea milipuko Rais aliondoka zake kwenda Ulaya, kama rais anafanya safari kipindi kigumu kama hicho, ni wazi wananchi watapoteza imani naye, Profesa alisema Rais Kikwete alikimbia wageni kutoka nchi mbalimbali kutazama fursa za uwekezaji, lakini Rais aliondoka kwenda nje.
Mwananchi Machi 15 2011
Akihutubia mkutano wa hadhara uwanja wa Mwanga Centre mkoani Kigoma juzi, Profesa Lipumba alisema rais anapaswa kuwa makini na kuonyesha misingi bora ya uongozi.
Rais wetu amekuwa akichezewa ovyo na watu na kutukanwa bila sababu za msingi, hali hii inasababishwa na rais kutokuwa makini. kwa bahati mbaya sana, ana udhaifu wa kutokuwa makini, jambo linalofanya baadhi ya watu kupoteza imani naye na kumuona kama mfano mbaya wa kiongozi wa nchi.
Rais amekuwa hajali matatizo ya wananchi na kutoa mfano wa milipuko ya makombora ya Gongo la Mboto.
Baada ya kutokea milipuko Rais aliondoka zake kwenda Ulaya, kama rais anafanya safari kipindi kigumu kama hicho, ni wazi wananchi watapoteza imani naye, Profesa alisema Rais Kikwete alikimbia wageni kutoka nchi mbalimbali kutazama fursa za uwekezaji, lakini Rais aliondoka kwenda nje.
Mwananchi Machi 15 2011