GE2025 Profesa Kitila: Wakati wa uchaguzi kama huu, maneno maneno lazima yawepo, lakini mama Samia yupo imara

GE2025 Profesa Kitila: Wakati wa uchaguzi kama huu, maneno maneno lazima yawepo, lakini mama Samia yupo imara

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mafyangula

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2025
Posts
505
Reaction score
887
"Wakati wa uchaguzi kama huu, maneno maneno lazima yawepo, lakini mama yupo imara, amestahimili, kwa dua zenu Mungu pia hatamuacha, atasimama naye na tutavuka salama tarehe 29 Oktoba na nchi yetu itasonga mbele" -Prof. Kitila

‎Prof. Kitila ameeleza hayo Oktoba 09.2025, kwenye kongamano la dua ya kuliombea Taifa kuelekea uchaguzi mkuu, lililo andaliwa na Jumuiya ya Wanawake wa kiislamu Tanzania (JUWAKITA) na kufanyika katika ukumbi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kata ya Manzese

 
"Wakati wa uchaguzi kama huu, maneno maneno lazima yawepo, lakini mama yupo imara, amestahimili, kwa dua zenu Mungu pia hatamuacha, atasimama naye na tutavuka salama tarehe 29 Oktoba na nchi yetu itasonga mbele" -Prof. Kitila
'Sycophants' wanaoweka pembeni kabisa akili zao, ili mradi wajaze tumbo!

Hata hao anao zunguumza nao wanamwona yeye kama hazimtoshi kichwani.

Kuna uchaguzi gani uliowahi kufanyika katika mazingira yaliyopo sasa; awaeleze hao watu.

Kuna uchaguz ambao watu wamekuwa wakitekwa, kupotezwa na kuuawa kama huu?
Kuna uchaguzi wowote uliofanyika wakati mgombea wa chama alwaogopa watu wa chama chake na kujiteua yeye mwenyewe?

Kuna uchaguzi ambao kampeni zake zote zimedorola kama huu; na watu kusombwa kwa nguvu kwenda kwenye mikutano ya kampeni?

Naona kaalikwa na kundi maalum kutoa nasaha kwao; kuna wakati wowote katika historia ya nchi hii ambapo wananchi waligawanywa katika makundi kama ilivyo sasa?

Haya yote waTanzania wanayaona; ila yeye anayachukulia kuwa mambo ya kawaida wakati wa uchaguzi?

Hawa malaya wa kisiasa wanaodhalilisha elimu waliyopata ili kuwasaidia waTanzania wao wanaigeuza kuwa mtaji wa kujiuza inabidi watambuliwe na umma kuwa maadui wa taifa hili.
 
Zamani nilimuonaga huyu jamaa ana akili, baada yakukaa kwenye meza na watawala amekua mjinga mjinga sana.
Huyu siyo "mjinga", huyu ni mpumbavu hasa; kwa maana si kwamba hajui kuhusu ushiriki wake katika uovu; anajuwa vizuri kabisa.
Kuteka watu na kuuwa ni maneno maneno sawa Professor . Yaani ndiyo wasomi wetu hawa eti!
Itafaa pawepo na utaratibu wa kuwatambua michango yao hawa wasomi katika kuwakandamiza waTanzania. Ni mhimu pawepo na kumbukumbu inayo elezea michango yao hiyo, ili historia ibaki ikiwatambua hivyo.
 
G2WZpGgXEAAHoA4.jpeg
 
"Wakati wa uchaguzi kama huu, maneno maneno lazima yawepo, lakini mama yupo imara, amestahimili, kwa dua zenu Mungu pia hatamuacha, atasimama naye na tutavuka salama tarehe 29 Oktoba na nchi yetu itasonga mbele" -Prof. Kitila

‎Prof. Kitila ameeleza hayo Oktoba 09.2025, kwenye kongamano la dua ya kuliombea Taifa kuelekea uchaguzi mkuu, lililo andaliwa na Jumuiya ya Wanawake wa kiislamu Tanzania (JUWAKITA) na kufanyika katika ukumbi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kata ya Manzese

Kitila inatakiwa kunyanganywa vyeti vyote alivyopata UDSM , Udsm university haikuwai zalisha watu wa hovyo , anyanganywe haraka sana ,hii ni haibu kwa chuo ambacho kimetoa viongozi mbalimbali wa kitaifa na kimataifa .

Jk kama mkuu wa chuo Udsm ebu anza na hili nyanganya vyeti vyote vya Kitila alivyo pata Udsm , siwezi kuwa member wa UDSM UN , na kuwa group moja na wapumbavu kawa hawa , hii haikubaliki ,huu ni upumbavu na kudhalilisha chuo chetu tz
 
Kuna haja watoto wa hawa jamaa nao wachezee ndoige ili tuongee lugha moja. Hayawezi kuwa maneno maneno kama mtoto wa Mkumbo atapotezwa na wasiojulikana, tutaongea same language.
 
Kuna mambo yanasikitisha sana sio tu ni aibu,hawa ndugu zetu wamepigwa upofu mkubwa sana hata kama ni siasa basi hii sio ni ushaitwan,shauri zao watapata majibu yao.
 
Back
Top Bottom