Prof. Tibaijuka adhalilishwa mkutano wa kampeni za maoni CCM, Mkutano wavunjika

Hii nchi ilivyojaaliwa raia waajabu usishangae ukisikia amerudi bungeni kwa ushindi wa kishindo
 
Pole sana Anna. Sisi wengine tunajua wewe ni "iron lady". Siasa ziko rough na endelea kujifunza mbinu za kupambana.

Usimdanganye kwani huo muda wa kuendelea kujifunza hatakua nao. Unauelewa umri wake? Yeye na mzazi wake aliemzaa wanapishana kwa miezi sita tu (just kidding) na hata hivyo jina lake lisingerudi lazima likatwe.
 
Aliyekuwa Mbunge wa Muleba Kusini, Prof Anna Tibaijuka anayewania jimbo hilo kwa mara ya pili, jana alishushwa jukwaani kwa kuzomewa na wananchi wake katika kata ya Nshamba wilayani Muleba.



Prof Tibaijuka alishushwa jana wakati wa kampeni za kura za maoni kupitia CCM.


Hali ya kuzomewa ilidumu kwa dakika kadhaa jambo lililofanya Wagombea hao kulazimika kuondoka.Kwa mara ya kwanza alizomewa juni 8, wakati wa ziara ya katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana katika kata hiyo hiyo.


Akiwa na Kinana wananchi walimtuhumu ufisadi wa fedha za Escrow na kushindwa kutekeleza ahadi ya kuwajengea barabara ya lami.


Source: Mwananchi

siungi mkono tabia ya kuzomea wasomi wetu. najuwa Anna ameponzwa na mfumo wa kiwizi-wizi wa ccm, lakini utu wake na hadhi yake kama professor havipashwi kudharauliwa hata kidogo kwa kisingizio chochote. tuwache siasa za majitaka.
 
Uchaguz na maamuzi upo ndni ya wanashamba wenyewe. Tatizo lingine ni ukweli usio pinginka kuwa baadhi ya wapinzani kutika Nshamba wako so cheap kurubuniwa ni hela ya mboga. 2010 kuna kamaa wa NCCR inasemekana alipewa hela ya mboga M2 akabuy boda na kuamua kuuza jimbo.
Mwaka huu UKAWA wamesema hamna jimbo litakalopita bila kupingwa.
 
siungi mkono tabia ya kuzomea wasomi wetu. najuwa Anna ameponzwa na mfumo wa kiwizi-wizi wa ccm, lakini utu wake na hadhi yake kama professor havipashwi kudharauliwa hata kidogo kwa kisingizio chochote. tuwache siasa za majitaka.

Usomi sio kuitwa professor ndugu.hata maji marefu ni professor,mtu asiye kuwa na heshima na kuwaheshimu watu uwezi kumuita msomi.!!!
 
liyekuwa Mbunge wa Muleba Kusini, Prof Anna
Tibaijuka anayewania jimbo hilo kwa mara ya pili, jana
alishushwa jukwaani kwa kuzomewa na wananchi wake
katika kata ya Nshamba wilayani Muleba. Prof Tibaijuka
alishushwa jana wakati wa kampeni za kura za maoni
kupitia CCM. Hali ya kuzomewa ilidumu kwa dakika
kadhaa jambo lililofanya Wagombea hao kulazimika
kuondoka.
Kwa mara ya kwanza alizomewa juni 8, wakati wa ziara
ya katibu mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana katika
kata hiyo hiyo. Akiwa na Kinana wananchi walimtuhumu
ufisadi wa fedha za Escrow na kushindwa kutekeleza
ahadi ya kuwajengea barabara ya lami.
Source: Mwananchi
Nini maoni yako kuhusu hilo?

Maoni yangu ni kuwa huyo mama a some alama za nyakati kwani wapiga kura wake hawamtaki,awachie jimbo kwa cdm
 
siungi mkono tabia ya kuzomea wasomi wetu. najuwa Anna ameponzwa na mfumo wa kiwizi-wizi wa ccm, lakini utu wake na hadhi yake kama professor havipashwi kudharauliwa hata kidogo kwa kisingizio chochote. tuwache siasa za majitaka.

Ufinyu wako huo wa kuwaza wasomi walio potoka umepitwa na wakati.Wasomo wapuuzi na wezi kama hawa hatuwahitaji katika jamii wanapaswa kupingwa kwa mbinu zozote zile kwani ni zaidi ya haramu.Naunga mkono kuzomewa kwao.
 
Mambo yalipokuwa magumu ikabidi
Mama wa Mboga
aombe askari wa ulinzi kumtoa kwenye mkutano.



Leo Katika hali isiyo ya kawaida,Mkutano wa Wananchi na Watia Nia wa Ubunge Jimbo la Muleba Kusini kwa Tiketi ya CCM umeshindwa kufanyika na kuahairishwa kutokana na Vurugu zilizojitokeza pale aliposimama Mama Anna Tibaijuka Mbunge wa Jimbo La Muleba Kusini maarufu kama "Mama wa Mboga"

Ilivyokuwa;
Watia nia hao wa CCM kwa pamoja wakiwa wameambatana na Prof Anna Tibaijuka,walitoka Wilayani na kwenda moja kwa moja katika Makao Makuu ya Kata ya Nshamba.Pale Nshamba Mjini Ahamuhumula,walienda kujinadi kwa Wananchi wa Nshamba.

Kama kawaida kwenye mkusanyiko wa Wananchi kunakuwa na Watu wa vyama tofauti.

Ndipo wakati watia nia wakiongea,ikafika zamu ya Mama wa Mboga,Mama Anna Tibaijuka kuongea na Wananchi wa Nshamba.

Kabla hajaanza kumwaga sera,ndipo pembeni pembeni ikaanza kusikika minongono ya watu wakihoji kuwa Mama Aseme aliwaona wapi wakinywa Viroba alivyosema siku akiwa na Kinana?

"Kwanza utwambie ulituona wapi tukinywa viroba?,huyu Mama hana heshima amelewa madaraka"…"Na Ccm mkirogwa kumrudisha huyu,Jimbo tunawapa Upinzani hilo mlijue"… Walisikika baadhi ya watu wakiongea kwa sauti mkutanoni hapo hali iliyomfanya Prof Anna aanze kuweweseka na kughafirika na kuanza tena kujibu mapigo kwa maneno ya kejeli!

Akatamka kwamba "Watu wa Nshamba hamuwezi kuniyeyusha kama Mshumaa… mimi siyo mshumaa,kaeni na ujinga wenu".

Basi hali hiyo ikaleta mtafaruku! Zomea zomea maarufu kwa Kihaya "Okugegeeza" ikaanza kupita kiasi… ndipo Mama alipotolewa kwa Ulinzi mkali wa Polisi na Green Guard ili kukwepa "amabare ga abanyansi" na Mama akatokomea,na ndipo Mkutano ulipohairishwa na Mc wa Mkutano huo… huku watia nia wengine wakisema wamenyimwa haki yao ya kujinadi! Lakini hatimaye Mkutano umehairishwa mpaka baadae itakapotangazwa tena.

Kilichofurahisha zaidi ni wakati pale Watu wa Nshamba wakipaza sauti kwa mama Tibaijuka… walisikika wakiongea Kiswahili safi na kilichonyooka kisicho na Lafudhi ya Kihaya… hali hiyo inaonesha sasa Nshamba imekuwa,na imeanza kupiga hatua! Kiswahili safi kabisa!


Credit: Mr Edmund Revelian


Wange kateela mabare
 
Last edited by a moderator:
prof%2Btba.jpg

Mbunge wa jimbo la Muleba kusini Prof anna Tibaijuka jana july 21,2015 alidhalilishwa na wana CCM katika kata ya Nshamba baada ya yeye na wagombea wenzake kufika eneo hilo kujinadi kabla ya kupigiwa kura hapo august 1,2015.Mwendeshaji wa mkutano alikuwa ni katibu wa CCM wa wilaya kwa kumkaribisha kila mgombea kueleza sera zake.


Chanzo: Bukobanewz



yaan uprofesa ndo namna hii?kwa nn asiachane na siasa afanye kazi yake aliyosomea?kwa staili hii kumbe siasa ni utumwa!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom