Tume ya Katiba
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,896
- 1,862
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa, Sospiter Muhongo, amewataka wananchi kuvuta subira wakati akishughulikia orodha ya watumishi wanaolihujumu Shirika la Umeme (Tanesco) kwani yeye si mtu wa kukurupuka.
Aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na NIPASHE mjini hapa juzi.
Vuta subira unajua mimi nimelelewa katika sayansi, si mtu wa kukurupuka tu, ni lazima tufanye uchunguzi kwanza suala si kuyataja tu, alisema.
Alisema hataki kumuonea wala kumpendelea mtu, hivyo watafanya uchunguzi wa kina, kuyaanisha matatizo na kisha kuja na njia za utatuzi kabla ya kutoa taarifa kwa umma.
Profesa Muhongo, alisema hayuko tayari kusema mambo nusu nusu katika vyombo vya habari na kutaka wananchi kuvuta subira.
Hivi karibuni, Profesa Muhongo, alikwenda kutembelea Tanesco na kuwataka watumishi kuwataja watu wanaolihujumu shirika hilo kwa kutumia kura za siri.
sosi: Ippmedia.com
Aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na NIPASHE mjini hapa juzi.
Vuta subira unajua mimi nimelelewa katika sayansi, si mtu wa kukurupuka tu, ni lazima tufanye uchunguzi kwanza suala si kuyataja tu, alisema.
Alisema hataki kumuonea wala kumpendelea mtu, hivyo watafanya uchunguzi wa kina, kuyaanisha matatizo na kisha kuja na njia za utatuzi kabla ya kutoa taarifa kwa umma.
Profesa Muhongo, alisema hayuko tayari kusema mambo nusu nusu katika vyombo vya habari na kutaka wananchi kuvuta subira.
Hivi karibuni, Profesa Muhongo, alikwenda kutembelea Tanesco na kuwataka watumishi kuwataja watu wanaolihujumu shirika hilo kwa kutumia kura za siri.
sosi: Ippmedia.com