Prof Muhongo ni MUONGO au ANATANIA!!

Prof Muhongo ni MUONGO au ANATANIA!!

nimepitwa na kioja cha wiki..... CENTEMETRE.... CENTIMETER.... Kipimo kipya cha ukuaji wa uchumi.....!!!!

mwambie mkuu aache kumlisha maneno profesa muongo!!!yule jamaa kasoma hadi kakuta kibao kimeandikwa 'no skuli' afu mkuu anamtania na kumdhalilisha kuwa jamaa hajui kusema sentimita aaaah no pasenti?hiyo sikubaliiiiii
 
Tatizo liko wapi, unajua vigezo vya ukuaji uchumi ni Tofauti na Ustawi wa Jamii? Yule Profesa keshasema yeye haongelei porojo kama unazoleta hapa? Economic Growth na Welfare of Society ni Vitu viwili tofauti sio kwa
ni Dunia nzima ila Kwa kuwa wewe ni bwe.gwe ukatupa kalamu na kurukia ki laptop/PC chako kuwahi kuleta uj.inga wako. Thibitisha kuwa uchumi haukui kwa kiwango hicho, Hata Tafiti za WB na IFM zinasema the same thing, Ukuaji wa Uchumi hauzungumzii Mlo mmoja au kuishi chini ya Dola moja kwa siku hayo hayana uhusiano na Economic Growth, Shule mlipata vyeti badala ya elimu basi walau muwe mnazurura Mtaa GOOGLE mnaweza mkaziba viraka ya u.jinga vilivopo kichwani. Hapo kwenye Red umemlisha maneno Profesa Vipimo vya ukuaji wa uchumi havitumii vipimo vya CENTEMETR.

IFM hii hii ya hapo Posta??
 
Nilimsikiliza pia lakini nikagundua kuwa ana kujiamini kupita kiasi. Kuna wakati alisema gharama ya mafuta TANESCO ni trilioni mia tisa na kitu baada ya kubadili dola milioni kadhaa za Marekani. Wabunge wengi waliguna lakini bado hakutaka aonekane amekosea na akajifanya kupotezea kiaina na kusema kuanzia wakati ule angeanza kutaja hayo mapesa kwa dola manake kubadilisha kwenda kwenye shilingi inasumbua. Kazi kweli kweli!!!
 
ungetuletea hotuba nzima tungekuona unaakili,badala ya kutuwekea vitu vya maana,una kimbilia vitu vya kijinga,acha unafiki
 
Kiukweli alikosea kwa bahati mbaya na alirekebisha hapo hapo, na si hilo tuu alikosea hata kutaja mkoa wa Simanjiro hadi alioulizwa na Spika pia alikosea hata kubadilisha dola kwa shilingi pale aliosema Dolla milioni mia tano ni sawa na shilingi trioni mia saba na alipokosolewa alisema haya mambo ya shilingi yanamchanganya.
 
Tatizo liko wapi, unajua vigezo vya ukuaji uchumi ni Tofauti na Ustawi wa Jamii? Yule Profesa keshasema yeye haongelei porojo kama unazoleta hapa? Economic Growth na Welfare of Society ni Vitu viwili tofauti sio kwa Tanzania ni Dunia nzima ila Kwa kuwa wewe ni bwe.gwe ukatupa kalamu na kurukia ki laptop/PC chako kuwahi kuleta uj.inga wako. Thibitisha kuwa uchumi haukui kwa kiwango hicho, Hata Tafiti za WB na IFM zinasema the same thing, Ukuaji wa Uchumi hauzungumzii Mlo mmoja au kuishi chini ya Dola moja kwa siku hayo hayana uhusiano na Economic Growth, Shule mlipata vyeti badala ya elimu basi walau muwe mnazurura Mtaa GOOGLE mnaweza mkaziba viraka ya u.jinga vilivopo kichwani. Hapo kwenye Red umemlisha maneno Profesa Vipimo vya ukuaji wa uchumi havitumii vipimo vya CENTEMETR.

Wewe unapingana na mleta mada au unapingana na waziri muongo yeye alitamka hiyo CENTEMETR wewe unabisha tuambie basi alitamka nini.
 
Hahahahaha lol! kama hii ni kweli itakuwa ni kituko cha hali ya juu. Nitaisaka hii hotuba Utube.
Ni kweli kabisa na Huyu waziri kaniingiza nkenge ni kakurupuka kuchukua kalamu na Karatasi....ila alipoanza ku'justify' ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kuja Dar kwa mifano ya mabomba ya gesi ya Brazil kendwa Bolivia, Iran kwenda Pakstani huku akisisitisha kuwa kwake yeye kutoa mahesabu yake kwa dola za kimarekani ni rahisi zaidi kuliko pesa za kitanzania nikaona huyu bure kabisa.
 
Dah! Huyu uproffessor wake unaanza kutia shaka, maana madudu anayoongea hayaendani na mtu mwenye kiwango cha elimu aliyokuwa nayo.

Ni kweli kabisa na Huyu waziri kaniingiza nkenge ni kakurupuka kuchukua kalamu na Karatasi....ila alipoanza ku'justify' ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kuja Dar kwa mifano ya mabomba ya gesi ya Brazil kendwa Bolivia, Iran kwenda Pakstani huku akisisitisha kuwa kwake yeye kutoa mahesabu yake kwa dola za kimarekani ni rahisi zaidi kuliko pesa za kitanzania nikaona huyu bure kabisa.
 
Leo baada ya Kipindi cha Maswali na Majibu Bungeni nilibahatika kuwa karibu na TV huku nikiingalia TBC japo Sijisikii Vizuri kutizama kituo hiki cha TVCCM. Lakini kwa kua sikua na njia Mbadala kwani nilikua na hamu sana ya kumuona Waziri wa Nishati na Madini,mwenye Mbwembwe nyingi Prof Muhongo akihitimisha hotuba ya Bajet ya wizara yake.

Kama nilivyotarajia kweli alianza kwa kuikosoa Hotuba ya kambi ya upinzani kuwa ni ya Porojo na haina takwimu. Tena akawashauri wapinzani wakajifunze kwa Wafadhili wao jinsi ya kuwasilisha Bajet ya Upinzani.
Hakuishia hapo bali alimkosoa Sendeka kwa kumuita Muongo anaemlisha Mh rais maneno ambayo hakuyasema.

Baadae nilimshangaa wakati akiwasisitiza Wabunge na wananchi kua kila mmoja anae msikiliza achukue,Kalamu na Karatasi kwani anaenda kutoa Takwimu Kisayansi na sio Porojo! Pale na mimi nikachukua Kalamu na Karatasi.Hakika baada ya kuelezea mambo ya ujenzi wa Bomba la gesi kutoka Mtwara kuja Dar km Zaidi ya 400 na kufananisha garama na umbali wa ujenzi wa bomba la nchini China km 8000,Naigeria 500,Brazil 400na Ujerumani kwa hakika nikajua kweli huyu ndie Profesa.
Likaja swala la ukuaji wa Uchumi.Hapo ndipo niligundua kwamba jamaa anasoma vitu vya kuambiwa baada ya KUSEMA KUWA UCHUMI WA TANZANIA UNAKUA KWA CENTEMETRE 6 HADI 7 kwa Mwaka. Hakika baada ya kusikia hivyo nilitupa kalamu na kusema Kimoyomoyo kumbe Profesa ni Mtupu na hana tofauti na Prof Maji Marefu!!
acheni upumb.avu, tuache siasa cha uchochoroni, KATI YA MAWAZIRI BORA TZ muhongo ni mmoja wapo. kama mnashida na usomi wake, huyu ni profesa alikuwa anafundisha universities kule south africa, alikuwa na opportunities kimataifa lakini jk alipoona ni mtu muhimu alimwita akaja alitumikie taifa.

kwahabari ya kumuua mkewe, nilikuwa sijui kama hana mke, alimuuaje jamani...kwakweli siasa ni mchezo mchafu. kama kweli alifanya icho kitu, tunaomba mtujuze kwasababu kwa upande wangu, hata kama mtuu ni mzuri sana, kama alifanya mauaji ya mtu asiye na hatia, huyo hatufai. please tell us how he killed his wife...
 
Waziri Muhongo...
Umeonyesha umahiri mkubwa wa kuongea na kuonyesha kwamba unayoyawasilisha una uhakika nayo. Lakini kumbuka wizara unayoiongoza ni sensitive zaidi ya unavyofikiria.
Kumbuka kauli yako uliyotoa miezi kadhaa iliyopita 'kuwatukana' watu wa Mtwara kuwa ni wapumbavu na wabinafsi ni mojawapo ya kauli zililolifikisha taifa hapa lilipo juu ya ishu ya Mtwara.
Umekuwa mwepesi sana wa kukosoa kwa kejeli na majivuno makubwa na kuonyesha kwamba unayoyawaza wewe tu ndiyo sahihi. Pengine ni kweli maana wewe ni profesa... msomi na hakuna msomi kama wewe hapa Tanzania. Lakini kumbuka tu kitu kimoja,... hao unaowadharau na kuwaona wapumbavu kuna siku utahitaji kuungwa nao mkono ili hiyo mipango yako ya kiprofesa itekelezwe
Waziri Muhongo, nimesikitishwa zaidi na namna unavyolishughulikia suala la Mtwara kwa kuita mawazo yeyote mbadala kuwa ni "porojo". Lakini umesahau kuwa hawa unaowaambia wanapiga porojo wana ushawishi mkubwa katika jamii, wanakubalika na wengi katika jamii na wana nafasi kubwa sana katika jamii. Kama profesa nilitarajia kuwa majibu yako kwa maoni ya kambi ya upinzani yawe ya kidiplomasia zaidi. Nilitarajia useme 'maoni ya kambi ya upinzani tumeyasikia, tutajitahidi kuyafanyika kazi yale yenye manufaa kwa wananchi'... kisha ukaendelea na hotuba yako. Si ndivyo mnavyotufundisha hata huko vyuo vikuu profesa? Kwamba unapotakiwa kutetea hoja yako katika jambo lililo tense basi uwe diplomatically neutral?
Hivi profesa unadhani wananchi wa Mtwara na sehemu nyingine walioshika kalamu na karatasi jana walikuwa wangapi?
Hivi profesa unadhani kwa kutengeneza unnecessary "bifu" na wapinzani ndio utakuwa umeshinda mchezo?
Pinda anaenda Mtwara sasa, kujadiliana na "wapiga porojo", na watamuuliza umekuja kusikiliza porojo zetu?

Mheshimiwa profesa, mimi sina ueledi wowote wa kukushauri, lakini nakuomba kuanzia sasa kabla hujaja kutusomea hotuba zako za takwimu, walau zipitishe kwa "afisa mahusiano ya jamii" wa wizara yako apitishe hapo macho...
 
Ongea kwa Takwimu badala ya porojo, Kama huwezi kuandaa Hoja nenda kaige kwa Wafadhili wenu- Professor Sospeter Muhongo.
 
mmmmh napita tu ntarudi nikiwa na hoja nzito za kujibu.....
 
Waziri Muhongo...
Umeonyesha umahiri mkubwa wa kuongea na kuonyesha kwamba unayoyawasilisha una uhakika nayo. Lakini kumbuka wizara unayoiongoza ni sensitive zaidi ya unavyofikiria.
Kumbuka kauli yako uliyotoa miezi kadhaa iliyopita 'kuwatukana' watu wa Mtwara kuwa ni wapumbavu na wabinafsi ni mojawapo ya kauli zililolifikisha taifa hapa lilipo juu ya ishu ya Mtwara.
Umekuwa mwepesi sana wa kukosoa kwa kejeli na majivuno makubwa na kuonyesha kwamba unayoyawaza wewe tu ndiyo sahihi. Pengine ni kweli maana wewe ni profesa... msomi na hakuna msomi kama wewe hapa Tanzania. Lakini kumbuka tu kitu kimoja,... hao unaowadharau na kuwaona wapumbavu kuna siku utahitaji kuungwa nao mkono ili hiyo mipango yako ya kiprofesa itekelezwe
Waziri Muhongo, nimesikitishwa zaidi na namna unavyolishughulikia suala la Mtwara kwa kuita mawazo yeyote mbadala kuwa ni "porojo". Lakini umesahau kuwa hawa unaowaambia wanapiga porojo wana ushawishi mkubwa katika jamii, wanakubalika na wengi katika jamii na wana nafasi kubwa sana katika jamii. Kama profesa nilitarajia kuwa majibu yako kwa maoni ya kambi ya upinzani yawe ya kidiplomasia zaidi. Nilitarajia useme 'maoni ya kambi ya upinzani tumeyasikia, tutajitahidi kuyafanyika kazi yale yenye manufaa kwa wananchi'... kisha ukaendelea na hotuba yako. Si ndivyo mnavyotufundisha hata huko vyuo vikuu profesa? Kwamba unapotakiwa kutetea hoja yako katika jambo lililo tense basi uwe diplomatically neutral?
iHivi profesa unadhani wananchi wa Mtwara na sehemu nyingine walioshika kalamu na karatasi jana walikuwa wangapi?
Hivi profesa unadhani kwa kutengeneza unnecessary "bifu" na wapinzani ndio utakuwa umeshinda mchezo?
Pinda anaenda Mtwara sasa, kujadiliana na "wapiga porojo", na watamuuliza umekuja kusikiliza porojo zetu?

Mheshimiwa profesa, mimi sina ueledi wowote wa kukushauri, lakini nakuomba kuanzia sasa kabla hujaja kutusomea hotuba zako za takwimu, walau zipitishe kwa "afisa mahusiano ya jamii" wa wizara yako apitishe hapo macho...

Angalia sana huyo chura ni muuwaji. Asije kukuua
Alimuua mkewe. Mropokaji mkubwa. Eti profesa, pengine profesa maji marefu
 
Angalia sana huyo chura ni muuwaji. Asije kukuua
Alimuua mkewe. Mropokaji mkubwa. Eti profesa, pengine profesa maji marefu

Mkuu hata asiponiua yeye najua kuna siku nitakufa... Hamna sababu ya kumuogopa.
 
Dah! Huyu uproffessor wake unaanza kutia shaka, maana madudu anayoongea hayaendani na mtu mwenye kiwango cha elimu aliyokuwa nayo.

Unajua mimi nina wasiwasi JK alimjua huyu jamaa kuwa ni professa wa vitabu wala si professa mwenye weledi. Na ili afanikiwe kuwa demolize wasomi wa tanzania wanaolalamika kuwa wakitoa ushauri hawasikilizwi akaona umuweke huyu 'prof.' apate kisingizio cha kuataa ushauri wao kuwa ushauri wao, wasomi wanatoa ushauri bila kujari utu, hekima, busara na weledi kutaja machache ya namna hiyo.
 
Mkuu RevolutionaryTZ sorry hii ishu ya huyu Chura kumuua mkewe mbona siielewi? Naiona humu mara kadhaa sasa hebu weka mambo hadharani kinagaubaga..
 
Back
Top Bottom