Prof. Mbarawa fanya mabadiliko kituo cha Ubungo kiwe cha daladala na SIMU 2000 kiwe mabasi ya mikoa

mgt software

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
13,767
7,115
Mh. Waziri muda mrefu abiria tunaopenda kutumia mwendo kasi tunaumia sana, umbali kutoka m2000 mpaka ubungo stand kufuata mwendo kasi mkubwa, kupitia wakala wa barabara badilisha hizi stand, ya ubungo iwe ya daladala na simu 2000 yawe ya mabasi ya mikoani, hapo utakuwa umeondoa usumbufu. Mfano ukitoka Tegeta au kawe kama unawahi mjini ukitumia mabasi ya mwendokasi inaturahiaishia. Hatujui aliyebuni kituo hiki alifikiria nini mpaka tukapata adhabu hii. Leo hii barabara ya kuingia huko simu 2000 haitamamaniki. Abiria tunachelewa makazini tukiangaika na mabasi yanayoruka matuta.
 
Tatizo stendi wanataka kuingia si yalale humo humo huo ni upuuuzi.... Mabasi yakishusha abiria ni kusepa kutafuta parking
Umeona ndio maana ikaitwa basi stand sio basi parking, mabasi yapewe ratiba ya kuingua na kutoka hapo nafasi kibao, kuliko kutesa abilia kutoka mawasiliano kwenda ubungo mataa. Mbalawa ajaribu kupanda basi kutoka bunju hadi ubungo mwendokasi alafu atupe jibu.
 
, kupitia wakala wa barabara badilisha hizi stand, ya ubungo iwe ya daladala na simu 2000 yawe ya mabasi ya mikoani, hapo utakuwa umeondoa usumbufu. .
Daah! Mshikaji sina cha kusema zaidi ya kusema kuwa wewe ni 'The akili kubwaz, le Mutuz haingizi mguu kwako'... Hiyo ingekaa poa sana kwa ku connect usafiri wa dala dala...
 
We jamaa mbinafsi saana yaani vituo vibadilishwe kisa tuu unapata usumbufu wa kwenda kupanda mwendokasi......kama hoja yako ni usumbufu hata vituo vikibadilishwa ili kukupunguzia usumbufu ww kuna watu wengine utakuwa umewa sababishia usumbufu huo(mfano wapanda mwendokasi toka Kariakoo na Kimara na wapanda dala dala wa Tabata na Buguruni) watakao kuwa wanaenda kupanda magari/Mabasi ya Mkoa.
 
Kituo cha Simu 2000 hakifai kuwa kituo cha mabasi ya mkoa. Ni kidogo mno mno mno. Pia hakina huduma inazahitajika kwa kazi kubwa hivyo.

Tuache kufanya vitu temporary kama vile tuko kwenye rehersal.

Hivi vituo ni fursa za mapato kwa Halmashauri. Nashauri halmashauri husika zitenge maeneo (Kinondoni kwa ajili ya mabasi ya Kaskazini, Temeke kwaabasi ya Kusini na Kinondoni tena kwa ajili ya Njia ya Kati). Wakishatenga hayo maeneo, watengeneze michoro na kutengeza business plan. Baada ya hapo watafute mikopo ya benki au wadau wa PPP wajenge hivyo vituo. Walahi nakuambia vitalipa.

Tuchukue mfano wa kituo cha Boko kwa ajili ya mabasi ya Kaskazini;

1. Halmashauri inatoa ardhi na master plan

2. Kituo cha shelli wanajenga Total kwa mfano

3. Vyumba vya ofisi wanajenga wadau kwa kuzungatia michoro. Wadau wanakuja kuvipangisha kwa maopereta wa mabasi na wauza maduka

4. Motel kwa ajili ya wasafiri zinajengwa na wadau wajasiriamali kwa vigezo walivyopewa.

5. Vyoo na mabafu wanajenga wadau wajasiriamali kwa viwango vikali walivyopewa na Halmashauri

6. Maegesho ya mabasi na yanajengwa kwa kiwango cha lami na Halmashauri.

7. Zahanati, zimamoto, police station, na ofisi kuu zinajengwa na Halmashauri

Unakuwa unemaliza kazi. Tuiache serikali kuu ifanye mambo makubwa zaidi.
 
Mh. Waziri muda mrefu abiria tunaopenda kutumia mwendo kasi tunaumia sana, umbali kutoka m2000 mpaka ubungo stand kufuata mwendo kasi mkubwa, kupitia wakala wa barabara badilisha hizi stand, ya ubungo iwe ya daladala na simu 2000 yawe ya mabasi ya mikoani, hapo utakuwa umeondoa usumbufu. Mfano ukitoka Tegeta au kawe kama unawahi mjini ukitumia mabasi ya mwendokasi inaturahiaishia. Hatujui aliyebuni kituo hiki alifikiria nini mpaka tukapata adhabu hii. Leo hii barabara ya kuingia huko simu 2000 haitamamaniki. Abiria tunachelewa makazini tukiangaika na mabasi yanayoruka matuta.
hii iko sawa sanaa jamaa
 
Ukitaka yafiti inawezekana, mabasi ya tanga, moshi arusha yahamishiwe bunju karibu na daraja. Ya kusini yaanzie mbagara, baadhi ya dom na mbeya yaanzie kibaha. Hapo no foleni na mwendo kasi itaendeshwa kwa faida.
Sawa kabisa.... Ya Kilimanjaro Arusha na Tanga yaishie Maili Moja...
 
Kwa mara ya kwanza mtoa post kaongea pumba, sijui kapatwa na nini leo. reseach uliyofanya wewe haina kiwango hivyo nakupa 5% kwa leo hadi ujirekebishe na reseach zako
 
Kwa mara ya kwanza mtoa post kaongea pumba, sijui kapatwa na nini leo. reseach uliyofanya wewe haina kiwango hivyo nakupa 5% kwa leo hadi ujirekebishe na reseach zako
MZee Falcon hata 5 inanitosha kwani aliyebuni kituo hicho sumbufu ana 0.005%
 
Back
Top Bottom