Prof. Mark Mwandosya ni mpotoshaji

Prof. Mark Mwandosya ni mpotoshaji

Aisee. Mwambie Mwenyekiti amfukuze chamamani. FAHAMU kuna makabila Tanzania wanapendana no matter what na mfano ni wa kutoka Mbeya, Kilimanjaro, Mikoa ya Wasukuma, Kanda ya Ziwa hapa Mara na Kagera. Hawa watu wana asili ya kwao. Na hata sasa inajidhihirisha wazi. Hivyo huwezi kuongelea la Sugu Mbeya. Na nikuambie kisiasa lina impact kubwa mno kwa wanambeya ninaowafahamu. Hapo kuna tension kubwa na Chama Changu ninawasihi muwe makini na msikurupuke.
 
Na Jumanne Lutengano Majoka
Mjasiriamali Mbeya Mjini.

Hakuna mashaka kuwa mapokezi ya bashasha na kauli aliyoiandika Prof. Mark Mwandosya katika ukurasa wake wa Twitter baada Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi “Sugu” kuachiwa kwa msamaha wa Rais hapo jana anaungana na kauli ya Sugu mwenyewe kuwa adhabu aliyoipata kwa kumtusi Rais ilikuwa ni kifungo cha kisiasa.

Kwa Prof. Mwandosya na Sugu mwenyewe ni vizuri kujiepusha na upotoshaji huu. Sugu alifungwa kwa kosa la jinai na hivyo alikuwa mfungwa wa kosa la jinai na sio mfungwa wa kisiasa kama anavyodai.

Mfungwa wa kisiasa ni mtu aliyefungwa jela kutokana na kujihusisha na shughuli ama imani za kisiasa. Hapa ndipo mtu kama Nelson Mandela anaitwa mfungwa wa kisiasa.

Lakini Sugu sio mfungwa wa kisiasa, Sugu ni mhalifu, alifanya makosa ya kuvunja sheria za nchi kwa kumtukana Rais. Hata utambulisho wake anaitwa Mfungwa namba 219/2018 na sio Mfungwa wa Kisiasa namba 219/2018 kama anavyodai na kama Prof. Mwandosya anavyounga mkono.

Hizi ni siasa za kipuuzi na zinapoungwa mkono na mtu mwenye utumishi kwa nchi kama Prof Mark Mwandosya inatia wingu zito na inavunja heshima.

Nimejiuliza sana kuhusu lengo la Prof. Mark Mwandosya kumpokea Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi “Sugu” aliyetolewa jana Mei 10, 2018 kwa msamaha wa Rais na ujumbe aliouandika kupitia ukurasa wake wa Twitter. Tena Prof. Mwandosya kafunga safari hadi nyumbani kwake Sugu kumpokea na kuandika alichoandika.

Kwa ambao hamjasoma alichopost Prof. Mwandosya, kapiga picha akiwa na Sugu nyumbani kwa Sugu kaandika hivi nanukuu “Nikimpa hongera Mbunge wa Mbeya Mhe.Joseph Mbilinyi kwa kuhitimu Chuo cha Uanasiasa,Gereza la Ruanda,Mbeya.Kutofautiana vyama,itikadi na misimamo kusilete uhasama na uadui.Mungu Ibariki Tanzania.

Na akaendelea kwa kimombo “Congratulating Hon.Joseph Mbilinyi-right after graduating from Ruanda Prison Mbeya”

Baadaye Sugu nae kapost picha kwenye Instagram wakiwa wamekaa na Prof Mwandosya nyumbani kwake Sugu na Prof Mwandosya akinywa juisi na kaandika “Nikiwa na Prof. Mwandosya nyumbani kwangu leo. Asante kwa maneno ya busara na ujasiri ulionipa leo na hata ulipokuja kuniona gerezani”

Ukiunganisha nukta za kauli za Prof. Mwandosya na Sugu haileti mashaka kuwa wanaongea lugha moja kwamba Sugu ni mfungwa wa kisiasa na wanataka kuaminisha umma kuwa Sugu alionewa kwa adhabu ile.

Niseme hivi kwa Sugu kutoa kauli hizo haina shida kwa sababu kwa namna yoyote baada ya kukumbwa na adhabu ile ilitarajiwa kuwa atataka kuitumia kwa manufaa ya kisiasa, lakini kwa Prof Mwandosya kuna ukakasi.

Kuna ukakasi kwa sababu Prof. Mwandosya ni Mwanachama wa CCM na aliyetukanwa na Sugu ni Mwenyekiti wake. Kwa alichokiandika Prof. Mwandosya ni wazi kuwa anaamini Sugu alionewa na anamtia moyo kuwa amefuzu chuo cha uanasiasa katika gereza la Ruanda. Anaamini kuwa Rais Magufuli alistahili kutukanwa vile na Sugu na hakubaliani na adhabu aliyopewa na mahakama kwa mujibu wa sheria.

Prof. Mark Mwandosya ni Mwenyekiti wa Bodi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ambacho awali kilifanya kazi ya kutengeneza makada na sasa kinafundisha kozi mbalimbali za uongozi, siasa, uchumi n.k. Aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa chuo hiki na Rais Magufuli ambaye ametukanwa na Sugu na hakukataa uteuzi huu.

Prof. Mwandosya ni Waziri mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne na ni mtu aliyejitokeza mara mbili kutaka ridhaa ya wana CCM ili agombee kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila mafanikio.

Kwa miaka takribani 7 sasa Prof. Mwandosya amekuwa akisumbuliwa na maradhi makubwa ambayo yamelazimu awe anapatiwa matibabu nchini India kwa gharama za Serikali. Hata sasa anaishi na vyuma ambavyo anahitaji kupatiwa matibabu nje ya nchi.

Kwa mazingira hayo hapo juu, Prof. Mwandosya angepaswa kuwa makini na kauli zake na ikiwezekana aamue moja ama kujipambanua kuwa yeye sasa anaunga mkono siasa za upinzani na kujihusisha na upinzani kwa uwazi ama kuchunga kauli zake. Aamue ama kuwa moto ama kuwa baridi aache double standards.

Ni jambo linalokanganya kwamba anatumikia cheo alichopewa na Rais Magufuli, anatibiwa na Serikali inayoongozwa na Rais Magufuli na ni mwanachama wa chama kinachoongozwa na Rais Magufuli halafu anamuunga mkono mtu anayemtukana Rais Magufuli.

Na hii sio mara ya kwanza kwa Prof. Mwandosya kufanya double standards hizi. Mwaka 2015 alipokosa kuteuliwa kugombea Urais kupitia CCM aliibuka na kumshambulia Mwenyekiti wake Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, akipinga mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM.

Ilitushangaza wengi kwa sababu Prof. Mwandosya alipaswa kujua kwa nini chama kiliamua kumteua Magufuli na angepaswa kuelewa hata manufaa ambayo chama kimeyapata maana ni wazi kwamba kama wangepitishwa waliokuwa wanatajwatajwa pengine chama kingepoteza kwenye uchaguzi mkuu.

Nakusihi Prof Mwandosya kama una mahaba na upinzani hamia huko, mimi kama Mtanzania ninayeamini katika utawala wa sheria, na ninajitahidi kupambanua mambo kwa maslahi ya Taifa naona unachokifanya sio sawa, kama wanavyosema vijana inawezekana unataka kupata Kiki au uendelee kupata umaarufu wa kisiasa, lakini kwa heshima yako hili unalolifanya unakuwa Kivuruge.

Sipendezwi na aina ya siasa zinazofanywa na upinzani na ni miongoni mwa watu wanaopenda kuwepo upinzani wenye tija na sio upinzani unalivuruga Taifa kama huu tulionao Tanzania. Tuna upinzania ambao hauna dalili za kushika dola na hauna tija.

Namsihi Rais Magufuli kuwa makini na Prof. Mwandosya, tunaojua mienendo ya kisiasa tunajua kuwa huyu ana visilani vya kisiasa na alihofiwa sana kwa siasa za ukanda.

Alituhumiwa hivyo kutokana na namna alivyofanya siasa zake mwaka 2005 alipochuana na Jakaya Kikwete katika ngazi ya chama. Kwa wakati ule zilikuwa ni nguvu za mtandao. Mtandao wa Prof. Mwandosya ulibeba sura ya kikanda zaidi.

Nionavyo mimi kama Prof. Mwandosya hatojisahihisha ni wakati sasa wa Rais Magufuli kumuengua katika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kilichopo Kigamboni. Aachwe huru ili afanye siasa za upinzani kwa uhuru zaidi, aungane na Sugu na wanasiasa wengine wa upinzani kufanya siasa bora zaidi.

Prof Mwandosya aamue kuwa baridi au kuwa moto.

Mimi ni mwananchi wa Tanzania
Naitwa Jumanne Lutengano Majoka.
Unaandika sana lakini hakuna cha maana ulichoandika.
Ungeelewa Muktadha wa swala zima lilivyokua usingeandika huu utumbo hapo juu.
Maneno aliyoyatoa Sugu mpaka akakamatwa hakuyatoa Akiwa Kanisani, Bar au Mpirani. Maneno hayo aliyatolea kwenye Jukwaa la Siasa, alikua akifanya Siasa ndio maana akakamatwa na Kufungwa.

Pili Unamshambulia Mwandosya kwa mambo ambayo hayahusiani na huu Muktadha. Ugonjwa wake, siasa alizofanya mwaka 2005, Uenyekiti wake wa Bodi havitengui wala kuhusiana na kile alichokisema wakati akimpokea Sugu.
 
Na Jumanne Lutengano Majoka
Mjasiriamali Mbeya Mjini.

Hakuna mashaka kuwa mapokezi ya bashasha na kauli aliyoiandika Prof. Mark Mwandosya katika ukurasa wake wa Twitter baada Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi “Sugu” kuachiwa kwa msamaha wa Rais hapo jana anaungana na kauli ya Sugu mwenyewe kuwa adhabu aliyoipata kwa kumtusi Rais ilikuwa ni kifungo cha kisiasa.

Kwa Prof. Mwandosya na Sugu mwenyewe ni vizuri kujiepusha na upotoshaji huu. Sugu alifungwa kwa kosa la jinai na hivyo alikuwa mfungwa wa kosa la jinai na sio mfungwa wa kisiasa kama anavyodai.

Mfungwa wa kisiasa ni mtu aliyefungwa jela kutokana na kujihusisha na shughuli ama imani za kisiasa. Hapa ndipo mtu kama Nelson Mandela anaitwa mfungwa wa kisiasa.

Lakini Sugu sio mfungwa wa kisiasa, Sugu ni mhalifu, alifanya makosa ya kuvunja sheria za nchi kwa kumtukana Rais. Hata utambulisho wake anaitwa Mfungwa namba 219/2018 na sio Mfungwa wa Kisiasa namba 219/2018 kama anavyodai na kama Prof. Mwandosya anavyounga mkono.

Hizi ni siasa za kipuuzi na zinapoungwa mkono na mtu mwenye utumishi kwa nchi kama Prof Mark Mwandosya inatia wingu zito na inavunja heshima.

Nimejiuliza sana kuhusu lengo la Prof. Mark Mwandosya kumpokea Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi “Sugu” aliyetolewa jana Mei 10, 2018 kwa msamaha wa Rais na ujumbe aliouandika kupitia ukurasa wake wa Twitter. Tena Prof. Mwandosya kafunga safari hadi nyumbani kwake Sugu kumpokea na kuandika alichoandika.

Kwa ambao hamjasoma alichopost Prof. Mwandosya, kapiga picha akiwa na Sugu nyumbani kwa Sugu kaandika hivi nanukuu “Nikimpa hongera Mbunge wa Mbeya Mhe.Joseph Mbilinyi kwa kuhitimu Chuo cha Uanasiasa,Gereza la Ruanda,Mbeya.Kutofautiana vyama,itikadi na misimamo kusilete uhasama na uadui.Mungu Ibariki Tanzania.

Na akaendelea kwa kimombo “Congratulating Hon.Joseph Mbilinyi-right after graduating from Ruanda Prison Mbeya”

Baadaye Sugu nae kapost picha kwenye Instagram wakiwa wamekaa na Prof Mwandosya nyumbani kwake Sugu na Prof Mwandosya akinywa juisi na kaandika “Nikiwa na Prof. Mwandosya nyumbani kwangu leo. Asante kwa maneno ya busara na ujasiri ulionipa leo na hata ulipokuja kuniona gerezani”

Ukiunganisha nukta za kauli za Prof. Mwandosya na Sugu haileti mashaka kuwa wanaongea lugha moja kwamba Sugu ni mfungwa wa kisiasa na wanataka kuaminisha umma kuwa Sugu alionewa kwa adhabu ile.

Niseme hivi kwa Sugu kutoa kauli hizo haina shida kwa sababu kwa namna yoyote baada ya kukumbwa na adhabu ile ilitarajiwa kuwa atataka kuitumia kwa manufaa ya kisiasa, lakini kwa Prof Mwandosya kuna ukakasi.

Kuna ukakasi kwa sababu Prof. Mwandosya ni Mwanachama wa CCM na aliyetukanwa na Sugu ni Mwenyekiti wake. Kwa alichokiandika Prof. Mwandosya ni wazi kuwa anaamini Sugu alionewa na anamtia moyo kuwa amefuzu chuo cha uanasiasa katika gereza la Ruanda. Anaamini kuwa Rais Magufuli alistahili kutukanwa vile na Sugu na hakubaliani na adhabu aliyopewa na mahakama kwa mujibu wa sheria.

Prof. Mark Mwandosya ni Mwenyekiti wa Bodi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ambacho awali kilifanya kazi ya kutengeneza makada na sasa kinafundisha kozi mbalimbali za uongozi, siasa, uchumi n.k. Aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa chuo hiki na Rais Magufuli ambaye ametukanwa na Sugu na hakukataa uteuzi huu.

Prof. Mwandosya ni Waziri mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne na ni mtu aliyejitokeza mara mbili kutaka ridhaa ya wana CCM ili agombee kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila mafanikio.

Kwa miaka takribani 7 sasa Prof. Mwandosya amekuwa akisumbuliwa na maradhi makubwa ambayo yamelazimu awe anapatiwa matibabu nchini India kwa gharama za Serikali. Hata sasa anaishi na vyuma ambavyo anahitaji kupatiwa matibabu nje ya nchi.

Kwa mazingira hayo hapo juu, Prof. Mwandosya angepaswa kuwa makini na kauli zake na ikiwezekana aamue moja ama kujipambanua kuwa yeye sasa anaunga mkono siasa za upinzani na kujihusisha na upinzani kwa uwazi ama kuchunga kauli zake. Aamue ama kuwa moto ama kuwa baridi aache double standards.

Ni jambo linalokanganya kwamba anatumikia cheo alichopewa na Rais Magufuli, anatibiwa na Serikali inayoongozwa na Rais Magufuli na ni mwanachama wa chama kinachoongozwa na Rais Magufuli halafu anamuunga mkono mtu anayemtukana Rais Magufuli.

Na hii sio mara ya kwanza kwa Prof. Mwandosya kufanya double standards hizi. Mwaka 2015 alipokosa kuteuliwa kugombea Urais kupitia CCM aliibuka na kumshambulia Mwenyekiti wake Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, akipinga mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM.

Ilitushangaza wengi kwa sababu Prof. Mwandosya alipaswa kujua kwa nini chama kiliamua kumteua Magufuli na angepaswa kuelewa hata manufaa ambayo chama kimeyapata maana ni wazi kwamba kama wangepitishwa waliokuwa wanatajwatajwa pengine chama kingepoteza kwenye uchaguzi mkuu.

Nakusihi Prof Mwandosya kama una mahaba na upinzani hamia huko, mimi kama Mtanzania ninayeamini katika utawala wa sheria, na ninajitahidi kupambanua mambo kwa maslahi ya Taifa naona unachokifanya sio sawa, kama wanavyosema vijana inawezekana unataka kupata Kiki au uendelee kupata umaarufu wa kisiasa, lakini kwa heshima yako hili unalolifanya unakuwa Kivuruge.

Sipendezwi na aina ya siasa zinazofanywa na upinzani na ni miongoni mwa watu wanaopenda kuwepo upinzani wenye tija na sio upinzani unalivuruga Taifa kama huu tulionao Tanzania. Tuna upinzania ambao hauna dalili za kushika dola na hauna tija.

Namsihi Rais Magufuli kuwa makini na Prof. Mwandosya, tunaojua mienendo ya kisiasa tunajua kuwa huyu ana visilani vya kisiasa na alihofiwa sana kwa siasa za ukanda.

Alituhumiwa hivyo kutokana na namna alivyofanya siasa zake mwaka 2005 alipochuana na Jakaya Kikwete katika ngazi ya chama. Kwa wakati ule zilikuwa ni nguvu za mtandao. Mtandao wa Prof. Mwandosya ulibeba sura ya kikanda zaidi.

Nionavyo mimi kama Prof. Mwandosya hatojisahihisha ni wakati sasa wa Rais Magufuli kumuengua katika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kilichopo Kigamboni. Aachwe huru ili afanye siasa za upinzani kwa uhuru zaidi, aungane na Sugu na wanasiasa wengine wa upinzani kufanya siasa bora zaidi.

Prof Mwandosya aamue kuwa baridi au kuwa moto.

Mimi ni mwananchi wa Tanzania
Naitwa Jumanne Lutengano Majoka.
Kwahiyo unataka tukuone wewe ni zaidi ya Prof. Mwandosya kwa uharo uliou-post hapa? Wenye kumwelewa Prof. Mwandosya tulishamwelewa. Vijineno vyako haviwezi kutufanya tufute tulichokisoma ktk maneno ya Prof. na Sugu mwenyewe kuhusiana na saga hili.
 
Na Jumanne Lutengano Majoka
Mjasiriamali Mbeya Mjini.

Hakuna mashaka kuwa mapokezi ya bashasha na kauli aliyoiandika Prof. Mark Mwandosya katika ukurasa wake wa Twitter baada Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi “Sugu” kuachiwa kwa msamaha wa Rais hapo jana anaungana na kauli ya Sugu mwenyewe kuwa adhabu aliyoipata kwa kumtusi Rais ilikuwa ni kifungo cha kisiasa.

Kwa Prof. Mwandosya na Sugu mwenyewe ni vizuri kujiepusha na upotoshaji huu. Sugu alifungwa kwa kosa la jinai na hivyo alikuwa mfungwa wa kosa la jinai na sio mfungwa wa kisiasa kama anavyodai.

Mfungwa wa kisiasa ni mtu aliyefungwa jela kutokana na kujihusisha na shughuli ama imani za kisiasa. Hapa ndipo mtu kama Nelson Mandela anaitwa mfungwa wa kisiasa.

Lakini Sugu sio mfungwa wa kisiasa, Sugu ni mhalifu, alifanya makosa ya kuvunja sheria za nchi kwa kumtukana Rais. Hata utambulisho wake anaitwa Mfungwa namba 219/2018 na sio Mfungwa wa Kisiasa namba 219/2018 kama anavyodai na kama Prof. Mwandosya anavyounga mkono.

Hizi ni siasa za kipuuzi na zinapoungwa mkono na mtu mwenye utumishi kwa nchi kama Prof Mark Mwandosya inatia wingu zito na inavunja heshima.

Nimejiuliza sana kuhusu lengo la Prof. Mark Mwandosya kumpokea Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi “Sugu” aliyetolewa jana Mei 10, 2018 kwa msamaha wa Rais na ujumbe aliouandika kupitia ukurasa wake wa Twitter. Tena Prof. Mwandosya kafunga safari hadi nyumbani kwake Sugu kumpokea na kuandika alichoandika.

Kwa ambao hamjasoma alichopost Prof. Mwandosya, kapiga picha akiwa na Sugu nyumbani kwa Sugu kaandika hivi nanukuu “Nikimpa hongera Mbunge wa Mbeya Mhe.Joseph Mbilinyi kwa kuhitimu Chuo cha Uanasiasa,Gereza la Ruanda,Mbeya.Kutofautiana vyama,itikadi na misimamo kusilete uhasama na uadui.Mungu Ibariki Tanzania.

Na akaendelea kwa kimombo “Congratulating Hon.Joseph Mbilinyi-right after graduating from Ruanda Prison Mbeya”

Baadaye Sugu nae kapost picha kwenye Instagram wakiwa wamekaa na Prof Mwandosya nyumbani kwake Sugu na Prof Mwandosya akinywa juisi na kaandika “Nikiwa na Prof. Mwandosya nyumbani kwangu leo. Asante kwa maneno ya busara na ujasiri ulionipa leo na hata ulipokuja kuniona gerezani”

Ukiunganisha nukta za kauli za Prof. Mwandosya na Sugu haileti mashaka kuwa wanaongea lugha moja kwamba Sugu ni mfungwa wa kisiasa na wanataka kuaminisha umma kuwa Sugu alionewa kwa adhabu ile.

Niseme hivi kwa Sugu kutoa kauli hizo haina shida kwa sababu kwa namna yoyote baada ya kukumbwa na adhabu ile ilitarajiwa kuwa atataka kuitumia kwa manufaa ya kisiasa, lakini kwa Prof Mwandosya kuna ukakasi.

Kuna ukakasi kwa sababu Prof. Mwandosya ni Mwanachama wa CCM na aliyetukanwa na Sugu ni Mwenyekiti wake. Kwa alichokiandika Prof. Mwandosya ni wazi kuwa anaamini Sugu alionewa na anamtia moyo kuwa amefuzu chuo cha uanasiasa katika gereza la Ruanda. Anaamini kuwa Rais Magufuli alistahili kutukanwa vile na Sugu na hakubaliani na adhabu aliyopewa na mahakama kwa mujibu wa sheria.

Prof. Mark Mwandosya ni Mwenyekiti wa Bodi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ambacho awali kilifanya kazi ya kutengeneza makada na sasa kinafundisha kozi mbalimbali za uongozi, siasa, uchumi n.k. Aliteuliwa kuwa Mwenyekiti wa chuo hiki na Rais Magufuli ambaye ametukanwa na Sugu na hakukataa uteuzi huu.

Prof. Mwandosya ni Waziri mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne na ni mtu aliyejitokeza mara mbili kutaka ridhaa ya wana CCM ili agombee kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila mafanikio.

Kwa miaka takribani 7 sasa Prof. Mwandosya amekuwa akisumbuliwa na maradhi makubwa ambayo yamelazimu awe anapatiwa matibabu nchini India kwa gharama za Serikali. Hata sasa anaishi na vyuma ambavyo anahitaji kupatiwa matibabu nje ya nchi.

Kwa mazingira hayo hapo juu, Prof. Mwandosya angepaswa kuwa makini na kauli zake na ikiwezekana aamue moja ama kujipambanua kuwa yeye sasa anaunga mkono siasa za upinzani na kujihusisha na upinzani kwa uwazi ama kuchunga kauli zake. Aamue ama kuwa moto ama kuwa baridi aache double standards.

Ni jambo linalokanganya kwamba anatumikia cheo alichopewa na Rais Magufuli, anatibiwa na Serikali inayoongozwa na Rais Magufuli na ni mwanachama wa chama kinachoongozwa na Rais Magufuli halafu anamuunga mkono mtu anayemtukana Rais Magufuli.

Na hii sio mara ya kwanza kwa Prof. Mwandosya kufanya double standards hizi. Mwaka 2015 alipokosa kuteuliwa kugombea Urais kupitia CCM aliibuka na kumshambulia Mwenyekiti wake Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, akipinga mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM.

Ilitushangaza wengi kwa sababu Prof. Mwandosya alipaswa kujua kwa nini chama kiliamua kumteua Magufuli na angepaswa kuelewa hata manufaa ambayo chama kimeyapata maana ni wazi kwamba kama wangepitishwa waliokuwa wanatajwatajwa pengine chama kingepoteza kwenye uchaguzi mkuu.

Nakusihi Prof Mwandosya kama una mahaba na upinzani hamia huko, mimi kama Mtanzania ninayeamini katika utawala wa sheria, na ninajitahidi kupambanua mambo kwa maslahi ya Taifa naona unachokifanya sio sawa, kama wanavyosema vijana inawezekana unataka kupata Kiki au uendelee kupata umaarufu wa kisiasa, lakini kwa heshima yako hili unalolifanya unakuwa Kivuruge.

Sipendezwi na aina ya siasa zinazofanywa na upinzani na ni miongoni mwa watu wanaopenda kuwepo upinzani wenye tija na sio upinzani unalivuruga Taifa kama huu tulionao Tanzania. Tuna upinzania ambao hauna dalili za kushika dola na hauna tija.

Namsihi Rais Magufuli kuwa makini na Prof. Mwandosya, tunaojua mienendo ya kisiasa tunajua kuwa huyu ana visilani vya kisiasa na alihofiwa sana kwa siasa za ukanda.

Alituhumiwa hivyo kutokana na namna alivyofanya siasa zake mwaka 2005 alipochuana na Jakaya Kikwete katika ngazi ya chama. Kwa wakati ule zilikuwa ni nguvu za mtandao. Mtandao wa Prof. Mwandosya ulibeba sura ya kikanda zaidi.

Nionavyo mimi kama Prof. Mwandosya hatojisahihisha ni wakati sasa wa Rais Magufuli kumuengua katika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kilichopo Kigamboni. Aachwe huru ili afanye siasa za upinzani kwa uhuru zaidi, aungane na Sugu na wanasiasa wengine wa upinzani kufanya siasa bora zaidi.

Prof Mwandosya aamue kuwa baridi au kuwa moto.

Mimi ni mwananchi wa Tanzania
Naitwa Jumanne Lutengano Majoka.


Sasa wewe Mbona umemdhalilisha prof kwa kutaja ugonjwa wake ns kusema sijui ana vyuma na hakuna atakayekupeleka mahakamani. Na pia umemwita MTU mzima mpotoshaji - matusi makubwa sana.
Na unamchagulia cha kuamin na kuandiia, inamchagulia marafiki- huo ni udhalilishaji na matusi kwa MTU mzima.
Alivyopelekwa nje kwa matibabu ilikuwa hisani au kwa mujibu wa sheria?
Huo uenyekiti wa Bodi ya chuo alituma barua ya maombi???
Kwa siasa za Tz ambazo wananchi wanafuata na kuamin watu badala ya itikadi, CCM inamwitaji Mwandosya huko nyanda za juu kusini kuliko anavyohiitaji ( angalia ya kanda ya kadkazini na ENL na kilichotokea katika election ta 2015).
Kwa hiyo utulie kijana, wenye busara kwenye chama watajua namna ya kuliweka kibusara zaidi.
 
Sio jambo jema kumpangia Prof Mwandosya aina ya marafiki. Ni mtu mzima, msomi na anazo akili timamu.

Kulitambua hilo ndio maana halisi ya ukomavu wa kisiasa na hata katika masuala ya mahusiano ya kibinadamu.
 
Wako wengi haina yake Prof Mwandosya ambao kwa kutoshwa na Serikali inayongozwa na Dr Magufuli, hawafichi hasira na chuki zao. Haitomsaidia katu.
Aliposhindwa kuteuliwa kugombea uraisi kupitia CCM jina lake lilipokatwa hasira zake zilianzia pale
 
Mwandosya kafanya kitu gani cha kukumbukwa kwenye utumishi wake katika taifa hili?? Hata CCM walishamkataa amegombea mara mbili kwenye kura za maoni ya uraisi lakini hakupata kitu!! Sasa uprofesa wake unatusaidia nini sasa?? Ana stress za kushindwa kwenye kura za maoni mara mbili. Aende huko hatusaidii kitu kama Chadema wanafikiri atawasaidia wampendekeze kugombea uraisi 2020 apambane na Raisi Magufuli tuone nani zaidi.

Tuambie ni akina nao hao waliofanya ya kufaa na ni yepi??
Usiwe na za mkizi, kutofautiana mtazamo sio uadui?? Chuki ya nini?
Why unune wenzio wanapofurahia ndugu yao kumaliza kifungo??? .
Tulis tafakari ni sababu gani zinakufanya utoe povu kiwango hiki??? Why??
 
prof Mwandosya ana akili kukuzidi wewe mtoa mada, tulia kimya
 
yaani nyie kiongozi yeyote anayeongea ukweli ni adui wa Rais sasa mbona kama vile tutakuwa ni Taifa la ndio mzee jambo ambalo sio sawa, kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake kadiri ya utashi wake, nami nakubaliana sana na prof na wala musimkashifu mzee wa wakati anajua alichozungumza
 
Ninasikia hata Mbeya hajafanya kitu chochote. Mbeya vijana wengi ninasikia ni wasomi na ni jobless, naambiwa hajafanya chochote na ni mselfish. Mbeya wanamkumbuka Mwakangale, Mwambulukutu, Mwaikambo kidogo kwa mbali sasa wanatumaini na Dr Tulia. Mwandosya ni mtu wa Visasi na Hana msaada Wowote kwenye Chama au serikali Mbeya. Ukiona kijana wa Mbeya yupo kwenye nafasi yoyote Jua kajipigania na si kwa sababu ya Mwandosya
 
Sio jambo jema kumpangia Prof Mwandosya aina ya marafiki. Ni mtu mzima, msomi na anazo akili timamu.

Kulitambua hilo ndio maana halisi ya ukomavu wa kisiasa na hata katika masuala ya mahusiano ya kibinadamu.
Kuna umri ukifika ukastaafu Ni vizuri kuendelea na Mambo mengine Kama kulea wewajukuu nk sio kuendelea na Yale uliyostaafia .Mwandosya umri umeenda Bado anaota siasa na wazee wenzie akna Sumaye
 
Aliposhindwa kuteuliwa kugombea uraisi kupitia CCM jina lake lilipokatwa hasira zake zilianzia pale

Mtasema mengi.Siku hazigandi , sugu katoka gerezani. Hata ingekuwa miaka 20 ingeisha tu.
Msifikiri kila MTU alifurahia kushitakiwa na hatimaye kufungwa kwa Sugu.
 
Hakuna haja ya kutetea sana uhalali wa kesi na hukumu ya Sugu. Dunia inajua na Watanzania wote wanajua juu ya kesi ya Sugu, mwenendo wa hakimu, polisi na upande wa mashitaka.

Vv
 
Soma vizuri sababu za kisheria za Nelson Mandela kufungwa. Kwa makaburu, Mandela alifanya na kufungwa kwa makosa ya jinai. Actually, kwa definition yako ya wafungwa was kisiasa hakuna hata mmoja katika uliowataja au unaowajua mbao ni wafungwa wa kisiasa.....wengi ya tunaowajua walifungwa kwa makosa ya jinai! Kote shida huwa ni tafsiri ya hizo jinai....watawala huweka sheria (zisizokubalika, za kibaguzi), ukikataa hiyo ni jinai tu. Hakuna katika sheria zetu na za wengine adhabu za kifungo kwa "makosa ya kisiasa". Ukiona mtu kafungwa, ujue ni jinai tu kwa mujibu wa watawala.

CCM wakitukana wapinzani sio jinai ni siasa, wapinzani wakitukana watakatifu wa kijani ni jinai!
 
Lumumba kuna tatizo kubwa. Yatakiwa uwe na ujivunie kuwa mnafiki. Uwe msharika wa ibada ya kumsifu na kumshangilia Mfalme Jiwe kwa kila kitu.
 
Back
Top Bottom