kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, amesema bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012, inayotarajiwa kusomwa katika Mkutano ujao wa Bunge, itakuwa ngumu.
Aliyasema hayo jana alipozungumza katika mahojiano maalum na NIPASHE, ofisini kwake, jijini Dar es Salaam juzi.
Alisema ugumu wa bajeti hiyo, unatokana na viashiria kuonyesha uwezekano mkubwa wa nchi wafadhili na taasisi wahisani duniani wanaosaidia bajeti ya serikali kupunguza misaada yao katika bajeti ya mwaka huu.
"Bajeti ya mwaka huu itakuwa ngumu, ngumu, ngumu sana," alisema Profesa Lipumba alipotakiwa na NIPASHE kutoa maoni yake kwamba, nini kifanyike ili hali iwe nzuri katika bajeti ya mwaka huu.
Profesa Lipumba alisema nchi wafadhili na taasisi wahisani zinazosaidia bajeti ya serikali, zitapunguza misaada yao kutokana na baadhi yao kukabiliwa na matatizo ya kiuchumi na nyingine kuchukizwa na mambo kadhaa yanayofanywa na serikali ya Tanzania. Baadhi ya mambo hayo, ni pamoja na usimamizi mbaya wa fedha, ambazo serikali hupata.
"Nchi za Ulaya zinapunguza misaada. Kwa mfano kama Ireland wana matatizo. Sasa kama walikuwa wakikusaidia dola milioni 6, hawawezi kukusaidia tena kiasi walichokuwa wakikusaidia," alisema Profesa Lipumba. Alisema Uholanzi ni miongoni mwa nchi wafadhili, ambazo hazifurahishwi na serikali inavyosimamia fedha inazopata.
Alisema kielelezo kimojawapo kinachothibitisha usimamizi mbaya wa fedha za umma, ni upotevu wa mabilioni ya shilingi kwa mwezi unaosababishwa na vitendo vya uchakachuaji ubora wa mafuta vilivyokithiri nchini. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Charles Mwijage, kumekuwa na takwimu tofauti za kiasi cha fedha, ambazo serikali hupoteza kwa mwezi kutokana na vitendo vya uchakachuaji ubora wa mafuta nchini.
Mwijage, ambaye pia ni Mbunge wa Muleba Kaskazini (CCM), alisema tofauti hiyo inaonekana katika taarifa ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ambayo inaeleza kuwa fedha, ambazo serikali hupoteza kwa mwezi kutokana na uchakachuaji ubora wa mafuta ni Sh. bilioni 25.
Aliyasema hayo jana alipozungumza katika mahojiano maalum na NIPASHE, ofisini kwake, jijini Dar es Salaam juzi.
Alisema ugumu wa bajeti hiyo, unatokana na viashiria kuonyesha uwezekano mkubwa wa nchi wafadhili na taasisi wahisani duniani wanaosaidia bajeti ya serikali kupunguza misaada yao katika bajeti ya mwaka huu.
"Bajeti ya mwaka huu itakuwa ngumu, ngumu, ngumu sana," alisema Profesa Lipumba alipotakiwa na NIPASHE kutoa maoni yake kwamba, nini kifanyike ili hali iwe nzuri katika bajeti ya mwaka huu.
Profesa Lipumba alisema nchi wafadhili na taasisi wahisani zinazosaidia bajeti ya serikali, zitapunguza misaada yao kutokana na baadhi yao kukabiliwa na matatizo ya kiuchumi na nyingine kuchukizwa na mambo kadhaa yanayofanywa na serikali ya Tanzania. Baadhi ya mambo hayo, ni pamoja na usimamizi mbaya wa fedha, ambazo serikali hupata.
"Nchi za Ulaya zinapunguza misaada. Kwa mfano kama Ireland wana matatizo. Sasa kama walikuwa wakikusaidia dola milioni 6, hawawezi kukusaidia tena kiasi walichokuwa wakikusaidia," alisema Profesa Lipumba. Alisema Uholanzi ni miongoni mwa nchi wafadhili, ambazo hazifurahishwi na serikali inavyosimamia fedha inazopata.
Alisema kielelezo kimojawapo kinachothibitisha usimamizi mbaya wa fedha za umma, ni upotevu wa mabilioni ya shilingi kwa mwezi unaosababishwa na vitendo vya uchakachuaji ubora wa mafuta vilivyokithiri nchini. Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Charles Mwijage, kumekuwa na takwimu tofauti za kiasi cha fedha, ambazo serikali hupoteza kwa mwezi kutokana na vitendo vya uchakachuaji ubora wa mafuta nchini.
Mwijage, ambaye pia ni Mbunge wa Muleba Kaskazini (CCM), alisema tofauti hiyo inaonekana katika taarifa ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ambayo inaeleza kuwa fedha, ambazo serikali hupoteza kwa mwezi kutokana na uchakachuaji ubora wa mafuta ni Sh. bilioni 25.