Prof. Lipumba ataka suluhu na Maalim Seif

Prof. Lipumba ataka suluhu na Maalim Seif

. Mchezo ushaisha kijana na ''Seif kapigwa tumboni/chini ya mkanda''
13319725_1800187683550379_1013107293094425438_n.jpg
Hiyo ni fashion tu siku hizi, pini huwekwa sehemu nyeti zaidi ya hapo, isikupe shida! Subiri kindumbwe ndumbwe
 
Maalim Seif yampasa kutumia fursa hii ya mwisho aliyopewa na Mwenyekiti wa CUF Mheshimiwa Prof.Ibrahim Lipumba, la sivyo atapoteza vyote.
Bahati mbaya sana Huyo ni mwenyekiti wa wa chungu kikubwa cha kuhifadhia MAJI ya kunywa vijijini kinaitwa nini vile? mtu nini vile? siyo mwenyekiti wa CUF!
 
BARUA YA MSAJILI ITABARIKI,KUMBUKA RUZUKU INATOLEWA NA SERIKALI.
Kwa Msajili huyu hili unalolisema linawezekana, ingawa kwa kufanya hivyo atakuwa ametangaza rasmi kuwa CUF ni mali binafsi ya CUF na hapo sio tu atakuwa amechochea moto mgogoro huu kama alivyofanya awali kwa kudai Lipumba ni mwenyekiti halali wa CUF, bali atakuwa amemwaga petroli kwenye huo moto aliouchochea. Matokeo ya hilo sijui itakuwaje!
 
Lipumba anawatia aibu wasomi!Sasa huyu ndiye anayesema anaweza kusaidia nchi kutoka kwenye umaskini wakati yeye mwenyewe ana NJAA!!
Huyu sio hata mtu wa kumwongelea!
Sio kweli, ukiwa Msomi unabaki kuwa msomi tatizo ukiwa MWANASIASA na Lipumba
kwa sasa amesimama kama mwanasiasa na si msomi.
 
Wanabodi wenzangu wakati hao wanafukuzana CUF , ukichangia vibaya nakufukuza hapa,

Mi naona kila mmoja ana agenda yake ya siri,
Maalimu seif ana agenda ya siri, kama hana agenda ya siri kwanini asikubali lipumba akaendelea mpaka uchaguzi ujao??

Pili na Lipumba naye haeleweki, kwani Kazi pekee ni uenyekiti kwanini asikae pembeni, maana ukiona kuna husda watasema unawatimulia vumbi wakati unacheza kwenye maji,

Ushauri wangu kwa Lipumba , najua anapitia hapa Mara kwa Mara , aachie ngazi , pia na maalimu seifu naye aachie ngazi ili CUF Iwe mikononi mwa vijana,

CUF inafuata historia ya NCCR mageuzi sasa,

Pia Mbowe asipende kuingilia ugomvi wa hawa watu , kwani hamuoni mwenyekiti wa CCM alivyo kimya?

Wenye uelewa Mdogo tunaweza tusielewe kwanini lipumba labda anafanya vile , labda anaona mbali, ila kwakuwa anaotuongoza ni watu wa akili fupi basi yeye yake iwe ndefu ajiuzuru kuendana na matakwa ya wenye akili fupi wengi,


Pia Seifu nawe umezeeka mipango yako ya kuwa rais uitenge Zanzibar kutoka bara imeshakwama kwahiyo ni vema uvumilie kama jumbe basi
 
Tumechona na hizi ngonjera leta maada zingine
 
KWA KUZINGATIA UKWELI KUWA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA TANZANIA NI MTEULE WA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA AMBAYE NI MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) TAIFA. - KUNA VIASHIRIA KUWA UTEKELEZAJI WA MAJUKU YAKE UNA USHAWISHI WA CCM – SEI SHARIF HAMAD

14519749_1293751223968344_8069283043392016265_n.jpg


Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la The Civic United Front CUF linatambua kuwa Chama cha The Civic United Front (CUF) kinaongozwa na Katiba yake halali, toleo la mwaka 2014, iliokubalika na kusajiliwa na ofisi yako, ambayo haijapata kuhoji uhalali wake.

Prof. Ibrahim Haruna Lipumba aliandika barua ya kujiuzulu nafasi ya Mwenyekiti wa CUF Taifa kuanzia tarehe 5/08/2015 ambayo ni siku aliyoandika barua hiyo na aliutangaza uamuzi wake huo mbele ya vyombo vya habari tarehe 6/8/2015.
Katika Barua yake ya kung’atuka wadhifa wa Mwenyekiti wa Taifa wa CUF ilisema ;
”Leo tarehe 5 Agosti 2015 najiuzulu rasmi nafasi ya Mwenyekiti wa Taifa wa CUF. Naendelea kuwa Mwanachama na kadi yangu nimeilipia mpaka 2020.”
Prof. Lipumba alitekeleza kujiuzulu kwake bila kusubiri kukubaliwa na Mkutano Mkuu wa Chama kwa mujibu wa Ibara 117(2) ya Katiba ya Chama. Prof. Lipumba alikua na mamlaka ya kuhakikisha kuwa Mkutano Mkuu unaitishwa ili kukubali kujiuzulu kwake lakini hakufanya hivyo.
Kama ulivyoeleza katika taarifa yako, Katiba ya CUF inatambua haki ya kujiuzulu uongozi lakini haizungumzii kutengua uamuzi wa kujiuzulu. Prof Lipumba asingeweza kutengua uamuzi wake wa kujiuzulu kwa sababu alishautekeleza. Na aliacha ofisi na majukumu ya Mwenyekiti wa Taifa wa CUF kwa mujibu wa Ibara ya 91 ya Katiba ya Chama kwa zaidi ya miezi kumi.

Kamati ya Uongozi ya awali iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Mhe. Twaha Taslima ambayo hukuhoji uhalali wake na uliitambua na hata kufanya kazi nayo ilipokuwa ikiwasiliana na wewe. Haiwezekani uone na utambue uhalali wa Baraza Kuu la Uongozi la Taifa kuunda Kamati ya Uongozi kwa kipindi cha Agosti 2015 hadi Agosti 2016 lakini usione uhalali wa kuundwa Kamati ya aina hiyo hiyo iliyoundwa tarehe 28 Agosti, 2016.

Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la The Civic United Front CUF limejiridhisha kuwa katika taarifa yako fupi umeweka hitimisho ambalo linatoa hukumu (judgment) mamlaka ambayo huna kisheria badala ya kushauri au kutoa taarifa kama ulivyoitaja.

Mwisho, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la The Civic United Front CUF haliukubali ushauri wako kwa sababu umevuka mipaka ya mamlaka yako uliyokabidhiwa na Sheria namba 5 ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992, imekiuka miongozo ya mhimili wa Mahakama ambayo imekwishatolewa juu ya mamlaka yako na unakiuka misingi ya katiba ambayo inamtaka kila mtu aliyepewa mamlaka katika nchi yetu azingatie sheria za nchi.

Chanzo : Seif Sharif Hamad
 

Attachments

  • ProPesa#11.jpg
    ProPesa#11.jpg
    74.8 KB · Views: 33
Tayari tunafahau na sio kuamini tu.
Hata kabla ya rejuvination ya ufake chairpersonship
 
Kuna vitu ukivitazama katika hili sakata utaona shida imeegemea wapi,hata kama huna taaluma ya maswala ya sheria.
Anza na kujiuzulu kwa bwana yuleeeee.Hili alilifanya kwa makusudi ya kuvuruga mwelekeo wa kiuchaguzi uliokuwa unaendelea na hatimae kukimbilia Rwanda ambako hatujui alifuata nini...maelezo zaidi baadae
Pili,kuvuruga kika cha CUF na kuingiza wahuni.
Tatu,kuvamia ofcn na kujenga kambi ofcn
Tukumbuke,hizi vurugu zote zinafanyika pasipo kupigiwa kelele na vyombo husika,kana kwamba hawajui nini kinatendeka.
Mbaya zaidi kuonekana kubebwa na hao wenye mamlaka juu yao

TANZANIA NCHI YA AJABU SANA.
 
Habari wakuu,bila kuwapotezea muda niende kwenye mada moja kwa moja.

Wote tunafahamu kinachoendelea ndani ya chama cha CUF na msimamo wa katibu Mkuu Seif sharifu Hamad dhidi ya mwenyekiti wake Prof Lipumba, Lakini hebu tujikumbushe hili la kihistoria.

CCM mwaka 2000 walifanya makubwa sana mpaka kufikia hata kuua wanachama wa CUF lakini CUF hawa walipotakiwa kukaa meza moja na CCM katibu Maalim Seif alikubali kukaa meza moja na CCM na muahafaka ukafikiwa.

Cha kusikitisha ni kwamba leo prof lipumba kwa kile wanachokiita alifanya makosa wanaposhauriwa wakae pamoja wafanye makubaliano tena kwa ushauri wa wajumbe wa mkutano mkuu maalim hayuko tayari napata kigugumizi kidogo katika hili inamaana lipumba ni kosa gani zaidi ya kuua alilowafanyia CUF?

Kubwa utagundua kwamba kama mgogoro huu ungeachwa kwa wenyewe CUF hadi sasa ungekuwa umekwisha, Tatizo ni kwa katibu mkuu Maalim Seif anashghurikia mgogoro huu kwa maelezo kutoka Office za CHADEMA pale Mtaa wa Ufipa.
 
Kwako Mtimbo, una ushahidi gani kuwa CUF wanapata maelekezo kutoka chadema? nafkr si muda mwafaka kwa CUF kukaa meza moja na Lipumba kupata suluhu. hivyo mtu anaharibu chama kwa maksusudi, amepandikizwa na ametumwa kwa kazi hiyo halafu unaweka mazingira ya kuongea kwa kupata suluhu, haingii akilini kwa mtu mwenye kutafakari.

Chuki zako dhidi ya CUF, chadema na UKAWA hazitokusaidia, nafikiri ni busara kwako mgomba ukauita mgomba na sio mpapai. Jifunze kuongea ukweli na kuitazama vyema na kwa jicho la uhalisia mgogoro huu uliopandikizwa ndani ya CUF na wasioitakia mema CUF.
 
Back
Top Bottom