Prof. Kabudi: Sheria mpya za madini hazitahusu migodi inayoendelea

Kwa msimamo Wa Huyu Kabudi inatosha kumuambia atupishe katika kiti alichokalia maana anaonyesha kuwa na msimamo sawa na ule Wa akina Tundu lissu ambao kwa namna Moja ama nyingine wanaelekea kuwa wamhongwa na acacia.

Rais chukua hatua kwa huyu mtu

Prof. Kabudi: Sheria mpya za madini hazitahusu migodi inayoendelea
Jiongeze : kwani hujui kuwa magufuli kaanzisha mikwara ili na yy kama wenzake, Kumbuka mkapa akula kwa njia zake akaja Kikwete akajidai kurekebisha mikataba kwa hati ya dharula akapiga zake akaondoka na sasa yupo Canada kuangalia jinsi ya kulinda masilahi yake tokea zamani, kwa sasa Magufuli na yy yupo anaandaa njia zake za kula hiyo pesa ndiyo hiyo kaleta waziri , wameshajua watanzania wengi hawajui chochote juu ya madini wameamua kuja na mbinu zao ili na wao waambilie chochote kabla ya 2020.
 
Siyo kwamba anamuunga mkono Lissu, Sheria huwa hairudi nyuma. Hiyo migodi wataendelea kuchukua dhahabu kwa mujibu wa mikataba ya kina Chenge. Kitakachofanyika ni kuwapigia magoti ili angalau waongeze asilimia ya mrahaba , na wanaweza kukataa na hatutawafanya chochote.
 
Ukimtumbua Kabudi basi ukamtumbue na Magufuli pia as it seems he shares the same thoughts.

Wewe hujiulizi kwa nini hawa BARRICK/ACACIA mpaka dakika hii wapo wanakwangua madini huko migodini kwa raha zao huku wakilindwa kwa mitutu ilhali Osoro kamuaminisha Magufuli na Umma kwamba wale jamaa ni fake na wanaoperate hapa illegally?
makinikia ni 5% ya madini lakini kule migodini kuna 95% bado inapigwa juu kwa juu yaani wale Wajanja wa CCM tokea kipindi hicho bado wanakula pesa bila kwele, Magufuli kaja na mbinu zake apate kula na yy hii ndiyo Tanzania zaidi ya uijuavyo
 
..ulichoeleza ni utaratibu ambao unatumika kwenye sheria nyingi.

..mimi nimejaribu kujazia tu ktk hoja yako kwamba yapo mazingira maalum ambapo sheria hushughulika na makosa/masuala yaliyotokea kabla sheria haijatungwa.

..kwa mfano sikubaliani na hoja yako kwamba tukiondoa kinga ya Maraisi hatuwezi kuwagusa Maraisi waliopita.

..Bunge la Tz lilipitisha sheria ya mafao ya viongozi wakuu wakati Waziri Mkuu ni Salim Ahmed Salim. Sheria hiyo ilielekeza kwamba hata Mawaziri Wakuu[kawawa, msuya] waliotumikia kabla ya Salim Salim nao watapata mafao ya viongozi wakuu.

..mfano huo unathibitisha hoja yangu kwamba wakati mwingine sheria inaweza kurudi nyuma. Mfano mwingine ni sheria ya Uhujumu uchumi ya wakati wa utawala wa Baba wa Taifa.

..Ila lazima NIKIRI kwamba watetezi wa haki za binaadamu wanapinga sheria zinazorudi nyuma haswa ktk masuala yanayohusu jinai.
Hata mimi nakubaliana na wewe kabisa. Serekali yetu 'ikiamua' (asante kwa kunipa hii vocabulary) inaweza. Si waliamua kuwaingiza mawaziri wakuu kwenye mafao yasiyowahusu!!!, si waliamua kukamata watu then kuwaundia sheria ya uhujumu uchumi!!!. Waliamua na imefanyika. Kwa kuamua, serekali zetu ziko mbele sana. Mchana kweupeeee, wanaamua kuisigina katiba na maisha yanaendelea. Kwahiyo tuko pamoja mkuu, mi nakukubali.
Lakini sasa tukikaa mezani tuanze kuangalia taratibu zinasemaje, hapo ndo mimi nasema mikataba ilikwisha sainiwa haiathiriwi na sheria mpya.
Tena ukimsikiliza Kabudi kwa 'sikio lako la tatu', Kabudi anasema "tumekwama". Kwa povu lile la Magufuli halafu 'tusiamuwe' kuwashirikisha kwenye mabadiliko ya sheria........ nakuhakikishia tumekwama. Kwani na wewe si unajua mbabe akikwama huwa anarudi kuangalia sheria zinasemaje!!!!.
 
Mikataba ya uwekezeaji kwenye madini ccm waliipitisha kwa wino wa damu kwa hiyo si rahisi kufutika hadi kizazi kichafu cha chama hiki kitakapopita
Wino wa damu you mean wale watu alikuwa anasemaje lisu wamefukiwa. Damu haituachi tuombee hao wadhalimu walipishwe na vizazi vyao
 
Hadi Leo watanzania tukiambiwa ukweli uwa tunaona msemaji ni msaliti.

Lisu alitoa mfano Venezuela jinsi ya kujitoa kwenye lindi la mikataba ya kimangungo

Leo hii prof anasema kirahisi kua mikataba ya zamani uwezi gusa hapa pana mashaka mno pamoja Acacia kutosajiliwa brela lakini bado hatuna hapo?

Wazungu huko hawana mdhaa kwenye kodi hadi messi, ronaldo wanaitwa kizimbani sisi tunawaita ikulu.

Hatari sana kwa vizazi vijavyo tuache kujiangilia wenyewe waangalie na watoto wa wajukuu wako nao wataishi hapa hapa
 
Ata akitumbuliwa hana chochote cha kupoteza atarudi idarani lakini pia mwenzako ni LEARNED BROTHER kitambo kwa siku anaweza kuingiza 20k usd per day kwa kusuka MoU. Maskini tunashida sana.
Pole dada! Wanamchokonoa dingi
 
Mimi nampongeza Professor,kaitendea haki taaluma yake. Kama kwa mtazamo wa kisheria tungeweza kuingia kwenye matatizo,basi kwa kuepuka kama nchi ikaonekana inafaa At First,tuanze upya,kwa wale waliotayari na makubaliano,waombwe angalau amendments ziwaguse katika ile tuiitayo Win-Win situation,tukiwaendea kidoplomasia,naamini watatuelewa. Sheria iko hivyo. Nampongeza Mh Waziri wa Sheria na Katiba kwa kufuata professionalism ili kwanza nchi inufaike na rasilimali zake lakini pia kuiondolea kuingia kwenye mgogoro wa kidiplomasia ya kiuchumi.

Kuna mchangiaji kawaomba Mods waifute thread hii kwa madai kuwa ni ya chuki. Nafikiri kweli kichwa cha habari kina udhi,japo maudhui yaliyopo ndani hayaudhi.
mpongeze pia na tundu lisu kwa kutoa tahadhari mapema ambayo kabudi ameitumia
 
Kusema kweli mimi sikuwahi kusoma popote zaidi ya kujaza blanks tu na picha
ha ha ha... hata mimi nilijaza blanks na picha tu. hapo ndo tulipokosea na kuwapa loophole ya kufanya wanavyotaka. Kuna mtu alinionesha kipengele hicho nilichoka kabisa. kama isingekuwa hivyo, kesi hiyo wangeshinda asbuhi kabisa. kwa grounds kwamba sharia hutumika pale ilipotungwa naa kutowagusa wa nyuma.
 
Maajabu ya Tanzania,sheria ya bodi ya mikopo imetungwa mwaka jana lkn inawahusu waliohitimu vyuo vikuu kuanzia mwaka 1994 na wanakatwa asilimia 15 badala ya 8 waliyosaini.Hii ya madini yenyewe inaanza kuanzia ilipotungwa kwenda mbele hairudi nyuma na haitayahusu makampuni ambayo yanaendelea na uchimbaji!Hivi inaingia akilini kweli?wanasheria humu jukwaani saidieni kunielewesha hapa

Yale yale RC na DC na wabunge sifa nikujua kusoma na kuandika uhakiki hautawsusu alafu wanaojua kusoma na kuandika ndo wanoenda kumfokea na kumkejeri mtu mwenye degree Tanzania Nchi ya ovyo sana
 
Wachangiaji
Uharaka wa nini kama sio makinikia. Kweli lisu anatetea majizi
Wachangiaji hapo juu wote akili zenu za kushikiwa, mpaka kuamua kucomment inamaana unauhakika na ulicho kisoma tatizo lenu mmekurupuka nawashauri mngeomba kwanza awapatie hiyo crip ya prof. Kabudi kutoka kwayo ndo comments zianze otherwise nonsense.
 
Yale yale ya Uhakiki wa vyeti hautawausu wabunge na mawaziri pamoja na RC na DC hii nchi inaviongozi wa ovyo hawajawai kutokea
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom