kinepi_nepi
JF-Expert Member
- Aug 16, 2007
- 869
- 236
Excellent tuko pamoja. Ila hujaweza kuwafanya lolote, tufanyeje ndugu? tututukane? basi, tuwavute baadhi yao waje chadema halafu tukiingia ikulu tuwashtaki? is not this the ultimate goal?
Mkuu,
Kumbuka CCM sio kwamba ni wajinga, wanajua mchezo na wanajua wakipoteza stage nini kitatokea. Ndio maana wanatumia mbinu zote kubakia madarakani. Kwa sasa wanatumia mbinu za hayati mubutu kupandikiza watu wao kila mahala. Ni kweli kumtukana mtu haisadii ila nakubali kuwamaliza kwa hoja. Kama upande wa pili utajenga hoja zenye mashiko na kuwa na mkazo siku zote, kuelimisha jamii kwa nguvu watatoka tu madarakani.
Kumbuka vyama vya kikomunisti vilijijenga sana kwa kutumia hofu kwa watu wake. Hivyo kuna kizazi bado kina hofu kuu. Na kwa upande mwingine ukumbuke ukimfungia paka chumbani ukaanza kupiga viboko akikosa pakutokea anakua chui. Wananchi wamefungiwa kwa muda mrefu huku wakichapwa sasa wamegeuka kuwa chui. Hapa wa kulaumiwa ni CCM wamezalisha kizazi kisicho amini utawala wa sasa wala haki mbele ya sheria. Kwa mtaji wa maisha haya no umeme, no maji, no barabara, no hospitali no haki no usawa, no sheria. usitegemee lugha safi.
Ukitembea mitaani kila mtu analaani serikali. umeme ukikatika kila mtu anatukana serikali. Juzi nilikuwa na waziri wa serikali ya CCM, umeme ukakatika akatukana serikali, nikamwambia kwani na wewe si sehemu ya serikali akasema huyu ngeleja bwana sijui ana nini. Kwa hiyo wengi tu wapo humo ndani ila nao wanaona moto.
Nchi inawaka moto, hakuna amani tena, hakuna utulivu. Ni bomu linasubiria kulipuka, tunaweza hata tusibalishane tena madaraka kwa amani kama busara hazitatumika mapema kurekebisha hali mbaya ya maisha. Kila mtu yuko tayari kuingia mtaani. Ukiona watu wanaandika lugha kali sana ujue mambo sio sawa. Wenye akili husoma ishara za nyakati, na wengine hupuuza. Mambo ya Misri, Libya, tunisia ni matokeo ya Viongozi kupuuza kuamini kwamba wao ni smart kuliko viongozi wote duniani. hili kosa linafanywa na serikali ya CCM. wanaamini wanaweza kuwadanganya wananchi wao milele.
Ukimwibia mtu usimletee mzaha tena. Ukimlia mtu chakula chake ukamwacha na njaa usimletee masihara. Ukimuulia mtu mwanae usimwone mjinga anaweza kufanya vituko vingi.