mayenga
JF-Expert Member
- Sep 6, 2009
- 4,118
- 1,973
Ndege zote zinazonunuliwa na PW ni mpya- brand new!
Amini usiamini PW wana routes nyingi na hakuna ndege inayokuwa on ground kusubiria itakayopata hitilafu.
Kila ndege mpya inayokuja inapangiwa route yake, na si rahisi kuvunja route ya kwenye ratiba.
Hii ndiyo shida ya kuwa na ukame wa mashirika ya ndege nchini, lau yangekuwepo PW wangekodi ingine ikapiga route husika.
Nawasifu sana PW so far kwa kuwa National Carrier, na wanaiepusha nchi na aibu ya mwaka.
Labda niwaulize wote mnaolaumu na kubeza kazi iliyotukuka ya PW kuwa ni kipi bora, kurusha ndege yenye snag, au kuipeleka kwanza hangar ikarekebishwe hata kama matengenezo yatakula masaa 6? Naomba jibu.
Mnazifahamu vizuri ajali za ndege, na jinsi zisivyo na Mswalie Mtume katika kuchinja abiria, halafu leo mnambeza rubani anayetoa taarifa kuwa ndege ina snag! kwa watu waliostaarabika walitakiwa watoe compliment kwa PW kwa kuzingatia kanuni za Usalama wa ndege na wasafiri.
Nawapongeza sana PW kwa umakini wenu, ndiyo maana hadi leo hamjakumbwa na fatal au catastrophi accident. Huu ni uzingatiaji wa juu sana wa kanuni za usalama.
Ki-aviation inasemekana kuwa 85% ya ajali za ndege husababishwa kutozingatia kanuni za usalama. Masuala kama mchafuko wa hali ya hewa na mis-communication yanachangia percent ndogo iliyobakia.
Ndege katika hali ya kawaida ina uwezo wa juu sana wa kujiepushia ajali yenyewe inapokuwa angani. Ndege inaweza kudevelop tatizo kubwa ikiwa angani, lakini ikatumia spare-capacity yake kukata mawingu hadi mwisho wa route yake, then ikishatua haitatoa go-ahead kwa rubani kuiondoa tena hadi irekebishwe.
Sasa system za safety zenye akili namna hiyo tunazibeza, tunataka nini?
Ile kawaida yetu ya kushinda tunalaumu tusiiingize kwenye masuala ya technical, na hasa maeneo nyeti kama usafiri wa anga.
Angani hakuna parking au stendi meen.
Ahsante Mkuu!!