DPN
Member
- Sep 28, 2020
- 31
- 68
KWA POSTMASTER GENERAL, TPC.
Tarehe 13/3/2020 nilituma mzigo kwa njia ya posta kutoka Magu, MWANZA kwenda Mbinga, RUVUMA; ambapo nilihudumiwa na REGINA SEDEDE ambaye alinipa Invoice Namba M-7203-03200066751 ya shilingi 11,900/= (Elfu kumi na moja na mia tisa tu) ambazo nililipa taslimu na mzigo wangu ukapewa Register namba RD037111148TZ tayari kwa kusafirishwa.
Mzigo huo ulikuwa na vitu vyenye thamani ya shilingi 140,000/=; ukijumlisha na gharama kusafirishia mzigo huo nilizolipa posta shilingi 11,900/=, thamani ya mzigo huo inafikia shilingi 151,900/=
Nilimtumia namba ya Register niliyopewa posta mtu niliyemtumia mzigo (kama nilivyoshauriwa na mfanyakazi aliyenihudumia posta); na nilianza kuwasiliana na niliyemtumia mzigo huo wiki moja baada ya kutuma mzigo, ili afuatilie mzigo huo Posta Mbinga, lakini mpaka leo mzigo huo haujamfikia.
Baada ya kufuatilia kwa Posta Masta Magu, jibu alilonipa ni kuwa, tracking system inaonyesha mzigo ulipokelewa Posta Dar-es-salaam kutoka Posta Mwanza tangu tarehe 17/3/2020; na siku hiyohiyo 17/3/2020 mzigo ukatumwa kwenda Posta Songea kwa gari la posta; lakini system hiyo haionyeshi chochote baada ya mzigo kutoka posta Dar-es-Salaam
Nimeendelea kufuatilia mzigo huo Posta Magu, na nimekuwa nikishauriwa kuwasiliana na niliyemtumia mzigo; lakini naye jibu lake kutoka Posta Mbinga limekuwa ni hilohilo kwamba mzigo haujafika Posta Mbinga.
Leo ni zaidi ya miezi tisa tangu nitume mzigo huo (tarehe 13/3/2020) lakini mpaka leo haujanfikia niliyemtumia.
Nimeshaandika barua na kupiga simu mara nyingi kwa Posta Masta Magu na Mwanza nikifuatilia mzigo huo, lakini hakuna jibu la maana ninalopewa ambalo linaleta ufumbuzi wa hicho kilichotokea; wanachofanya mabosi hao ni kupotezea mpaka nichoke kufuatilia hatimae ninyamaze, maisha yaendelee wakati nimepoteza
Hiyo siyo sawa, wala siyo haki, maana hamko hapo kwa ajili ya kunyang'anya mali za watu ndani ya shirika hilo la umma huku mkilipwa mishahara; mnasababisha madhila kwa watu na hata kuharibu maisha yao!!
POSTMASTER GENERAL, nina kila sababu ya kuamini kwamba mzigo huo umeibiwa na watumishi wa shirika unaloliongoza; na kama ndivyo, nina kila sababu ya kuamini kwamba mizigo mingi ya wateja inaibwa na watumishi wako wasiokuwa waaminifu, na wewe umeshindwa kukomesha tabia hiyo mbaya ambayo inalichafua shirika.
Kwa vile umeshindwa kufikisha mzigo huo kwa niliyemtumia, basi fanya utaratibu upasao ili unifidie mzigo wangu; niko tayari kutoa uthibitisho wa madai yangu ili unifidie.
Asante; wako katika ujenzi wa Taifa.
DPN
Tarehe 13/3/2020 nilituma mzigo kwa njia ya posta kutoka Magu, MWANZA kwenda Mbinga, RUVUMA; ambapo nilihudumiwa na REGINA SEDEDE ambaye alinipa Invoice Namba M-7203-03200066751 ya shilingi 11,900/= (Elfu kumi na moja na mia tisa tu) ambazo nililipa taslimu na mzigo wangu ukapewa Register namba RD037111148TZ tayari kwa kusafirishwa.
Mzigo huo ulikuwa na vitu vyenye thamani ya shilingi 140,000/=; ukijumlisha na gharama kusafirishia mzigo huo nilizolipa posta shilingi 11,900/=, thamani ya mzigo huo inafikia shilingi 151,900/=
Nilimtumia namba ya Register niliyopewa posta mtu niliyemtumia mzigo (kama nilivyoshauriwa na mfanyakazi aliyenihudumia posta); na nilianza kuwasiliana na niliyemtumia mzigo huo wiki moja baada ya kutuma mzigo, ili afuatilie mzigo huo Posta Mbinga, lakini mpaka leo mzigo huo haujamfikia.
Baada ya kufuatilia kwa Posta Masta Magu, jibu alilonipa ni kuwa, tracking system inaonyesha mzigo ulipokelewa Posta Dar-es-salaam kutoka Posta Mwanza tangu tarehe 17/3/2020; na siku hiyohiyo 17/3/2020 mzigo ukatumwa kwenda Posta Songea kwa gari la posta; lakini system hiyo haionyeshi chochote baada ya mzigo kutoka posta Dar-es-Salaam
Nimeendelea kufuatilia mzigo huo Posta Magu, na nimekuwa nikishauriwa kuwasiliana na niliyemtumia mzigo; lakini naye jibu lake kutoka Posta Mbinga limekuwa ni hilohilo kwamba mzigo haujafika Posta Mbinga.
Leo ni zaidi ya miezi tisa tangu nitume mzigo huo (tarehe 13/3/2020) lakini mpaka leo haujanfikia niliyemtumia.
Nimeshaandika barua na kupiga simu mara nyingi kwa Posta Masta Magu na Mwanza nikifuatilia mzigo huo, lakini hakuna jibu la maana ninalopewa ambalo linaleta ufumbuzi wa hicho kilichotokea; wanachofanya mabosi hao ni kupotezea mpaka nichoke kufuatilia hatimae ninyamaze, maisha yaendelee wakati nimepoteza
Hiyo siyo sawa, wala siyo haki, maana hamko hapo kwa ajili ya kunyang'anya mali za watu ndani ya shirika hilo la umma huku mkilipwa mishahara; mnasababisha madhila kwa watu na hata kuharibu maisha yao!!
POSTMASTER GENERAL, nina kila sababu ya kuamini kwamba mzigo huo umeibiwa na watumishi wa shirika unaloliongoza; na kama ndivyo, nina kila sababu ya kuamini kwamba mizigo mingi ya wateja inaibwa na watumishi wako wasiokuwa waaminifu, na wewe umeshindwa kukomesha tabia hiyo mbaya ambayo inalichafua shirika.
Kwa vile umeshindwa kufikisha mzigo huo kwa niliyemtumia, basi fanya utaratibu upasao ili unifidie mzigo wangu; niko tayari kutoa uthibitisho wa madai yangu ili unifidie.
Asante; wako katika ujenzi wa Taifa.
DPN