Posta yafanya mazungumzo ya kibiashara na DSTV

Posta yafanya mazungumzo ya kibiashara na DSTV

PendoLyimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2014
Posts
1,059
Reaction score
1,133
Kaimu Postamasta Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania Bwana Macrice Daniel Mbodo amekutana na kufanya mazungumzo ya kibishara na Maafisa Biashara wa kampuni ya MultiChoice Tanzania maarufu kama DStv.

Mazungunzo hayo yamefanyika leo tarehe 27 Oktoba, 2021 kwenye ukumbi wa Bodi uliopo gorofa ya 12 katika Makao Makuu ya Posta, jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo ulilenga kujadili namna ambavyo taasisi hizi mbili zitakavyowahudumia wananchi wengi zaidi na kwa haraka kupitia mtandao mpana ulioenea nchi nzima wa Shirika la Posta Tanzania.

Ujumbe kutoka Kampuni ya Multichoice Tanzania uliongozwa na Meneja Kitengo cha Bishara Bi. Enna Kiondo, Mkuu wa Kitengo cha Biashara Bw. Eriq Mfinanga pamoja na Afisa Biashara wa Kampuni hiyo Bw. Matoke matoke

Aidha, mkutano huo ulihudhuriwa na Mameneja Wakuu wa Shirika la Posta nchini pamoja na viongozi wengine waandamizi wa Shirika la Posta.

Imetolewa na,
Kitengo cha Mawasiliano,
Shirika la Posta Tanzania.
27 Oktoba, 2021.
 
Kwa hiyo ndiyo kusema DSTV Wamechoka kuanika visimbuzi vyao barabarani baada ya kuona maji yanazidi unga, wanataka posta iwasaidie.!!!! Kusambaza siyo?
 
Posta wanataka kuwasaidia Dstv kuuza Ving'amuzi vyao sio

Sent using Jamii Forums mobile app
Hawa Posta sio Wabunifu kweli acha wafu wazike wafu-DSTV kutokana na VOD pamoja na IPTV ,pamoja na Azam na Startimes wapo ICU kinachowabeba ni Mpira...ila uko mbeleni watapotea.

Posta kweli wanaweza zalisha faida nyingi sana kwa mwaka Tatizo wanatumia njia za 1947!!.Ningetamani kuwashauri ili wafike pale panapotakiwa.

Kutokana na ICT kudominate karibia kila kitu kuna ajira za aina fulani azina 10 yrs kufutika Duniani pia Makampuni na Huduma tena nyingi tu!Je what is POSTA master plan for 3 years starting 2022? mfano with ATC ,POSTA can make $ 100M kwa Mwezi.

With Telecom Companies pia anaweza ingiza zaidi ya $5M kwa mwezi. Tuna vyama vya msingi vya mazao,Hivi Vinaweza muingizia POSTA zaidi ya $10M kwa mwezi .na bado ajafanya upande wa Zanzibar na nchi jirani....POSTA wanaweza make $250 Millions kwa mwezi.

In Today World Business Modeling that include Technology evolvement is Very important to any Companies to Survive
 
Posta wana mambo mengi sana. Hawajamaliza hili wanadakia hili.
Ule mpango wa Ndugulile umeishia wapi? One stop centre. Taasisi zote za umma zihamie Posta ha ha ha ha ha
yaani hapo ndo wanapochemsha! alafu hizo huduma za One stop Center-Ni Daily Consumed au just kuokoteza okoteza 😁
 
Back
Top Bottom