Post Graduate Diploma v/s Bachelor Degree

Post Graduate Diploma v/s Bachelor Degree

windows8.1

Member
Joined
Apr 10, 2014
Posts
15
Reaction score
0
Za muda tena wadau wa jukwaa hili!

Naomba kujua je! mtu mwenye post graduate diploma iliyo tofauti na digrii yake ya kwanza anaweza kuwa na ufanisi ulio sawa katika utendaji na mtu mwenye bachelor degree ya kozi husika? Kalibuni sana.
 
Kweli wengi tunataka ufafanuzi,ni nani mwenye elimu kubwa kati ya hawa!
 
Huwezi kufananisha mlimao na mchungwa japo vyafanana, huwezi kufafanisha kadiploma na Degree, mwenye degree ana akili sana tofauti na mwenye kadiploma ka manati even though kanaweza kupachikwa jina la Advanced diploma baada ya mtu kuongezea kaelimu but ukweli utasimama daima.
 
Huwezi kufananisha mlimao na mchungwa japo vyafanana, huwezi kufafanisha kadiploma na Degree, mwenye degree ana akili sana tofauti na mwenye kadiploma ka manati even though kanaweza kupachikwa jina la Advanced diploma baada ya mtu kuongezea kaelimu but ukweli utasimama daima.
Nani kakudanganya kwamba adv.dip ndo post?hivi hua mnasomaga mada kabla yakujibu?nani umemuona anadiploma akaenda kusoma post bila kua na Bsc?yani hiki kizazi Mungu atuokoe tu maana kama hata wewe unadegree basi tuna tatizo kubwa.samahani lakini inatia mashaka
 
Jamani kwa uelewa wangu mtu mwenye post graduate diploma ni mtu mwenye degree tayari ila alikuwa ana ufaulu mdogo degree wa kuweza kuendelea na masters so ina mbidi asome post graduate diploma kubost qualification zake ili aendelee kusoma master....asante
 
Za muda tena wadau wa jukwaa hili! naomba kujua; je,mtu mwenye post graduate diploma iliyo tofauti na digrii yake ya kwanza anaweza kuwa na ufanisi ulio sawa katika utendaji na mtu mwenye bachelor degree ya kozi husika? Kalibuni sana.

katika uhalisia ndugu yangu hawa watu hawawezi kua sawa ingawa theoretically wanafit, maana post graduate diploma ni masoma ya ziada ya ujuzi(kama ninavojua),kwamfano, mtu flani alisoma public relations digrii lakini akaona aongeze ujuzi juu ya hapo akaenda kusoma post. graduate ya international diplomacy. mara nyingi post graduate ni taaluma zisizo na mifumo yaani utakuta Bsc.wildlife management lakini hakuna Bsc ya bush meat management. kwahyo mtu anatafuta ujuzi kwa kusoma course ili accomplish mission anayotaka.nadhani nitakua nimejaribu kukudadavulia japo kidogo maana wataalamu wengine watakuja naaimani hyo.lakini swala la ufanisi ni swala moja na swala la elimu niswala lingine maana unaona jitu lina degree lakini utendaji mbovu tena nanga wakutupa mpka inakupa mashaka juu ya elimu yake.nimawazo yangu
 
Huenda watu hapo juu (ukiondoa mleta mada) hawaielewi Postgraduate Diploma, na nimesema hivyo kutokana na post zilizowekwa hapo juu. Ili mtu usome Postgraduate Diploma, lazima uwe graduate. Kama watu hapo juu mngekuwa na uelewa wa matumizi ya prefix na suffix, bila shaka hata neno 'post' lingetosha kuvuta attention kwamba 'postgraduate' ni nini!

Tukirudi kwenye swali, mleta mada anahoji 'utendaji', na sio 'qualification'. Kwa kweli ili upate jibu sahihi, inabidi ufanywe utafiti (research), vinginevyo labda upokee majibu ya mtu mmoja mmoja tu ambayo katika research ni sawa na dodoso (questionnaire) moja moja tu. Kwangu mimi, tofauti ya ufanisi wa mtu katika kazi kati ya graduand wa fani husika na postgraduand wa fani husika lakini aliyetokea katika fani tofauti, inaweza ikawepo au isiwepo kutegemea na hiyo fani. Mfano mzuri ni Uhandisi (Engineering), kwa chuo kilicho makini hakiwezi kupokea mtu mwenye degree au advance diploma ya fani tofauti na Engineering asome Postgraduate Diploma ya Engineering kwani wanajua utendaji wa huyu wa postgraduate utakuwa low ukilinganisha na mtu aliyetoka nayo taratibu kuanzia mwaka wa kwanza hadi wa nne/tatu. The same to field za Health. Lakini fani za Biashara, utendaji na ufanisi unaweza usitofautiane kabisa hususan katika management, ila katika mambo ya kiufundi kama Audit, huenda mtu mwenye degree akawa mzuri zaidi.

Kwa ufupi utendaji wa kifanisi unategemea fani yenyewe
 
Huwezi kufananisha mlimao na mchungwa japo vyafanana, huwezi kufafanisha kadiploma na Degree, mwenye degree ana akili sana tofauti na mwenye kadiploma ka manati even though kanaweza kupachikwa jina la Advanced diploma baada ya mtu kuongezea kaelimu but ukweli utasimama daima.
Shardcole acha kupotosha watu jifunze kuuliza kabla ujapost kitu kishabiki.
Mtu anaesoma Post-graduate diploma maana yake anayo degree ya kitu kingine mfano Bsc in Agriculture so anahitaji asomee education hivyo anajiunga na kusomea Post-graduate diploma ya elimu na anasoma mwaka mmoja maana yake atasoma course za elimu pekee na anakuwa vizuri tena sana tu.
Advanced diploma is equivalent to Degree hamna tofauti yoyote, na mtu mwenye Advanced diploma akitaka kuendelea anasoma masters kama kawaida.
 
Kwa hiyo form six sawa na Degree ya kwanza??? kuweni makini
 
Kwa nini utumie neno "equivalent" yaani hesabu za makadilio ndio zinazo tufanya tukadilie kila kitu sasa 2.6 ni sawa na 3. Kwa wenzangu graduates wa degree na kuendeleaukipata GPA ya 2.8 sio sawa na 3 nadhani katika elimu hakuna makaribishio kwa nini wasiseme sawa na 2 tu so haya ni maneno yetu tuu, katika elimu hakuna ukaribishiaji bwana wa mambo.
 
Post graduate itabaki ni other course study attended after first degree graduation that's why is post graduate and not pre graduate diploma thus with post graduate you can do master degree .

Nb post graduate not equal to master degree
 
Jamani kwa uelewa wangu mtu mwenye post graduate diploma ni mtu mwenye degree tayari ila alikuwa ana ufaulu mdogo degree wa kuweza kuendelea na masters so ina mbidi asome post graduate diploma kubost qualification zake ili aendelee kusoma master....asante

Siyo lazima Mtu kuwa Na ufaulu mdogo Ndo usome Post Graduate Diploma, Post Graduate Diploma mara nyingi inasomwA km course ya ujuzi maalum! Mfano, Una shahada ya sheria,unaamua kusoma Post Graduate Diploma in Criminology,Hapo unakuwa umeongeza ujuzi wa sheria Za makosa ya jinai,So ujuzi Ama utaalam maalum!™
 
Kalibuni tena wadau katika mdahalo huu ingawa nimegundua baadhi hawajui tofauti ya Advanced Diploma & Post graduate Diploma.Kwa ufupi huwezi soma Post graduate diploma kama huna digrii ya kwanza tofauti na Advanced diploma.Nihayo tu.kalibuni!!
 
Siyo lazima Mtu kuwa Na ufaulu mdogo Ndo usome Post Graduate Diploma, Post Graduate Diploma mara nyingi inasomwA km course ya ujuzi maalum! Mfano, Una shahada ya sheria,unaamua kusoma Post Graduate Diploma in Criminology,Hapo unakuwa umeongeza ujuzi wa sheria Za makosa ya jinai,So ujuzi Ama utaalam maalum!™

Umeongea point sana.mfano kama mtu amesomea LLB akaajiriwa TRA inambidi asome postgraduate ya TAXATION ili imsaidie kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.au umesomea LLB ukaajiriwa JUBILEE INSURANCE kama mwanasheria wao hivyo ili uwe competent unalazimika kupata general knowledge ya mambo ya insurance hivyo unalazimika kusomea postgraduate ya insurance.kwahiyo sio lazima mtu awe na gpa ndogo sometime.
 
Back
Top Bottom