Posho za wabunge

regam

JF-Expert Member
Jan 4, 2011
269
51
Mshahara kwa mwezi tshs 2,300,000/=
2.Mafuta ya gari kwa mwezi 2,000,000/=i.e ltr 1000 kwa mwezi
3.Posho ya ubunge kwa mwezi 1,000,000/=
4.Posho ya kukaa bungeni kwa siku 80,000/=
5.Posho ya kuendesha ofisi kwa mwezi 700,000/=
6.Simu ya mkononi kwa mwezi 500,000/=
Jumla ya mapato hayo ni7,200,000/=ukiachilia mbali posho za vikao vya kamati mbali mbali na safari za nje. bado wameona pato hilo kwa mwezi halitoshi wamejiongezea posho ya vikao mpaka 200,000/= kwa kisingizio kuwa maisha ni magumu. madaktari walipogoma posho imeongezwa kufikia 25,000/=. waalimu wanalalamika hakuna anayejali. Hii imekaaje? na nini kifanyike?.
Tafadhali changieni bila ghadhabu. Nawasilisha.
 
Huu niwakati wavitendo watz tumekua shamba labibi kwawageni lakini sasa mpaka wenyewe kwawenyewe tunanyonyana kama kupe tena live, how come mtu anapata mshahara wamtu wa mwezi kwasiku halafu anasema maisha magumu nasisis tusemeje? Politics now is a bizz na inalipa vibaya
 
Kinachonipa shida ni kuwa pesa yote hiyo inakwenda kwa kundi la watu wachache wasiokuwa na tija kwa ukuaji na ustawi wa uchumi wa Taifa hili.
Matokeo yake watu wenye taaluma ambazo zinge saidia kuleta maendeleo kwa makusudi kabisa wamekatishwa tamaa na baadhi yao kuamua nao kujiingiza kwenye siasa kwa lengo la kupata kipato kizuri.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom