Safari_ni_Safari
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 23,268
- 17,099
Naona hesabu ni janga la kitaifa!
Ongezeko hapa ni shilingi 130,000 (yaani 200,000 ukitoa 70,000). Ongezeko hili ni asilimia 186 (i.e. 185.7 = 130,000x100/70,000). Hiyo 154% sijui mwandishi anaipataje!
Kama lengo ni kusema kiwango kipya ni mara ngapi ya kiwango cha awali....basi angeweza kusema "kiwango kipya cha posho ni zaidi ya mara mbili (au karibia mara tatu) ya kiwango cha awali" na kama ni katika muktadha rasmi sana au ule wa kitaaluma zaidi angesema "kiwango kipya cha posho ni mara 2.86 ya kiwango cha awali"
Kwa kuwa ni swala la kisheria na ili sheria ibadilishwe lazima wabunge wengi wawa unge mkono itu ambacho kimekuwa kigumu kiasi kwamba hata ndani ya CDM kuna wanafiki wanazitaka sana hizo posho...Mfano Shibuda yeye alisema anaomba iwe 500,000 kwa siku...lakini Zitto yeye alisema zitakuwa zinatumia kwenyemfuko wa jimbo lake kama sikosei...hivyo wengi wanaiona hii ndiyo njia sahihi kwa sasa kuzitumia kwenye jimbo au wewe unapendekeza nini.....?umenena vyema mkuu lakini waliziacha hizo posho na wana mikakati gani yakuigomea posho pamoja na kuwa zinaingia benki moja kwa moja
Na kwa nini amsitaje? Kwa mujibu wa taarifa na hoja hii anayoitetea Zitto, ni yeye tu na Januari Magamba ambao wanapinga posho za wabunge na za vikao.Kama Zitto angekaa na wabunge wenzake wa CHADEMA na kujadiliana nao kabla ya ku-issue hii statement kingeharibika nini? And what it the point ya ku-mtaja (kumpongeza January Makamba) kwenye hili?
Pole mkuu sikuwa na maana ya kukudhalilisha...kitendo cha wewe kuona tatizo katika hiyo habari peke yake kinaniambia unajua hesabu!Hilo lako ndio janga 2.86 ndiyo 286% yangu......nitake radhi ndugu
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe
Alipoulizwa kama amechukua posho hiyo ya Sh200,000 alisema hajafanya hivyo kwa sababu hazifuatilii.
"Sijui hata kama zimeanza kulipwa au la kwa sababu huwa sizifuatilii na haka kama suala la posho hilo zilijadiliwa wakati wa vikao vya mwanzo mimi sikuwepo kwa sababu tulikuwa kwenye kesi yetu Arusha na bungeni tulikuja mwishoni wakati wa Muswada wa Katiba," alisema Mbowe..
Hapo kwenye red umepotosha nilichokisema kwenye post yangu..lakini nakusamehe bure tu.Nimesimama kwenye kauli ya mtoa habari na si vinginevyo....nanukuu "Zimeongezeka kutoka Sh70,000 mpaka 200,000, wameanza kulipwa Bunge lililopita hili ni ongezeko la karibu mara tatu, yaani asilimia 154,"......2.86(286%) ndiyo mara tatu yenyewe approximately......huwezi kusema 130,000 ndio ongezeko mara tatu......hakuna janga na mimi ni mtaalamu wa hesabu
Hata hivyo hoja yangu ni kuwa huwezi kusema kuna ongezeko la 286% (wala 154%)! Ongezeko ni shilingi 130,000 na hiyo ni sawa na asilimia 186 (na sio asilimia 286 wala 154) ya shilingi 70,000.
Zitto's ostentatious nature is a reason behind his low popularity among his Chadema fellow high-profile figures. The guy is too bigheaded and think that he can stand on his own even in sober matters that seem to otherwise disturb Magamba's interests. His move to pressure on the Government to scratch sitting allowance was conspicuously plausible but only lacked his party's blessings before being mooted in the assembly. Unfortunately Zitto ignored the importance of his party's ratification of the issue and decided to take the task by his own, apparently for the sake of winning public approval. His plans have then proved failure and in the end sitting allowances have been increased.
wapinge mara ngapi? soma hotuba ya kambi rasmi ya upinzani (ya waziri kivuli wa fedha) then ndio urudi hapa jfNilitegemea wabunge wa Magwanda wangepinga ongezeko hili la kutisha lakini kimya sioni tofauti kati ya magwanda na Magamba wote sawa.
Kwa kuwa ni swala la kisheria na ili sheria ibadilishwe lazima wabunge wengi wawa unge mkono itu ambacho kimekuwa kigumu kiasi kwamba hata ndani ya CDM kuna wanafiki wanazitaka sana hizo posho...Mfano Shibuda yeye alisema anaomba iwe 500,000 kwa siku...lakini Zitto yeye alisema zitakuwa zinatumia kwenyemfuko wa jimbo lake kama sikosei...hivyo wengi wanaiona hii ndiyo njia sahihi kwa sasa kuzitumia kwenye jimbo au wewe unapendekeza nini.....?
Nimesimama kwenye kauli ya mtoa habari na si vinginevyo....nanukuu "Zimeongezeka kutoka Sh70,000 mpaka 200,000, wameanza kulipwa Bunge lililopita hili ni ongezeko la karibu mara tatu, yaani asilimia 154,"......2.86(286%) ndiyo mara tatu yenyewe approximately......huwezi kusema 130,000 ndio ongezeko mara tatu......hakuna janga na mimi ni mtaalamu wa hesabu
kwenye hili hakuna chama tawala au cha upinzani........wote wanashabikia kulipora taifa..................huku hakuna vigezo vya kulinganisha mapato ya wabunge na watendaji wengine serikalini..................................kama ni kubana mkanda si tubane wote lakini wabunge hawataki kwa sababu bunge lao wamelitukuza mithali ya Mwenyezi Mungu pale walipoliita bunge tukufu na wao ni waheshimiwa na sisi wengine hatuna hiyo taswira......ni walalahoi ila muhimu sana katika kuhalalisha ulaji wao kila baada ya miaka mitano