Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Salaam,
Posho za Vikao zinapingwa kwa sababu zinakataa mantiki- Mbunge kutokana na nafasi yake ni wazi atahudhuria vikao mbalimbali vinavyoendana na majukumu yake hivyo kumlipa posho kwa kuhudhuria vikao hivyo haiingii akilini na kama wengine walivyosema ni "wizi" wa wazi. Tukikubali mantiki hiyo lazima tuangalie kile kinachoitwa "posho ya Ubunge"
Mbunge analipwa posho ya Ubunge kwa vile yeye ni Mbunge- sijui kama kuna Posho ya Urais au ya Udiwani! Na sina uhakika kama Madaktari wanalipwa "posho ya udaktari" na wahasimu wa serikali wanalipwa "posho ya Uhasibu" au yumkini kuna posho ya weledi fulani ambayo mtu analipwa. Siwezi kushangaa ipo posho ya "ualimu" au ya "udereva". Lakini kwa vile sijui hayo mengine nigusie hii ya "ubunge".
Mbunge anapogombea Ubunge anagombea nafasi ya ajira na anapopata analipwa mshahara wa Mbunge. Siyo kazi ambayo alilazimishwa au kupewa baada ya kushikiliwa bunduki kichwani. Aliiomba kazi hiyo na alijua inakuja na majukumu mbalimbali. ni kwa sababu hiyo Mbunge analipwa mshahara na ameweka maslahi mengine tofauti kama Mbunge (mkopo mkubwa wa gari, nasikia wanajengenewa nyumba - sitashangaa wakauziwa kila mwisho wa term)). Lakini kumpa posho ya Ubunge tena!?
Posho ya vikao iondoke na pamoja (siyo ikifuatiwa) na posho ya Ubunge kwani zote mbili zinakataa mantiki.
POSHO ZA MADIWANI
Mimi kama Diwani nalipwa (sio mshahara) kwa mwezi shilingi laki moja na ishirini (Tzs 120,000).
Posho ya Kikao cha Halmashauri ni 50,000 x 4
Posho ya Vikao vya Kamati 50,000 X 4
Posho ya vikao vya ALAT 65,000
POSHO ZA WABUNGE
Posho ya mafuta 2500 kwa Lita 1000 = 2,500,000
Posho za Kikao = 100,000
Posho za ukarabati wa gari – 1,000,000
Posho za Dereva – 400,000 (mbunge anaamua amlipe kiasi gani dereva)
Posho za Jimbo – 450,000 (nje ya Mfuko wa Jimbo)
(I stand to be corrected)
Posho za Vikao zinapingwa kwa sababu zinakataa mantiki- Mbunge kutokana na nafasi yake ni wazi atahudhuria vikao mbalimbali vinavyoendana na majukumu yake hivyo kumlipa posho kwa kuhudhuria vikao hivyo haiingii akilini na kama wengine walivyosema ni "wizi" wa wazi. Tukikubali mantiki hiyo lazima tuangalie kile kinachoitwa "posho ya Ubunge"
Mbunge analipwa posho ya Ubunge kwa vile yeye ni Mbunge- sijui kama kuna Posho ya Urais au ya Udiwani! Na sina uhakika kama Madaktari wanalipwa "posho ya udaktari" na wahasimu wa serikali wanalipwa "posho ya Uhasibu" au yumkini kuna posho ya weledi fulani ambayo mtu analipwa. Siwezi kushangaa ipo posho ya "ualimu" au ya "udereva". Lakini kwa vile sijui hayo mengine nigusie hii ya "ubunge".
Mbunge anapogombea Ubunge anagombea nafasi ya ajira na anapopata analipwa mshahara wa Mbunge. Siyo kazi ambayo alilazimishwa au kupewa baada ya kushikiliwa bunduki kichwani. Aliiomba kazi hiyo na alijua inakuja na majukumu mbalimbali. ni kwa sababu hiyo Mbunge analipwa mshahara na ameweka maslahi mengine tofauti kama Mbunge (mkopo mkubwa wa gari, nasikia wanajengenewa nyumba - sitashangaa wakauziwa kila mwisho wa term)). Lakini kumpa posho ya Ubunge tena!?
Posho ya vikao iondoke na pamoja (siyo ikifuatiwa) na posho ya Ubunge kwani zote mbili zinakataa mantiki.
POSHO ZA MADIWANI
Mimi kama Diwani nalipwa (sio mshahara) kwa mwezi shilingi laki moja na ishirini (Tzs 120,000).
Posho ya Kikao cha Halmashauri ni 50,000 x 4
Posho ya Vikao vya Kamati 50,000 X 4
Posho ya vikao vya ALAT 65,000
POSHO ZA WABUNGE
Posho ya mafuta 2500 kwa Lita 1000 = 2,500,000
Posho za Kikao = 100,000
Posho za ukarabati wa gari – 1,000,000
Posho za Dereva – 400,000 (mbunge anaamua amlipe kiasi gani dereva)
Posho za Jimbo – 450,000 (nje ya Mfuko wa Jimbo)
(I stand to be corrected)