Posho za Ubunge nazo zifutwe

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Salaam,

Posho za Vikao zinapingwa kwa sababu zinakataa mantiki- Mbunge kutokana na nafasi yake ni wazi atahudhuria vikao mbalimbali vinavyoendana na majukumu yake hivyo kumlipa posho kwa kuhudhuria vikao hivyo haiingii akilini na kama wengine walivyosema ni "wizi" wa wazi. Tukikubali mantiki hiyo lazima tuangalie kile kinachoitwa "posho ya Ubunge"

Mbunge analipwa posho ya Ubunge kwa vile yeye ni Mbunge- sijui kama kuna Posho ya Urais au ya Udiwani! Na sina uhakika kama Madaktari wanalipwa "posho ya udaktari" na wahasimu wa serikali wanalipwa "posho ya Uhasibu" au yumkini kuna posho ya weledi fulani ambayo mtu analipwa. Siwezi kushangaa ipo posho ya "ualimu" au ya "udereva". Lakini kwa vile sijui hayo mengine nigusie hii ya "ubunge".

Mbunge anapogombea Ubunge anagombea nafasi ya ajira na anapopata analipwa mshahara wa Mbunge. Siyo kazi ambayo alilazimishwa au kupewa baada ya kushikiliwa bunduki kichwani. Aliiomba kazi hiyo na alijua inakuja na majukumu mbalimbali. ni kwa sababu hiyo Mbunge analipwa mshahara na ameweka maslahi mengine tofauti kama Mbunge (mkopo mkubwa wa gari, nasikia wanajengenewa nyumba - sitashangaa wakauziwa kila mwisho wa term)). Lakini kumpa posho ya Ubunge tena!?

Posho ya vikao iondoke na pamoja (siyo ikifuatiwa) na posho ya Ubunge kwani zote mbili zinakataa mantiki.
POSHO ZA MADIWANI
Mimi kama Diwani nalipwa (sio mshahara) kwa mwezi shilingi laki moja na ishirini (Tzs 120,000).

Posho ya Kikao cha Halmashauri ni 50,000 x 4
Posho ya Vikao vya Kamati 50,000 X 4
Posho ya vikao vya ALAT 65,000

POSHO ZA WABUNGE

Posho ya mafuta 2500 kwa Lita 1000 = 2,500,000
Posho za Kikao = 100,000
Posho za ukarabati wa gari – 1,000,000
Posho za Dereva – 400,000 (mbunge anaamua amlipe kiasi gani dereva)
Posho za Jimbo – 450,000 (nje ya Mfuko wa Jimbo)

(I stand to be corrected)
 
bora hata madaktari wangepewa posho kwa kuhudhuria au kuwepo hospitalini kuliko hawa wanasiasa ambao asilimia 80% ya ahadi zao hawajawahi kutekeleza au hazitekelezeki
 
Mkuu hiyo ya ubunge ni ipi tena? Nadhani ni vyema aneyezijua posho wanazolipwa wabunge na kwa sababu gani atuorodheshee hapa ili tuzipime. Kwa mfano hivi sasa tunajadili suala la posho ya vikao na tumeona kimantiki haitakiwi kulipwa kwa sababu kukaa bungeni ni kazi ya mbunge. Nawe mkuu umekuja na hii ya ubunge mimi sijajua inalipwa kwa sababu gani au inalipwa kwa kuwa mbunge kama ambavyo ukiwa askari unalipwa posho ya chakula?

Ni vema tukazijua posho zote tuzijadili na zinazostahili tuwaachie kama vile per diem japokuwa na yenyewe ina mgogoro kwa kuwa wengi wana nyumba zao dodoma. Hivi mbunge wa Dodoma mjini naye analipwa per diem?
 
Kwenye kikao cha Bunge Jummane (14[SUP]th[/SUP] June 2011), Naibu Waziri wa Uchukuzi, Athumani Mfutakamba alinukiliwa na vyombo vya habari akisema kuwa serikali haina uwezo wa kujenga Reli ya Mchuchuma/Liganga-Mtwara kutokana na uwezo mdogo kifedha. Alisema mradi huo utagharimu kiasi cha dola 1.5 bilioni za Marekani ambazo ni sawa na Sh 2.250 trilioni kiasi ambacho alisema ni kikubwa kwa nchi ya Tanzania peke yake!

Aliyeuliza hilo swali alikuwa ni Mh Mariamu Kasembe (mbunge wa Masasi- CCM). Sina shaka mbunge huyu atarudi jimboni kwake na kuwaambia wananchi ameuliza swali na serikali imesema haina fedha, lakini atendelea kuikumbusha serikali. Hata hivyo mbunge huyu anshindwa kuona kuwa yeye kama mbunge anachangia kutokuwepo kwa hii Reli.

Hoja yangu ya msingi hapa ni kwambwa both Naibu Waziri na huyu mbunge (wote ni ccm) wanasahau kwa mwaka wabunge wanachukuwa takribani trillion moja kama posho ya kukaa kitako kwenye eneo la kazi! (0.9 trillion). Sasa kama serikali itakomesha ‘huu wizi' basi ndani y miaka miwili na nusu tu wanaweza kujenga hiyo Reli ya Mchuchuma/Liganga-Mtwara.

Hii inadhihirisha wazi kuwa Tanzania haitaji kuwa ombaomba ila wabunge (na hasa wa ccm) wameshindwa au wamemua kwa makusudi kuendesha hii nchi kwa ‘umetonya' kwa sababu mapato ya nchi yanashia kwenye mifuko yao. You can see it very clear where the problem lies.
 
Mkuu hiyo ya ubunge ni ipi tena? Nadhani ni vyema aneyezijua posho wanazolipwa wabunge na kwa sababu gani atuorodheshee hapa ili tuzipime. Kwa mfano hivi sasa tunajadili suala la posho ya vikao na tumeona kimantiki haitakiwi kulipwa kwa sababu kukaa bungeni ni kazi ya mbunge. Nawe mkuu umekuja na hii ya ubunge mimi sijajua inalipwa kwa sababu gani au inalipwa kwa kuwa mbunge kama ambavyo ukiwa askari unalipwa posho ya chakula?

Ni vema tukazijua posho zote tuzijadili na zinazostahili tuwaachie kama vile per diem japokuwa na yenyewe ina mgogoro kwa kuwa wengi wana nyumba zao dodoma. Hivi mbunge wa Dodoma mjini naye analipwa per diem?

hapo kwenye RED i ni milioni 5 kila mwezi wanalipwa kwa kuwa wabunge msharaha wao ni
milioni 2 jumla inakuwa saba.

ndio maana Zitto alipogonga sitting allowance walikuja juu maana wanajua mengi yanaweza kuibuka.
hiyo milioni tano kama sikosehi inatakiwa kutumika kumlipia katibu wa mbunge mshahara wake
lakini wabunge wetu hawana makatibu, makatibu wao ni wapwa zao lakini kiutaratibu alitakiwa kuwa mtu
aliyemaliza kidato cha sita.
kwa maana hiyo kila jimbo linatakiwa kuwa na katibu na mbunge wake ili wananchi wasikose mtu wa kusikiliza
shida zao mbunge akiwa mjengoni.
wabunge kwa kutumia hati miliki za majimbo walizojipatia wanaona kuweka katibu ni kama kujitengenezea mwaasi wa baadaye na
kuchukuwa jimbo maana wengi wa wabunge wetu wameununua kwa bei kubwa sana.

hii nchi ina wizi mwingi kwa sababu wabunge wetu wengi ni wachafu na wamekwenda mjengoni kutajirika, bora kuondaa haya maposho
ili watu watakao gombea ubunge iwe kuwakilisha kweli na sio kutajirika.
sera za chama chetu cha mapinduzi bado zinatumaliza TIME IS NOW kama hawafuti hizo posho za kujikimu dawa ni sisi
wananchi kuwadai posho za kujikimu na hali ngumu ya maisha kama walivyofanya vyuo vikuu sasa watakula 10000
 
hapo kwenye RED i ni milioni 5 kila mwezi wanalipwa kwa kuwa wabunge msharaha wao ni
milioni 2 jumla inakuwa saba.

ndio maana Zitto alipogonga sitting allowance walikuja juu maana wanajua mengi yanaweza kuibuka.
hiyo milioni tano kama sikosehi inatakiwa kutumika kumlipia katibu wa mbunge mshara wake
lakini wabunge wetu hawana makatibu makatibu wao ni wapwa zao lakini kiutaratibu alitakiwa kuwa mtu
aliyemaliza kidato cha sita.
kwa maana hiyo kila jimbo linatakiwa kuwa na katibu na mbunge wake ili wananchi wasikose mtu wa kusikiliza
shida zao mbunge akiwa mjengoni.
wabunge kwa kutumia hati miliki za majimbo walizojipatia wanaona kuweka katibu ni kama kujitengenezea muasi wa baadaye na
kuchukuwa jimbo maana wengi wa wabunge wetu wameununua kwa bei kubwa sana.

hii nchi ina wizi mwingi kwa sababu wabunge wetu wengi ni wachafu na wamekwenda mjengoni kutajilika, bora kuondaa haya maposho
ili watu watakao gombea ubunge iwe kuwakilisha kweli na sio kutajilika.
sera za chama chetu cha mapinduzi bado zinatumaliza TIME IS NOW kama hawafuti hizo posho za kujikimu dawa ni sisi
wananchi kuwadai posho za kujikimu na hali ngumu ya maisha kama walivyofanya vyuo vikuu sasa watakula 10000

Mzee JF ingekuwa na critics kama wewe kumi hivi hadhi ya zamani ingerudi, umesema maneno makali sana ila yote ni ukweli mtupu. Tatizo linalotusibu wa Tanzania ni ubinafsi na hii inayoonekana kwa wabunge wetu ni reflection ya jamii nzima maana hawa si malaika kusema walishushwa ila ni wenzetu miongoni mwetu..
 
hapo kwenye RED i ni milioni 5 kila mwezi wanalipwa kwa kuwa wabunge msharaha wao ni
milioni 2 jumla inakuwa saba.

ndio maana Zitto alipogonga sitting allowance walikuja juu maana wanajua mengi yanaweza kuibuka.
hiyo milioni tano kama sikosehi inatakiwa kutumika kumlipia katibu wa mbunge mshara wake
lakini wabunge wetu hawana makatibu makatibu wao ni wapwa zao lakini kiutaratibu alitakiwa kuwa mtu
aliyemaliza kidato cha sita.
kwa maana hiyo kila jimbo linatakiwa kuwa na katibu na mbunge wake ili wananchi wasikose mtu wa kusikiliza
shida zao mbunge akiwa mjengoni.
wabunge kwa kutumia hati miliki za majimbo walizojipatia wanaona kuweka katibu ni kama kujitengenezea muasi wa baadaye na
kuchukuwa jimbo maana wengi wa wabunge wetu wameununua kwa bei kubwa sana.

hii nchi ina wizi mwingi kwa sababu wabunge wetu wengi ni wachafu na wamekwenda mjengoni kutajilika, bora kuondaa haya maposho
ili watu watakao gombea ubunge iwe kuwakilisha kweli na sio kutajilika.
sera za chama chetu cha mapinduzi bado zinatumaliza TIME IS NOW kama hawafuti hizo posho za kujikimu dawa ni sisi
wananchi kuwadai posho za kujikimu na hali ngumu ya maisha kama walivyofanya vyuo vikuu sasa watakula 10000

Hapa kweli yataibuka mengi. 5 mill posho kwa mwezi. Hiyo rate imefikiwafikiwaje?
 
Kwenye kikao cha Bunge Jummane (14[SUP]th[/SUP] June 2011), Naibu Waziri wa Uchukuzi, Athumani Mfutakamba alinukiliwa na vyombo vya habari akisema kuwa serikali haina uwezo wa kujenga Reli ya Mchuchuma/Liganga-Mtwara kutokana na uwezo mdogo kifedha. Alisema mradi huo utagharimu kiasi cha dola 1.5 bilioni za Marekani ambazo ni sawa na Sh 2.250 trilioni kiasi ambacho alisema ni kikubwa kwa nchi ya Tanzania peke yake!

Aliyeuliza hilo swali alikuwa ni Mh Mariamu Kasembe (mbunge wa Masasi- CCM). Sina shaka mbunge huyu atarudi jimboni kwake na kuwaambia wananchi ameuliza swali na serikali imesema haina fedha, lakini atendelea kuikumbusha serikali. Hata hivyo mbunge huyu anshindwa kuona kuwa yeye kama mbunge anachangia kutokuwepo kwa hii Reli.

Hoja yangu ya msingi hapa ni kwambwa both Naibu Waziri na huyu mbunge (wote ni ccm) wanasahau kwa mwaka wabunge wanachukuwa takribani trillion moja kama posho ya kukaa kitako kwenye eneo la kazi! (0.9 trillion). Sasa kama serikali itakomesha ‘huu wizi' basi ndani y miaka miwili na nusu tu wanaweza kujenga hiyo Reli ya Mchuchuma/Liganga-Mtwara.

Hii inadhihirisha wazi kuwa Tanzania haitaji kuwa ombaomba ila wabunge (na hasa wa ccm) wameshindwa au wamemua kwa makusudi kuendesha hii nchi kwa ‘umetonya' kwa sababu mapato ya nchi yanashia kwenye mifuko yao. You can see it very clear where the problem lies.

Mkuu hako ni kasehemu tu kwa watu takribani 400. Sasa ukiingia huko serikalini hiyo miposho ya vikao nadhani ni mara ishirini ya hiyo. Hii kitu itawaumiza wengi na ikipita itawasaidia wengi kama hiyo saving itatumiwa ipasavyo.
 
Hapa kweli yataibuka mengi. 5 mill posho kwa mwezi. Hiyo rate imefikiwafikiwaje?

wewe unashanga hii subiria siku raisi mwenye uzalendo akiingia ikulu utashangaa KIKWETE alikuwa anavuta
ngapi kwa mwezi,
kama siko hela ya aibu usiri wa nini? kuna nchi first lady analipwa pia sasa sijui wakwetu inakuwaje.
nje ya mikataba mibovu Tanzania tumefilisiwa na posho na misharaha mineno ya vigogo pamoja na wizi,
mbaya zaidi hiyo hela wanapeleka kimagendo nje ya nchi badala ya kufungua miradi.
ndio maana BOT kamwe hawataweza kuimalisha thamani ya pesa yetu ni kutoka na hawa hawa viongozi
kuichimbia na kuipoteza kwenye mzunguko
 
Naona mnataka kuua viongozi wetu lol! Hivi mnafahamu mtu mwenye tumbo kubwa akihisi njaa anakuaje? BTW hz pesa zichinjwe ipasavyo na kama wao walivyoshika bango la kujifanya ati viongozi wa set mindset za wananch kuhusu mipango ya maendeleo ya serikali vivyo hivyo na wao waset akili zao kwa dhati kabisa katika kupunguza matumizi makubwa ya Serikali na pesa za umma na kwa dhati kabisa wafahamu kuwa kwa mujibu wa katiba kazi yao ni kuisimamia serikali na si kuitetea serikali. Tukiendelea kwa mtindo huu tutaendelea kuwa na nchi ya posho tusikatae social stratification lkn kuwe na proportionality na accountability ya dhati.
 
Hiyo "posho ya ubunge" kwa kweli ni mjumuisho wa posho mbalimbali zinazohusiana na kazi za ubunge; kama mshahara wa dereva (sielewi kwanini wabunge ndio watumishi pekee wa umma wanaoajiri madereva wao bila kusimamiwa na yeyote - hata Rais haajiri dereva wake!), posho za mafuta (nasikia ni lita 1000 kwa mwezi - haijalishi kama anatumia kiasi hicho au la) na viposho vingin.
 
Kinachonichekesha ni pale baadhi ya wabunge na viongozi wa CCM na serikali kutaka kutuaminisha kwamba hatustahili kufahamu wabunge wanapata nini na is some sort of illegal kujadili mapato ya mbunge, waziri na hata raisi. This is where I salute democracy. This kind of a discussion would have never as it is by say 1995.

Yaani wewe umeajiriwa na ajira umeomba mwenyewe unalipwa mshahara halafu tena sijui mafuta, usafiri, posho ya dereva, posho ya pombe, posho ya ulinzi, posho ya cheo etc. etc. Sasa mshahara ni wa nini? Basi nao ungechambuliwa kiposhoposho. Posho ya msosi, posho ya viatu, posho ya nguo etc.
 
Binfsi sioo Posho Napeda kuona proirity za serikali zinaenda mpaka kwenye Salary scheme.

Sikubaliani na mfumo amabo mbunge ndo kuwa best paid public employee mkoani au wilayani.

Alfu serikali inasema sera yake ni ya kilimo kwanza????? Mimi sioni hoja na sababu kwa nini mbunge awazidi hawa watu hata kwa

  • Afisa Elimu wa mkoa au wilaya
  • Mganga mkuu wa mkoa na wilaya
  • RPC au DSO
  • Mhandissi wa mkoa au wilaya
  • Bwana/bibi Nyuki au Afisa mifugo wa mkoa au wilaya
Majukumu na wajibu wa hawa watu hapo yana umhimu mkubwa na ndio hasa watu wanatakiwa frontline uboesha maisha ya watu. Kutumia lugha ya dipmoasia tuseme lengo si kuwapunguzia wabunge lakini wabunge wahakikishe watu wenye majuumu sawa na wajibu sawa au zaidi yao wanapata zaidi yao au sawa na wao.

Nitafurahi kusikia mbunge anauliza kwa nini waanawazdi mshara hao watu.?

Na kama wanaiga wazungu waangalie uko katika mkoa au aijimbo who is best paid public employeee. Always sio politician. Lakini huku africa ni vice versa
 
Salaam,

Posho za Vikao zinapingwa kwa sababu zinakataa mantiki- Mbunge kutokana na nafasi yake ni wazi atahudhuria vikao mbalimbali vinavyoendana na majukumu yake hivyo kumlipa posho kwa kuhudhuria vikao hivyo haiingii akilini na kama wengine walivyosema ni "wizi" wa wazi. Tukikubali mantiki hiyo lazima tuangalie kile kinachoitwa "posho ya Ubunge"

Mbunge analipwa posho ya Ubunge kwa vile yeye ni Mbunge- sijui kama kuna Posho ya Urais au ya Udiwani! Na sina uhakika kama Madaktari wanalipwa "posho ya udaktari" na wahasimu wa serikali wanalipwa "posho ya Uhasibu" au yumkini kuna posho ya weledi fulani ambayo mtu analipwa. Siwezi kushangaa ipo posho ya "ualimu" au ya "udereva". Lakini kwa vile sijui hayo mengine nigusie hii ya "ubunge".

Mbunge anapogombea Ubunge anagombea nafasi ya ajira na anapopata analipwa mshahara wa Mbunge. Siyo kazi ambayo alilazimishwa au kupewa baada ya kushikiliwa bunduki kichwani. Aliiomba kazi hiyo na alijua inakuja na majukumu mbalimbali. ni kwa sababu hiyo Mbunge analipwa mshahara na ameweka maslahi mengine tofauti kama Mbunge (mkopo mkubwa wa gari, nasikia wanajengenewa nyumba - sitashangaa wakauziwa kila mwisho wa term)). Lakini kumpa posho ya Ubunge tena!?

Posho ya vikao iondoke na pamoja (siyo ikifuatiwa) na posho ya Ubunge kwani zote mbili zinakataa mantiki.
POSHO ZA MADIWANI
Mimi kama Diwani nalipwa (sio mshahara) kwa mwezi shilingi laki moja na ishirini (Tzs 120,000).

Posho ya Kikao cha Halmashauri ni 50,000 x 4
Posho ya Vikao vya Kamati 50,000 X 4
Posho ya vikao vya ALAT 65,000

POSHO ZA WABUNGE

Posho ya mafuta 2500 kwa Lita 1000 = 2,500,000
Posho za Kikao = 100,000
Posho za ukarabati wa gari – 1,000,000
Posho za Dereva – 400,000 (mbunge anaamua amlipe kiasi gani dereva)
Posho za Jimbo – 450,000 (nje ya Mfuko wa Jimbo)

(I stand to be corrected)

Posho zote pamoja na ruzuku kwa vyama vya siasa ni wizi na ujambazi usiovumilika. Tunaomba posho na ruzuku vifutwe mara moja.

1.Mbunge ama mfanyakazi atayelalamika kufutwa kwa posho ajiwajibishe mwenyewe kwa kukubali kuwaachia wengine watao kubali fanya kazi chini ya mshahara husika.

2. Chama cha siasa kitakacholalamika kufutwa kwa ruzuku ama kushindwa kujiendesha kwa michango ya wanachama wake, ina maana chama hicho hakikubaliki, ni halali yake kijifie, kwanini kuendesha chama kwa jasho la watu wengine ambao hawana vyama? Hii ni sawa na mahakama ya kadhi ama baraza la maaskofu kuendeshwa na kodi ya wananchi.
 
Mimi binafsi sioni faida ya hawa wabunge.....tujenge mabweni ya kisasa dodoma,yenye vitanda na wapishi na wasafishaji pamoja na walinzi ili ku-create jobs,
Watu waombe kwenda kufanya kazi msimu wa bajeti kupika na kusafisha hilo bweni,na kuwe na mabasi ya kuwapeleka bungeni,hakuna haja ya posho kama hawataki,watu wenye moyo watagombea ubunge kwani ni nafasi ya heshima sana haswa ukiwa unawafanyia kazi maskini walio vijijini.
Kama tunataka maendeleo,inabidi tuionyeshe Africa,who is the real revolutionary!...tutaheshimika na tutaendelea.
 
Salaam,

Posho za Vikao zinapingwa kwa sababu zinakataa mantiki- Mbunge kutokana na nafasi yake ni wazi atahudhuria vikao mbalimbali vinavyoendana na majukumu yake hivyo kumlipa posho kwa kuhudhuria vikao hivyo haiingii akilini na kama wengine walivyosema ni "wizi" wa wazi. Tukikubali mantiki hiyo lazima tuangalie kile kinachoitwa "posho ya Ubunge"

Mbunge analipwa posho ya Ubunge kwa vile yeye ni Mbunge- sijui kama kuna Posho ya Urais au ya Udiwani! Na sina uhakika kama Madaktari wanalipwa "posho ya udaktari" na wahasimu wa serikali wanalipwa "posho ya Uhasibu" au yumkini kuna posho ya weledi fulani ambayo mtu analipwa. Siwezi kushangaa ipo posho ya "ualimu" au ya "udereva". Lakini kwa vile sijui hayo mengine nigusie hii ya "ubunge".

Mbunge anapogombea Ubunge anagombea nafasi ya ajira na anapopata analipwa mshahara wa Mbunge. Siyo kazi ambayo alilazimishwa au kupewa baada ya kushikiliwa bunduki kichwani. Aliiomba kazi hiyo na alijua inakuja na majukumu mbalimbali. ni kwa sababu hiyo Mbunge analipwa mshahara na ameweka maslahi mengine tofauti kama Mbunge (mkopo mkubwa wa gari, nasikia wanajengenewa nyumba - sitashangaa wakauziwa kila mwisho wa term)). Lakini kumpa posho ya Ubunge tena!?

Posho ya vikao iondoke na pamoja (siyo ikifuatiwa) na posho ya Ubunge kwani zote mbili zinakataa mantiki.
POSHO ZA MADIWANI
Mimi kama Diwani nalipwa (sio mshahara) kwa mwezi shilingi laki moja na ishirini (Tzs 120,000).

Posho ya Kikao cha Halmashauri ni 50,000 x 4
Posho ya Vikao vya Kamati 50,000 X 4
Posho ya vikao vya ALAT 65,000

POSHO ZA WABUNGE

Posho ya mafuta 2500 kwa Lita 1000 = 2,500,000
Posho za Kikao = 100,000
Posho za ukarabati wa gari – 1,000,000
Posho za Dereva – 400,000 (mbunge anaamua amlipe kiasi gani dereva)
Posho za Jimbo – 450,000 (nje ya Mfuko wa Jimbo)

(I stand to be corrected)

it could be a good idea, but hii ya kudandia-dandia kabla hoja moja haijaisha ndio moja ya prime reasons watanzania tunashindwa kwenda mbele... we want to lift both legs and still walk like human beings

PESA INATUCHANGANYA SANA SIKU HIZI
 
it could be a good idea, but hii ya kudandia-dandia kabla hoja moja haijaisha ndio moja ya prime reasons watanzania tunashindwa kwenda mbele... we want to lift both legs and still walk like human beings

PESA INATUCHANGANYA SANA SIKU HIZI
Hilo ndio tatizo letu,tunajua kabisa kuwa tulikuwa na wabunge wanaolipwa sawa na afisa utumishi na walikuwa wakifanya kazi zao kama kawaida,they were writing bills and turning them to acts and ultimately laws,designing policies na kupitisha bajeti tena wakati mgumu sana....na walikuwa na ma land rover ambayo huyaacha majimboni mwao,na tulikuwa tunapanda nao UDA kama kawaida wakiwa hapa Dar kwenye kikao cha bajeti,
Wengi wao wakati nasoma forodhani walikuwa wananunua mihogo ferry kama kawaida......sasa nini kimebadilika? Usharobaro hauwezi kutufikisha popote pale,tutabaki kusifia mbunge wangu ana benz,hummer,BMW...mara ooh ipad,whateva!
We don't need that!,...we don't need to think twice.
Nilikuwa kwenye train moja na Elijah cummings,representative wa maryland,hana dereva.Representatives wa hapa US ni watu wenye chenji zao ila most of them wakiwa DC huwa wanakaa kwenye boarding houses....remember representative Stupak? kwenye obamacare?Walimbana kwa kuwa yeye na wenzake ambao wanaitwa K-street gang walikuwa wanaishi kwenye hosteli ya kanisa ambayo hailipiwi property tax(exempted),na Rachel maddow akajaribu kuunganisha uhusiano wa kanisa(K street hostel) na representative Stupak ambaye aliongoza democrats waliokuwa wanapinga Obamacare's support on abortion.
Ni mfano tu kukuonyesha kuwa wenzetu huku wanakaa hostel na sio hotel(ambazo pia wana uwezo wa kukaa humo).
 
Na sina uhakika kama Madaktari wanalipwa... ...Lakini kwa vile sijui hayo mengine nigusie hii ya "ubunge".
Sasa kama hujui hao wengine wanalipwa au hawalipwi hizo posho, hapo unawa compare na wabunge au unafanya nini? What's the point? Why raise the issue of other professions' perks?
 
it could be a good idea, but hii ya kudandia-dandia kabla hoja moja haijaisha ndio moja ya prime reasons watanzania tunashindwa kwenda mbele... we want to lift both legs and still walk like human beings

PESA INATUCHANGANYA SANA SIKU HIZI

Tatizo ni kuwa hoja haijawekwa sawa; kuna watu wanaamini kuwa tatizo ni "sitting allowances" hivyo wakisikia sitting allowances zimefutwa basi kwao tatizo la posho linakuwa limekwisha pia. Tushughulikie tatizo zima - posho. Once and for all kwanini tufanye kwa vipande vipande?

MkamaP amegusia suala la ruzuku - hivi kwanini vyama vya siasa vinapata ruzuku ili viweze kuja kututawala? Yaani badala ya kutoa ruzuku kusaidia makampuni na taasisi zetu ziweze kujijenga vizuri katika uzalishaji sisi tunatoa ruzuku ili waje kututawala? It makes absolutely no sense at all.
 
Back
Top Bottom