SI KWELI Popo huwa hawaoni? Ni vipofu

SI KWELI Popo huwa hawaoni? Ni vipofu

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Madia haya kuwa popo haoni yana uhalisia kiasi gani wakuu?

Mimekuwa ara kadhaa nikisikia kuwa nawe huoni kama popo, je ni kweli kuwa popo haoni? Kama anaona anaona mchana na usiku?
1781593533460.png

Picha Gettyimage
 
Tunachokijua
Popo anatajwa kama mnyama wa kuvutia sana huku akiwa mamalia (mnyama) pekee mwenye uwezo wa kuruka kweli. Hadi kufikia mwaka 2025 ilibainika kuwa kuna takribani spishi 1,500 za popo duniani huku ugunduzi zaidi ukiendelea.

Tovuti ya popo nchini Uingereza inaeleza kuwa Popo wanawakilisha zaidi ya robo ya spishi zote za mamalia nchini Uingereza, na takribani asilimia 20 ya spishi zote za mamalia duniani.

Kwa miaka mingi kumekuwa na imani kuwa popo hana uwezo wa kuona huku wengine wakitumia msamiti huo kurejelea watu kwa kuwaambia "kipofu kama popo" lakini je ni upi ukweli wa madai haya?

Je, ni kweli popo hawaoni?

JamiiCheck kupitia makala kumuhusu mnyama popo zimebaini kuwa madai hayo si ya kweli, kwani popo anao uwezo wa kuona.

Popo wana macho madogo yenye uwezo mkubwa wa kuona, yanayowasaidia kuona katika mazingira yenye giza kubwa ambalo binadamu angeweza kuliona kuwa giza totoro. Ingawa hawaoni kwa ukali na rangi nyingi kama wanavyoona binadamu, uwezo huo unawatosha kwa mahitaji yao.

Kwanini Popo hupendelea kuruka zaidi usiku?

Popo ni aina ya viumbe wanaotumia muda mwingi zaidi usiku kuwa macho (nocturnal), hivyo si rahisi kumuona popo akiruka mchana. Na mara nyingi popo hawaruki mchana pia kwa kuwa wapo kwenye hatari kubwa ya kushambuliwa na wanyama wanaoruka mchana.

Hata hivyo, popo anaweza kuonekana mchana ikiwa ana njaa (kwa mfano jike mwenye mtoto anayehitaji kulishwa), ana kiu (hasa wakati wa joto kali), au amesumbuliwa na shughuli za binadamu, hali inayoweza kumlazimu kuchukua hatari zaidi ili kutafuta chakula.

Popo anawezaje kusafiri gizani?


Licha ya kuwa na uwezo wa kuona, lakini usiku popo hutumia zaidi mwangi kuliko mwanga hii huitwa (echolant) kwa ajili ya kusafiri na kuwinda.

Popo hupata njia yao gizani kwa kusikiliza mwangwi wa sauti. Wanaporuka, hutoa sauti za juu sana (ultrasound) ambazo hugonga vitu vilivyo mbele yao na kurudi kama mwangwi. Mwangwi huo huwasaidia kujua mahali vitu vilipo ili wasigongane navyo wakati wa kuruka. Pia, mwangwi huo huwasaidia popo kuwinda wadudu na wanyama wengine wanapotafuta chakula.
Akiwa anaruka usiku Kuna mlio fulani anautoa, huo mlio ndio unaofanya asiparamie kilichopo mbele yake mfono ukuta, kutokana na kuwa mawimbi ya sauti aitoayo hugonga kile kilichopo mbele yake na kurudi masikioni mwake, jambo linalofanya akwepe kizuizi hicho.

Hii ☝️ ni kwa mujibu wa baba yangu Mdinyakobe Kimario.

kwa ufafanuzi zaidi King Kong III anakuja.
 
Akiwa anaruka usiku Kuna mlio fulani anautoa, huo mlio ndio unaofanya asiparamie kilichopo mbele yake mfono ukuta, kutokana na kuwa mawimbi ya sauti aitoayo hugonga kile kilichopo mbele yake na kurudi masikioni mwake, jambo linalofanya akwepe kizuizi hicho.

Hii ☝️ ni kwa mujibu wa baba yangu Mdinyakobe Kimario.

kwa ufafanuzi zaidi King Kong III anakuja.
Hahaa umenikumbusha enzi hizo form II Doppler Effect.
 
Akiwa anaruka usiku Kuna mlio fulani anautoa, huo mlio ndio unaofanya asiparamie kilichopo mbele yake mfono ukuta, kutokana na kuwa mawimbi ya sauti aitoayo hugonga kile kilichopo mbele yake na kurudi masikioni mwake, jambo linalofanya akwepe kizuizi hicho.

Hii ☝️ ni kwa mujibu wa baba yangu Mdinyakobe Kimario.

kwa ufafanuzi zaidi King Kong III anakuja.
Kila nikiona hii ID nakumbuka ile story ya mzee wako ambaye alinga'twa na Paka sehemu zake za siri.
 
Mkuu, Sijapewa username bado soma huu 👇 mkasa na upate kujifunza.


Ilikuwa mwaka 1998 mwezi wa tatu ambapo baba yangu alikumbwa na balaa zito lisiloelezeka kirahisi.

Kwanza kabisa baba yangu alikuwa anapendea sana kuvaa kanzu na ni mara chache sana kumkuta akiwa amevaa nguo nyingine tofauti na kanzu.

Baba yangu anawapenda sana mbwa na paka na Kwa kipindi... Kilichomkuta baba yangu miaka kadhaa iliyopita kisa kuvaa kanzu bila nguo ya ndani, soma ujifunze kitu
 
Mkuu, Sijapewa username bado soma huu 👇 mkasa na upate kujifunza.


Ilikuwa mwaka 1998 mwezi wa tatu ambapo baba yangu alikumbwa na balaa zito lisiloelezeka kirahisi.

Kwanza kabisa baba yangu alikuwa anapendea sana kuvaa kanzu na ni mara chache sana kumkuta akiwa amevaa nguo nyingine tofauti na kanzu.

Baba yangu anawapenda sana mbwa na paka na Kwa kipindi... Kilichomkuta baba yangu miaka kadhaa iliyopita kisa kuvaa kanzu bila nguo ya ndani, soma ujifunze kitu
Asante mkuu ndege mwandishi mwendesha ofisi, nitaupitia
 
Back
Top Bottom