Pongezi kwa TANESCO Dodoma, wanatatua matatizo ya wateja kwa wakati

the glassroof

JF-Expert Member
Apr 25, 2017
279
422
Ni mara tatu sasa mfululizo nakumbwa na matatizo ya umeme tena mida mibovu.
Kwa mara ya kwanza, tatizo lilipotokea sikujua nianzie wapi bahati nzuri nikapekuwa majina kwenye phone book yangu nikakuta jina moja la mtumishi wa TANESCO.
Nikampigia nakumuelezea tatizo langu, kwa kuwa ilikuwa mida mibovu akashauri niwapigie emergency mara moja.

Akili yangu ikanituma bora nipotezee tu, emergency na wabongo wapi na wapi. Na nikikumbuka TANESCO niliyokuwa naifahamu mmi, kuwapata mpaka utambikie.
Ila nikajisemea tena ngoja nijaribu.

Ile kupiga tu, napokelewa na mdada fulani akajitambulisha vizuri kabisa. Nikaeleza shida yangu mpaka mwisho bila kikwazo chochote.
Alichofanya yeye, ni kuniuliza mtaa ninaoishi na namba ya simu. Mwisho akasema, subiri muda si mrefu emergency watafika hapo kukusaidia na ilikuwa mishare kama ya 2 hivi usiku.

Mungu si athumani, by saa 3:30 usiku hivi simu ikaita, kucheki namba mpya nikapokea. Kijana mmoja kajitambulisha na kusema simama barabarani gari ya TANESCO itafika hapo hivi punde.

Mara paaaap! Vijana kweli hawa shusha ngazi panda rekebisha mambo safi kabisa bila kudai chochote. Wakanipa kijikaratasi fulani wao wanaita TB nadhani, ili asubuhi yake nifike ofisini kukamilisha suala langu.

Kesho yake huyo mjengoni, huduma safi kabisa, mpaka nikasema kulikoni ofisi hizi. Anyway, chap chap huduma nikapewa nikaenda zangu.

Baada ya siku kadhaa, Mita yangu ikapata hitilafu tena mida mibovu, nikapiga emergency, muda si muda hawa hapa wakatua. Ile kuchek Mita kumbe imeungua wakaahidi kesho watakuja kunibadilishia, bila hiana kesho yake mapemaaa! timu hiyo home wakabadili Mita bila longo longo na mpaka sasa nakula good time tu.

Haya yakiwa yanatendeka majirani nao wanashangaa kulikoni huyu jamaa anahudumiwa fasta kiasi hiki au wale wale. Kumbe wala, mie pangu pakavu sijui hili wala lile katika fani hiyo.

Siku ya siku mmoja wapo wa majirani zangu akapata shida, akaja kwangu nakuomba niwapigie. Kwa kujiamini kabisa nikavuta waya na bila kupoteza muda kama kawaida yao TANESCO wakafika na kutatua tatizo la jirani ambaye ni mfanyabiashara anaetegemea umeme asilimia ili mambo yake yaende.

Kutokana na experience hiyo waungwana nisiwachoshe, TANESCO Dodoma, kusema ukweli mmetisha kinoma noma. Taasisi zingine za serikali zijifunze kwa hawa jamaa.
Ni hayo tu. Big up sana na Mungu awabariki.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwao sema haya mambo ni sikuhizi tuu.

Back in days wakati Nkuhungu inaonekana kijiji, tulihamia nyumba yetu haina umeme, yani Tanesco gari inapita mbele ya mtaa inafunga umeme nyumba ya 5 wakati hao walihamia wametukuta.

It was sad aisee kuona watu wamehamia na kwao taa inawaka na hela tumelipa kitambo sana. Mama kila alikuwa akienda sokoni au mjini anaanzia TANESCO.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwao sema haya mambo ni sikuhizi tuu.

Back in days wakati Nkuhungu inaonekana kijiji, tulihamia nyumba yetu haina umeme, yani Tanesco gari inapita mbele ya mtaa inafunga umeme nyumba ya 5 wakati hao walihamia wametukuta.

It was sad aisee kuona watu wamehamia na kwao taa inawaka na hela tumelipa kitambo sana. Mama kila alikuwa akienda sokoni au mjini anaanzia TANESCO.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna namna wamelitazama shirika hili la umma liwe na tija kwa taifa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pongezi ziwaendee wafanyakazi wote hasa meneja wa TANESCO Dodoma. Mimi huwa nikienda kwenye taasisi fulani kupata huduma halafu nikaona huduma zao hadhirishi au hawajali wateja wala muda wa wateja wakati huo huo wanakiongozi wao anao wasimamia tena anapatikana humo humo mimi huwa na assume kiongozi wao ndio ana matatizo.
 
Pongezi ziwaendee wafanyakazi wote hasa meneja wa TANESCO Dodoma. Mimi huwa nikienda kwenye taasisi fulani kupata huduma halafu nikaona huduma zao hadhirishi au hawajali wateja wala muda wa wateja wakati huo huo wanakiongozi wao anao wasimamia tena anapatikana humo humo mimi huwa na assume kiongozi wao ndio ana matatizo.
Sio assumption mkuu huo ndio ukweli.

Uongozi m-bovu = Huduma mbovu
 
Hata DUWASA Dodoma wanajitahidi kurespond matatizo ya wateja kwa wakati endapo ukiwapiga simu au hata kwenda ofisini kwao. Taasisi zote za umma zinapaswa kuwa namna hii. Nadhani hapa suala ni uongozi hauchekicheki na watumishi wazembe. Taasisi nyingi za umma kuoneana aibu ndio chanzo cha ku perform chini ya kiwango

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata DUWASA Dodoma wanajitahidi kurespond matatizo ya wateja kwa wakati endapo ukiwapiga simu au hata kwenda ofisini kwao. Taasisi zote za umma zinapaswa kuwa namna hii. Nadhani hapa suala ni uongozi hauchekicheki na watumishi wazembe. Taasisi nyingi za umma kuoneana aibu ndio chanzo cha ku perform chini ya kiwango

Sent using Jamii Forums mobile app
Hongera mkuu, binafsi huwa nachukia sana kuona kiongoz wa umma anijivuta vuta kwenye kuhudumia wananchi ilihali anaempotezea ndo mwajiri wake kimsingi maana bila kodi hana kazi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pongezi ziwaendee wafanyakazi wote hasa meneja wa TANESCO Dodoma. Mimi huwa nikienda kwenye taasisi fulani kupata huduma halafu nikaona huduma zao hadhirishi au hawajali wateja wala muda wa wateja wakati huo huo wanakiongozi wao anao wasimamia tena anapatikana humo humo mimi huwa na assume kiongozi wao ndio ana matatizo.
Uko sahihi, kwa kweli meneja abarikiwe sana. Nilishakutana nae one day nikiwa na shida ya kubadilishiwa nguzo ya ofisini kwetu alinisaidia kwa haraka sana hata sikutegemea.

Nakumbuka huyu bwana anaitwa Engineer Nyali by that time sijui alikuwa anakaimu. Hongera sana bro popote ulipo. You are a good leader.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom