Kwa moyo safi kabisa napenda kumpongeza/kuwapongeza wakandarasi walioetengeneza na wanaomalizia barabara hiyo,nilikuwa nina muda kidogo sijapita njia hiyo leo ndo nimepita,ki ukweli sikuamini macho yangu jinsi barabara ilivyotulia hasa kipande cha kutoka mikumi hadi iringa kuna maeneo yalikuwa kero kupitiliza kiasi ambacho hata magari kupishana ilikuwa patashika,lakini leo nimepita magari yanapishana vizuri kabisa.
Tahadhari:
Wasimamizi na wakaguzi tunaomba wathibitishe ubora wa barabara hizo isijekuwa ni bomu ambalo litalipuka miaka michache ijayo,na wenye magari ya mizigo tunaomba wapitishe uzito ambao unastahili na kuzingatia matumizi bora ya barabara.
Tahadhari:
Wasimamizi na wakaguzi tunaomba wathibitishe ubora wa barabara hizo isijekuwa ni bomu ambalo litalipuka miaka michache ijayo,na wenye magari ya mizigo tunaomba wapitishe uzito ambao unastahili na kuzingatia matumizi bora ya barabara.