Pongezi kwa askari polisi wa Posta

Pongezi kwa askari polisi wa Posta

ashy da don

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2013
Posts
615
Reaction score
671
Wakuu habari za jioni humu ndani.
Najua wengi wetu ikiwemo mimi tunawachukia sana askari polisi kutokana na vitendo vyao vya unyanyasaji kwa raia.
Kwa hili nililoshuhudia hapa kituo cha stesheni ningeomba nichukue fursa hii kuwapongeza sana askari hawa. Takribani ni mwezi sasa nimeukuta utaratibu ambapo polisi husimamisha madaladala yote yanayotoka Mbagala rangi tatu, na Temeke na kuwaamuru wanafunzi wapande kwanza kwa utaratibu maalumu wa kupanga mstari na kila gari kuchukua wanafunzi takribani watano..
Utaratibu huu umenifurahisha sana kwani nikikumbuka enzi hizo nasoma Benjamin Mkapa tulikua tunasumbuliwa sana na makonda hadi kufikia hatua ya kuleta uadui kati yetu na wao.

Nachukua fursa hii Kuwapongeza jeshi letu hili la polisi na kuomba rai kwa vituo vingine kuiga mtindo huu kama polisi hawa..
 
safi saana, ulisoma mwaka gani mkuu. mimi pia nilisoma hapo
 
Wakuu habari za jioni humu ndani.
Najua wengi wetu ikiwemo mim tunawachukia sana askari polisi kutokana na vitendo vyao vya unyanyasaji kwa raia.
Kwa hili nililoshuhudia hapa kituo cha stesheni ningeomba nichukue fursa hii kuwapongeza sana askari hawa. Takribani ni mwezi sasa nimeukuta utaratibu ambapo polisi husimamisha madaladala yote yanayotoka Mbagala rangi tatu, na Temeke na kuwaamuru wanafunzi wapande kwanza kwa utaratibu maalumu wa kupanga mstari,na kila gari kuchukua wanafunzi takribani watano..
Utaratibu huu umenifurahisha sana kwani nikikumbuka enzi hizo nasoma Benjamin Mkapa tulikua tunasumbuliwa sana na makonda hadi kufikia hatua ya kuleta uadui kati yetu na wao.
Nachukua fursa hii Kuwapongeza jeshi letu hili la polisi na kuomba rai kwa vituo vingine kuiga mtindo huu kama polisi hawa..

unaweza ukawa classmate wewe ulimaliza benja mwaka gani
 
Ni kazi nzuri na inastahili kupongezwa, ila isije tu ikawa ni mbwembwe za kuelekea uchaguzi!
 
Bravo!! Wenzetu wa Nairobi hii kitu ipo toka zamani. Ingekuwa vema sana ifanyike katika vituo vyote
 
kweli ni la kuwapongeza...sasa maaskari mliopo humu msije mkalewa sifa na mkabadilika
 
Hivyo ndivyo tunavyopenda kusikia.

Kidogo kidogo tutafika tu, itafikia pia kuwapa kipa umbele wakina mama wajawazito.

Maana linapokuja suala la ustaarabu kwenye madalala kwa kweli tunashindwa, ni kugombania.

Kwa hilo nawapongezeni sana, safi
 
kweli ni la kuwapongeza...sasa maaskari mliopo humu msije mkalewa sifa na mkabadilika

Yah inapendeza sana mkuu. Unaweza kuta jitu la miraba minne linaekeana msuli na kitoto cha shule ya msingi.kwa huu utaratibu ni wa kupongezwa sana. Wanafunzi wanapanda bila bugudha yoyote ile
 
Hivyo ndivyo tunavyopenda kusikia.

Kidogo kidogo tutafika tu, itafikia pia kuwapa kipa umbele wakina mama wajawazito.

Maana linapokuja suala la ustaarabu kwenye madalala kwa kweli tunashindwa, ni kugombania.

Kwa hilo nawapongezeni sana, safi

Ni kweli mkuu. Ustaarabu kwenye madaladala ni sifuri kabisa. Imetokana na kuwa wengi wanaopanda wana tabia mbalimabli na ukichanganya na kazi tunazofanya hzi huku mjini.. Tupo kama machizi vile hakuna hata anayejali ustaarabu.
 
Wakuu habari za jioni humu ndani.
Najua wengi wetu ikiwemo mim tunawachukia sana askari polisi kutokana na vitendo vyao vya unyanyasaji kwa raia.
Kwa hili nililoshuhudia hapa kituo cha stesheni ningeomba nichukue fursa hii kuwapongeza sana askari hawa. Takribani ni mwezi sasa nimeukuta utaratibu ambapo polisi husimamisha madaladala yote yanayotoka Mbagala rangi tatu, na Temeke na kuwaamuru wanafunzi wapande kwanza kwa utaratibu maalumu wa kupanga mstari,na kila gari kuchukua wanafunzi takribani watano..
Utaratibu huu umenifurahisha sana kwani nikikumbuka enzi hizo nasoma Benjamin Mkapa tulikua tunasumbuliwa sana na makonda hadi kufikia hatua ya kuleta uadui kati yetu na wao.
Nachukua fursa hii Kuwapongeza jeshi letu hili la polisi na kuomba rai kwa vituo vingine kuiga mtindo huu kama polisi hawa..

mkuu mimi hiyo imeniathiri hadi sasa nilipo nawachukia makondakta wa daladala! nawachukia kutoka moyoni.... walisababisha nlichelewa sana vipindi shuleni!!
 
Back
Top Bottom