Pongezi Dr. Kitila Mkumbo

Status
Not open for further replies.

sir Alex Ferguson alimpiga kiatu David Beckham kwa kujifanya yeye ni zaidi ya Man U. Kazito katoke tu au kakiri na kujishusha
 

Huo ndo uelewa wako na mawazo yako and your promises can mislead the conclusion..
 

Umenena kweli kabisa
 
Kitila maefanya sana siasa za jukwaani...Umesahau kisa cha kule Iramba walipokuwa na Mnyika na Mwita Waitara mpaka Mwigulu Nchemba akatuma vijana wakafanye fujo kwenye mkutano? Unaposema Zitto asamehewe unamaanisha nini wakati mwenyewe hajaomba msamaha wala hajakiri makosa? Mtu akikana mashtaka, kazi ya mtoa mashtaka huwa ni kuthibitisha hayo mashtaka na baada ya haponi hukumu sio msamaha tena......Wahafidhina watawezaje kufanya kazi na Mwana demokrasia Zitto? Wenye Elimu ya maghumashi watafanyeje kazi na wenye elimu kubwa? Ni jambo lisilo wezekana kabisa
 
Pasco, na wewe Pamoja na unguli wako katika Medani za uchambuzi wa Siasa unaamini Kabisa Zitto hakuwa aware na ule waraka ????
Ulitaka Dr Kitttila aseme wazi wazi kuwa Zitto alikuwa aware na ule Waraka, huoni kuwa kaamua kusema tu kuwa Zitto hakuwa aware lakini anajua kabisaaa kuwa watu na akili zao watajua what was behind the scene ??? Pasco as days goes on hapa JF binafsi nazidi kuku rank na wale jamaa wa Buku 7 Project Fame Lumumba.
 
Last edited by a moderator:

Pengine ZZK mnamsikia tuu. Mpaka sasa yupo 1000 steps ahead of his enemies, vifaranga wooote mnataka hili jogoo ZZK lichinjwe. Lakini mama zenu wanajua athari za kulichinja hili jogoo. Kwani banda LA kuku bila jogoo so banda tena
 
Mkuu Bramo, naamini Mbowe anaujua ukweli halisi, Dr. Slaa anaujua ukweli halisi na kila mwenye akili tiumamu anaujua ukweli halisi ukiwaondoa wale waliozikabidhi akili zao kwa viongozi wa Chadema ndio pekee wasiujua ukweli kwa sababu akili za kuujua ukweli wamezikabidhi!.

Mtayarishaji wa waraka amekiri, mshirika wa waraka amekiri, ZZK ni mlengwa, hata kama ameona, ameonyeshwa amekuwa consulted na ameiridhia hiyo move, kosa lake ni lipi?!. Wanaoamini waraka ule ni uhaini wenye lengo la kufanya mapinduzi watakuwa ni vichaa!. Chadema inavichaa wengi kuliko unavyodhania!. Ule waraka ilikuwa ni kutengeneza "a winning coalition!" a lobby group ya kuhakikisha mtu wao ZZK ndio anashinda uchaguzi wa ndani wa Chadema!.

Wakati JK anagombea ndani ya CCM, Dr Salim, was not only the threat, but was the real man!. Kilichofanywa na Mtandao, JK anakijua and my be was behind!, Dr. Salim angeamua kwenda mahakamani, angeweza kumshitaki JK?, watenda kazi ni kina Salva, jee unajua nani was behind?!. Maadamu wahusika wanajulikana hata kama ilikuwa ni JK mwenyewe, sheria za ushahidi ni aliyekutwa na ngozi, na sio aliyeona kuambiwa au kusikia!.

Zitto ajue, asijue, alishirikishwa, hakushirikishwa kosa lake ni lipi?!.
Merry X-Mass
Pasco
 

Yaah binafsi nimefurahishwa pia na his strategy,he must be 'MZUKA' kichwani.

Anajielewa,kaandaaa kisha kachuja...jamaaa kwa 100% yupo sana katika siasa za chadema na siasa bora za ulimwengu....nadhani hii law imemsaidia ni msomi huyu...'NEVER OUTSHINE THE MASTER' hii kitu ya Robert Greene law # 1 katika kitabu cha The 48 laws of POWER.

Regards.
 
Umesema anasubir maamuz ya kamat kuu..maana yke hana utetez wa kuweza kumnasua..yy anaogopa kutokea kwenye media coz hlo lna wakera viongoz na yy bila chama hana pala..zzk anajua nn anaxho kifanya..coward is a dead person who is breathing
 
kumbe umeona umhimu wa elimu? mbona kwenye waraka waliposema ""elimu ya mkuu wa taasisi si tu ni ndogo bali pia ni ya maghumashi"" mlikasirika? kumbe waraka ulikuwa sahihi!!

Unaweza ukawa na Elimu kubwa ukafanya Vibaya katika Jamii,Lakini Pia unaweza Ukawa na Elimu ndogo na ukafanya Vizuri katika Jamii,and Vice Versa is true.
 

kwa nini dr slaa alienda kumchafua zito kgm,zito anajibu uongo wa dr slaa aliodanganya wana kigoma
 

kwani Dr.Slaa alienda kutangaza dini kule kigoma?
 

Kitira amebaini kuwa CHADEMA walikuwa wakimtumia kama DODOKI hivyo ameamua kuachana nao kimtindo. Hata akisamehewa hatakuwa active member kama ilivyokuwa awali.
 
Dr anaupeo mkubwa wa fikra.
nakubaliana nae kuwa hata elimu ya mwenyekiti wetu bado ni ndogo kuendesha taasisi kubwa kama Chadema.
Ila hilo ukilisema utaambiwa msaliti.
 
Wewe pasco nakuuliza hivi uliusoma ule waraka wa siri ambapo Zitto alibainika kupokea mabillioni ya shiliungi ili akivuruge chama!!!?hakika sikuelewi kabisa wewe ni kariba ipi hasa,hivi makubaliano ya Zitto na Mwigulu na baadhi ya wanaojifanya usalama wataifa ili akiujumu chama nahivyo kuleta unafuu cha ccm iweze walau kushinda uchaguzi wa 2015 umezisoma na kutathimini mwenendo ya Zitto iliuone ni kwanini watu tunasema huyu kijana hafai kuwa mwana chama ndani ya chadema. Achilia mbali kwa mikutano yote aliyofanya sehemu mbalimbali na kuonesha dharau ya wazi kwa viongozi wa juu wa chama alafu wewe bado unamtetea huyu msaliti na muuwaji pia mdumila kuwili tamaa mbele,kumbe hata elimu ya udsm haikumsaidia kitu hakika vijana wa namna hii hawafai tena ni bora mara mia kubakia na vizee madarakani haidhuru tutasema maamzi yao wameshindwa kwa vile umri umeenda kuliko vijana kama wewe na Zitto.
 


Unampa sifa za bure;Nakushauri utafute Raia Mwema ya 25/12/2013 Toleo:N.331-TUAHIRISHE DEMOKRASIA NDANI YA VYAMA HADI CCM ITAKAPONGO'KA? Ukimaliza kusoma hiyo pitia na hii;



Baada ya hapo tupe jibu.

Ni hofu yangu JF imekwisha ingiliwa na wanasiasa na kunaubaguzi au upendeleo.

Niliweka Tread kwa heading. "NAWASHAURI CHADEMA''-KITILA MKUMBO naimefutwa alafu muda si mrefu inakuja hii ya kusifiana!
 
hata kama ni Dr, lakini kwenye pesa aliingizwa mkenge
 

Natumai umejisomea Raia Mwema ya leo; 25/12/2013 Toleo:No.331.
Hakuna cha ukimya hawa mabwana wamekwisha onana kuwa sasa wamegundulika na hivyo hakuna kurudi nyuma harakati ya kubomoa CDM wakati wake ndio huu pamoja na kwamba hawakutaka iwe kwa namna ilivyojitokeza.

Yaani mpango wa M7/masalia ilipoharibika mpango mbadala ukawa huu wa Mkakati wa Mabadiliko lakini tatizo ni kwamba umegundulika kabla ya kuzinduliwa na kwasababu muda wa kujipanga kwa sasa ni mdogo na kwa sababu mtandao utakuwa umefahamika mikakati itakuwa migumu hivyo wameona ni Bora kushawishi Wanachama na hasa lengo ni kuvuga CDM ili by 2015 iko hoi!.
labda Mkuu Ben Saanane ataleta mchango mzuri
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…