Je, ni yale yaliyoingizwa nchini na CUF kama tulivyotahadharishwa na yule askari aliyestaafu siku wanamtandao walipochukua nchi akawaachia madaraka hawa wanaokuja mitandaoni kuchungulia kinachoandikwa?
hivi ujui hata mmbuyu ulianza kama mchichaSasa watu 50 tu ndo wanaokutisha?
naamini hizi ni hisia zako tu!tatizo ni kuwa wewe hujachukua tahadhari yoyote ya kujilinda. umeshindwa hata ku-organise club ya ukakamavu mtaani kwako. hata kwenye vikundi vya ulinzi shirikishi haupo.
nashukuru kwa ushauri wako mkuuSasa wewe hiyo akili ya kujilinda unaitumiaje? utaulizwa siku ya mwisho ujue!
Hivi kwa nini sehemu yoyote waliopo waislam panafukuta moshi ?
wanotoa kashfa na vitisho kwa dini nyingine serikali hii inawafahamu hakuna siri yoyote swala je ni kwa nini wachochezi hao wanaokashifu dini nyingine na kufanya wanavyotaka hawashughulikiwi?
huu ni upuuzi, watz ni watu wa aman
mimi siwezi kuongelea shehe ilunga..ilunga namjulia hapa jf,kwenye nyuzi,simfahamu hata kwa picha.
Sasa wewe ulikuwa unadai israel imeendelea bila kuwa na data hata kidogo wajameni.
Hao matajiri wenye asili ya kiyahudi sawa wameenea marekani na wameshika nyadhifa nyeti ,wanatuma pesa israel,lakini sio wote wanaunga mkono serikali ya kibaguzi ya israel.na wanapinga serikali ya israel.watu kama albert Eistein,alikua myahudi alipinga serikali ya israel.watu kama george soro ni tajiri yuko marekani haelewani na utawala wa israel,watu kama sergei yule mwenye google ni myahudi mrusi lakini juzijuzi hapa google wameitambua palestine kama nchi.
Ukitaka link nitakuwekea.
Hata hitler alikua myahudi lakini alitofautiana na wayahudi wenzake.
Israel inaishi kwa kutegemea hela za matumizi toka marekani.wamerekani wanalalamika kuwa israel imekuwa mzigo kwao.wao wanashida pesa inapelekwa kusaidia israel,free syria army,egypt,etc.
Well, sasa tumekubaliana kuhusu huyu Sheik. Hajaandaliwa kabisa kuongoza watu sema tu hujaona DVD zake. Hili tuliache.
Kuhusu Amedinajad, wala sijakupiga chenga na kamwe sikumaanisha yangempata yalompata Ghadafi. Hawa watu ni tofauti kabisa na waliongoza/ wanaongoza makundi mawili tofauti. Naomba umfatilie akitoka madarakani kwenye miaka mitatu, labda utanielewa namaanisha nini.
hukutwambia Israel ni ya ngapi kiuchumi katika nchi za mashariki na kati. Bado tu umeunga unga maneno na kutaja watu wanaochukia uongozi wa Israel (haya yote ya nini jamani?) hivi ukitaka kupata watu wanaochukia uongozi watanzania sasa hivi, si wengi tu? kila nchi uongozi wake kuna mtu anachukia. Ila naomba urudi kwenye topic, twambie ni ya ngapi na kama hujui sema!!! (sio kosa)
Ni wamarekani gani waliolalamika kwamba Israel imekuwa mzigo kwao? tupe link au quote ya rais Obama au mtu yeyote mwenye wadhifa wa uongozi, vinginevyo tumia busara tujibizane mada zenye ukweli wala sio kuchomeka maneno. Stay blessed.
kabla sijakusoma kiundani,kwanza nakataa kwamba israel ni taifa la mungu,kama umekuwa brainwashed usidhani ni kila mtu.
Kuhusu ahmednajacket,hapa unataka kunila chenga tu,ulitaka kuimanisha yatampata yaliyompata gadaf..lakini ujue kuwa,yeye bado ako na wiki mbili tu za kuwa rais kwahiyo wamarekani hawana advantage nae ya kumuua.
SOURCE: JIBU LA MAISHA
DATE: Sunday, May 12, 2013
ISSN: 1821-6463, No. 241
PAGE: 115
HEADLINE: ASKOFU PENGO AZIDI KUTISHIWA
- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -
Kwa matoleo kadhaa ya nyuma tumeripoti matukio ya kichochezi ya kusambazwa kwa CD na DVD zinazochochea utengano baina ya wakristo na waislamu nchini. Tumefanya hivyo kwa tahadhari kubwa na hata wakati mwingine kujitahidi kujiepusha na kuchapisha habari hizo.
Hata hivyo, tunalazimika kuripoti matukio haya ili kuzikumbusha mamlaka zenye dhamana zichukue hatua kali dhidi ya makundi haya ambayo yanaonekana moja kwa moja ni maadui wa umoja wa watanzania.
Katika kile kinachoonekana nia utaratibu maalumu, imetolewa CD mpya iliyopewa jina Ndege wote walie akilia bundi uchuro ambay pamoja na mambo mengine inaonyesha picha ya Askofu Kardinal Polycarp Pengo ikiwa na maandishi yanayosomeka WANTED ikiambatana na maneno makali ya kulaani Kanisa Katoliki na hata mengine, huku picha ya mtu anayechinjwa ikitumika kama logo inayojirejea kila wakati.
Juhudi za kumpata mtu anayeonekana katika DVD hiyo akitajwa kama Imam Hamza Omary, ili kufafanua ujumbe uliopo ndani ya mkanda huo hazikfanikiwa.
DVD hiyo ambayo JIBU LA MAISHA lina nakala yake inaonyesha mhadhiri akinukuu aya za Kuran na kuwaalika wenzake kwenye kile alichokiita Jihad (baadhi ya yale yanayosemwa hatuwezi kuyaandika kutokana na sababu za kimaadili)
Katika hilo Imam Omary anasema serikali imekuwa ikiegemea upande wa maaskofu na mabaraza yake, lakini si kwa waislamu.
Mkanda huo umeonyesha baadhi ya mazoezi makali ya vijana wa Kiislamu ingawa haionyeshi yanafanyika wapi.
Mhubiri huyo aliyashutumu pia mataifa ya kimagharibi akidai yamekuwa yakitoa silaha na kuwagombanisha wao kwa wao pasipo wenyewe kujua na hilo limeonekana kwa Saddam Hussein.
Aidha alionekana akidai kuwa jambo kubwa na la hatari kwa waislam wa sasa ni kutoongelea kabisa suala la Jihad, na hilo limekuwa donda ndugu.
Bila kupepesa maneno, Imam huyo alitaja viongozi ambao alidai eti wamekuwa wakibadili yale waliyokubaliana na waislam na wamekwenda kinyume kutokana na kutiwa msukosuko.
Vingozi na wasaniasa wanaotajwa katika DVD hiyo ni pamoja na Waziri wa mambo ya nje, Bernard Membe, Katibu Mstaafu wa CCM, Yusufu Makamba, na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
Alipomaliza hilo alimgeukiwa Rais wa Uganda, Museveni na kudai yeye ni kiongozi wa Afrika Mashariki anayetaka kuhakikisha anaungoa uislam kupitia mashehe kwa juhudi zote.
Aliyekuwa Kamanda wa Mkoa wa Mwanza, marehemu Liberatus Barlow, anatajwa kwenye mkanda huo, lakini JIBU LA MAISHA halitaongelea kilichoongelewa humo.
Yusuf Makamba ambaye ni muislam, wanadai naye mwaka 1998 akiwa Mkuu wa Mkoa Dar, wakati wao wakisema nchi inatawaliwa kwa mfumo Kristo, yeye alipinga na hilo likaonekana kuwa yuko kinyume na uislam.
Mwinjilisti Cecil Simbaulanga ambaye amekuwa akipita huku na kule kutetea wakristo ili wajue haki zao anatajwa kuwasisitiza wakristo kuchinja nyama wakati inajulikana siku zote kwamba waislamu ndiyo wenye kufanya jambo hilo hapa Tanzania.
.
Wakati hayo yakitokea, tukio la kurushwa bomu katika Kanisa la Parish of St. Joseph the Worker (Olasiti), mkoani Arusha, linarandana na maudhui ya kile kinachoelezwa kwenye mikanda kadhaa inayotolewa na watu wanaoaminika kuwa na imani kali ikionyesha chuki ya wazi dhidi na kanisa hilo.
Ndani ya DVD kadhaa zenye mlengo mmoja ambazo zimezagaa maeneo kadhaa jijini Dar, hasa maeneo ya Buguruni_Chama, inaelezwa kukamatwa kukamatwa kwa maaskofu ili kuwachinja ikiwa muislam atafanyiwa ubaya wowote au kuuliwa.
- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -- - - - - - - - -
Dini ya UPANGA (Kihistoria)
Dini ya UPANGA (Kihistoria)
Wanaitaji maombi hao.na Mwenyezi mungu awasamee bure.maana hawajui walitendalo
Kigoma watoto wadogo wanafundishwa kareti na judo misikitini, vikiulizwa vinasema vinajiandaa kumpiga khafiri ambaye hata havijui yukoje. kwa stail hii cjui itakuwaje.
Israel ni taifa teule la Mungu...lakini hapa kwa imani zetu hatutakubaliana. Ila tuangalie historia kidogo. Katika majibizano yetu nimegundua unajua sana habari za Farao. Hivi tujiulize, iweje Mungu afungue bahari watu wapite na awaangamize maadai wanaowafukuza? (assumming that hapa hutakataa kwamba hili jambo limewahi kutokea duniani.)
Swala jingine, iweje basi kanchi kadogo kazungukwe na maadui north, south, east & west na adui wengi wanatoka kwenye nchi kubwa sana lakini mpaka leo hawawezi kupatana na kukashambulia hako ka nchi? Haya wewe unaona ni ya kawaida?
Umeseka wanategemea misaada kutoka Marekani. Kwani Tanzania tunapata misaada mingapi kutoka nje? mbona hadi wezi wanaotuibia tunashindwa kuwakamata? Sisi tunaweza kupigana vita na mtu yeyote?
Naomba uangalie hayo mwenzangu. Ila comment kwenye ukweli. Usiunge maneno. Ndio wamarekani wanisaidia Israel na hata rais wa huko akiapishwa lazima akubali kuisaidia lakini pia Marekani inasaidia nchi nyingine. Nyingi ni adui wa Israel. Hapo unasemaje?