peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 12,829
- 21,461
Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), kimethibitisha kufariki dunia kwa mwanafunzi wa shahada ya kwanza ya Sanaa katika Elimu, katika Ndaki ya Insia na Sayansi ya Jamii, NusuraHassan Abdallah ambaye tangu mwanzoni mwa wiki taarifa zake zimekuwa zikisambaa kwenye mitandao ya jamii.
Bila kutaja sababu za kifo chake, taarifa zilizotolewa na kitengo cha masoko na mawasiliano Ijumaa Mei 5, 2023 imesema Mei 3, 2023 menejimenti ya chuo hicho ilipokea taarifa kutoka kwa mwanafunzi anasoma naye kuwa amepokea taarifa kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa mjomba wake Nusura akimjulisha kuwa mwanafunzi huyo amefariki dunia akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Faraja iliyopo Himo mkoani Kilimanjaro.
Hata hivyo, taarifa hiyo imesema hadi kufikia Aprili 27, 2023 Nusura alionekana chuoni akiendelea na masomo.
Mwananchi
UPDATES...
Bila kutaja sababu za kifo chake, taarifa zilizotolewa na kitengo cha masoko na mawasiliano Ijumaa Mei 5, 2023 imesema Mei 3, 2023 menejimenti ya chuo hicho ilipokea taarifa kutoka kwa mwanafunzi anasoma naye kuwa amepokea taarifa kutoka kwa mtu aliyejitambulisha kuwa mjomba wake Nusura akimjulisha kuwa mwanafunzi huyo amefariki dunia akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Faraja iliyopo Himo mkoani Kilimanjaro.
Hata hivyo, taarifa hiyo imesema hadi kufikia Aprili 27, 2023 Nusura alionekana chuoni akiendelea na masomo.
Mwananchi
UPDATES...