only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
Katika kile kinachoonekana kama kukosa akili kwa jeshi la polisi leo limezuhia mkutano wa CHADEMA ukiwa maandalizi yake yamefikia asilimia 99..Tangu asubuhi gari letu limepita kutangaza mkutano huu makini chakushangaza polisi wamekuja kutoa taarifa ya kusimamisha mkutano huu dakika za mwisho,habari za awali zinaonyesha hakuna sababu za msingi za kuzuia mkutano huu.Dalili za polisi kuingilia mkutano huu zilianza kuonekana mapema pale walipokusanyika kwenye vichochoro vya mji wa Dodoma karibu na uwanja wa barafu wakiwa na mavazi yao kama wamekuja kutuliza ghasia...mpaka natoa taarifa hii gari la CHADEMA lilikuwa polisi na bado taarifa za kina hazijatolewa...
Maoni ya wananchi:
Maoni ya wananchi:
- Baada ya kupata taarifa za kuhairishwa mkutano huu,watu walikaa vi-group vidogo vidogo wakionekana na hasira na wakataka kuwaomba viongozi wahutubie na wao watatoa ulinzi,na kijana mmoja akasema huo utakuwa ulinzi shirikishi..
- Wengine wakaomba tuanze maandamano mpaka ofisi ya kamanda wa polisi wa mkoa hili kumpa kilio chetu cha kuharishiwa mkutano dakika za mwisho....