Polisi watoa kituko cha kufungia mwaka leo

Polisi watoa kituko cha kufungia mwaka leo

CCM pekee ndo wanaruhusiwa kufanya siasa kwani si watu wa fujo. Nyie wengine hadi 2020!
 
Ni Jana tuu ndugu wadau Jeshi la Polisi kupitia kwa kamanda wake wa operesheni na mafunzo akitoa ufafanuzi kuhusu zuio la mikutano ya nje na maandamano ya vyama vya SIASA alisema kuwa jeshi hilo huwa haliombi msaada toka kwa RAIA katika kupambana na uhalifu kwani hawana ujuzi Wa mafunzo ya KIJESHI na mbinu zake. Hivyo huwa wanaomba msaada ikibidi kutoka majeshi Mengine.

Na akasisitiza kuwa watu kujikusanya na kwenda kulisaidia jeshi hilo huko Dodoma ni kutaka kuvunja Amani na utulivu uliopo na atakaye kwenda atakiona cha mtema kuni.

Leo jeshi la polisi wakishrikiana na polisi ya kimataifa (INTERPOL) kupitia kituo cha habari ITV saa mbili usiku wametangaza kukamatwa kwa wahalifu wa kimataifa pamoja na mali mbalimbali na siraha walizokuwa nazo wahalifu hao.

Pia Jeshi hilo limeomba RAIA wema KULISAIDIA kupambana na uhalifu na walifu mbalimbali hapa nchini ili kudumisha Amani na utulivu.

Hapo sasa ndo nikapata maswali magumu kwangu matatu ya MSINGI.

1. Kwani sisi RAIA tumepata mafunzo ya kijeshi na mbinu hizo lini mpaka watuombe tuwasaidie kazi zao?

2. Au wanataka tuwasaidie kazi hizo halafu watushugulikie Kama walivyo tangaza Jana tuu hata wiki haijaisha?

3. Au kauli ile ya Jana ya Jeshi la polisi imebatilishwa usiku waa manane wakati tumelala?

Karibuni ndugu zangu tuchangie hoja.
Ukijishughulisha sana na watu hao utapata kichaa. Huwa kila mmoja anatamka la kwake.
 
Kama umejichanganya, samahani lakini, maelezo yako hayajaonesha pahala ambapo jeshi la polisi limewaomba bavicha kwenda Dodoma kuwa saidia kupambana na wahalifu.
Bahati yako mods wanaban kila mwenye mawazo ambayo si kama yako
 
Hey dude, anaongelea logic ya polisi kuomba msaada kwa raia wakati jana walisema raia hawahitajiki kwani hawana mafunzo, jiongeze shing pin liu

Yameongelewa mambo tofauti umechagua hili ulilotaka na mimi nichagua nililotaka.
 
Kwa maoni yangu hakuna mantiki...alichoweka hapa ni kejeli...
Well, kama ni kejeli, basi hao waliokejeliwa imewapasa kukejeliwa maana wamejiaibisha wenyewe kwa kutoa kauli zinazokinzana ndani ya saa chache tu. By the way, ile kitu inaitwa polisi-jamii tafsiri yake nini? Maana raia wameambiwa hawana mafunzo yoyote ya kupambana na uhalifu kwa hiyo hawatakiwi kabisa kujishughulisha na mambo hayo.
 
Kama umejichanganya, samahani lakini, maelezo yako hayajaonesha pahala ambapo jeshi la polisi limewaomba bavicha kwenda Dodoma kuwa saidia kupambana na wahalifu.
So bavicha si binadamu wenye uhalali wa U-Tanzania?
Wanaweza wakawa ni Banyamulenge wanaoombwa msaada wa kusaidia polisi wa TZ
 
Kupambana na uhalifu siyo lazima wewe ndiye ukakamate wahalifu.

Unapotoa taarifa police kuhusu uvunjifu wa sheria au amani katika sehemu uliyopo, kimantiki utakuwa umepambana na uhalifu au wahalifu.

Siyo kila mwananchi amefuzu mafunzo ya kupambana na wahalifu ana kwa ana. Kutoa taarifa police ni njia isiyo na gharama kubwa kwa mwananchi wa kawaida katika kupambana na wahalifu.

Hii ndiyo mantiki ya police.
Kwan bavicha waliomba nauli polisi ili wafike Dodoma
 
Ni Jana tuu ndugu wadau Jeshi la Polisi kupitia kwa kamanda wake wa operesheni na mafunzo akitoa ufafanuzi kuhusu zuio la mikutano ya nje na maandamano ya vyama vya SIASA alisema kuwa jeshi hilo huwa haliombi msaada toka kwa RAIA katika kupambana na uhalifu kwani hawana ujuzi Wa mafunzo ya KIJESHI na mbinu zake. Hivyo huwa wanaomba msaada ikibidi kutoka majeshi Mengine.

Na akasisitiza kuwa watu kujikusanya na kwenda kulisaidia jeshi hilo huko Dodoma ni kutaka kuvunja Amani na utulivu uliopo na atakaye kwenda atakiona cha mtema kuni.

Leo jeshi la polisi wakishrikiana na polisi ya kimataifa (INTERPOL) kupitia kituo cha habari ITV saa mbili usiku wametangaza kukamatwa kwa wahalifu wa kimataifa pamoja na mali mbalimbali na siraha walizokuwa nazo wahalifu hao.

Pia Jeshi hilo limeomba RAIA wema KULISAIDIA kupambana na uhalifu na walifu mbalimbali hapa nchini ili kudumisha Amani na utulivu.

Hapo sasa ndo nikapata maswali magumu kwangu matatu ya MSINGI.

1. Kwani sisi RAIA tumepata mafunzo ya kijeshi na mbinu hizo lini mpaka watuombe tuwasaidie kazi zao?

2. Au wanataka tuwasaidie kazi hizo halafu watushugulikie Kama walivyo tangaza Jana tuu hata wiki haijaisha?

3. Au kauli ile ya Jana ya Jeshi la polisi imebatilishwa usiku waa manane wakati tumelala?

Karibuni ndugu zangu tuchangie hoja.
Hehehehe bongo nchi ya kusadikika wallaj
 
Hugo msaada unaombwa kwa raia wema waliofundishwa manbo ya kijeshi lakini mimi na wewe haturuhusiwi kikwapa msaada au ushirikiano. Ukithubutu tu utanyang'anywa silaa. Ulionja ile ya Lipumba?
 
Nafikiri jeshi letu la polisi halina communication strategist wazuri-inakua kama wanakurupuka bila kuangalia nani aseme nini na bila kuangalia implications za kile wasemacho. Mmoja anaruhusu mkutano Kahama na ndio mwenye mamlaka ya kufanya hivyo lakini wakuu dar wanapiga mikutano yote marufuku. Yule jamaa jana kasema bila chenga hawahitaji msaada wa kina sisi-hapo hapo wana sera ya polisi jamii. Si wangesema tu Bavicha hawaruhusiwi kwenda kusaidia 23/7 badala ya kusema hawahitaji msaada wa kina sisi. Pili nafikiri ni vizuri waandike na kusoma tu matamshi yao kwani katika kutaka kuonyesha kwamba wana zile nguvu za dola hujisahau na kuwakilisha ujumbe wao visivyo. Kuna mkutano mmoja wa CDM CCM walisema wanaupinga basi jeshi la polisi likafuta mkutano wa CDM-badala ya kuulinda hizo ndio contradiction za jeshi letu inakuwa vigumu kutabiri watasema au kufanya nini.
 
walisema hawahitaji msaada kuwalinda au kuwazuia CCM kukabidhiana kijiti.
 
Nilipenda sana kushuhudia hii expendable part 3 ya dodoma mbowe kaninyima utamu dah
 
Back
Top Bottom