Polisi wapigana kibaha mzani

Polisi wapigana kibaha mzani

Makamee

JF-Expert Member
Joined
Nov 29, 2013
Posts
2,029
Reaction score
1,201
Askari wawili wa jeshi la polisi jana usiku walipigana ngumi hadharani wakiwa eneo la kazi ktk eneo la mzani Kibaha.
Chanzo cha ugomvi inasemekana ni askari Trafic mwenye cheo cha Coplo kudai ameingiliwa majukumu yake na askari wa kawaida aliekuepo eneo hilo kwa kulikomalia gari lililozidisha mzigo lazima lipitie ktk mizani kitendo ambacho kilimkera coplo huyo na kuanza kumpiga askari mwenzie.
 
Baadhi ya hawa jamaa huenda watatusaidia sana huko mbeleni maana ndani yao kuna wasioridhika na hali iliyopo pia.
 
Rushwa haina advance wala risiti

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Halloo muraa limeniingila eneo langu la kula lzm nilidunde ovaaa"
 
Askari wawili wa jeshi la polisi jana usiku walipigana ngumi hadharani wakiwa eneo la kazi ktk eneo la mzani Kibaha.
Chanzo cha ugomvi inasemekana ni askari Trafic mwenye cheo cha Coplo kudai ameingiliwa majukumu yake na askari wa kawaida aliekuepo eneo hilo kwa kulikomalia gari lililozidisha mzigo lazima lipitie ktk mizani kitendo ambacho kilimkera coplo huyo na kuanza kumpiga askari mwenzie.


Ma constable wa polisi wanajenga majumba na kununua magari kwa sababu ya hiyo check point ya mizani ya Kibaha. Na kwa jinsi rushwa inavyotembea hapo ndio maana unaona askari wa kawaida anaamua kwenda kutega hapo ili angalau ajipatie chochote na huyu wa traffic akaona kuwa mapato yake yatapungua.
 
Kova anaona wenyeviti waliojiteka kuisingiza chadema tu ila hawa wala rushwaa..aah!!macho yake yanaangalia kwingine...
 
walizidiana kwenye kudai rushwa.....
 
Chanzo: Gazeti Jamhuri (wiki iliyopita)


Matrafiki Maili Moja
na rushwa ya nje nje

Mkata Mitaa (MM) anasema mtu anayetaka kujua nchi hii imeoza kwa kiwango gani kwa matukio ya rushwa, asipate shida!

Anayetaka kushuhudia rushwa inavyotolewa hadharani kana kwamba nchi hii haina Takukuru wala wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, basi afike pale Kituo cha Mabasi cha Maili Moja, na Mizani pale Kibaha mkoani Pwani.

Kama kuna mwenye kutaka kushuhudia sinema hii, anachopaswa kufanya ni kujihimu asubuhi na mapema na kuwapo hapo kituoni.

Awali, MM alikuwa haamini kinachosemwa juu ya mapolisi wa usalama barabarani waliojazana hapo kituoni. Baada ya kuguswa na jambo hilo, juzi aliamua kwenda kujionea.

Matrafiki waliopo hapo kituoni wote wamenona. Ukimuona mwembamba, basi ujue moja kati ya mawili-ama ana matatizo kiafya, au ni mgeni!

Kinachofanywa na matrafiki hao ni kuhakikisha wananyang'anyana magari. Kila basi linapotokea, MM aliwaona matrafiki wawili au watatu wakilikimbilia. Kuna wakati aliwaona wawili wakigombana-kila mmoja akitaka ‘apewe kadi'. Kondakta akatulia kwa sekunde kadhaa ili waamue nani ashike hiyo ‘kadi'. Baada ya muda trafiki mmoja akaondoka, lakini ni baada ya kuona kuna basi jingine linaingia.

Kinachofanywa na matrafiki hao ni kuhakikisha wanashikishwa kadi ambayo MM hajajua kama ni ya basi husika au ni ratiba. Wakati trafiki anapopokea, lazima vidole vyake vigusane na vya kondakta wa basi husika. Kwenye huo mgusano ndimo huwa kuna pesa.

Baada ya kuuliza, MM akaambiwa kila basi linalopota hapo lazima litokea si chini ya Sh 2,000. Kwenye rushwa ni dhambi, lakini kwa kiwango hiki hii ni dhambi kubwa kwa sababu waswahili husema ukiamua kula kondoo, basi chagua aliyenona! Hawa matrafiki wa Kibaha hawajali hilo, wanachotambua ni kupata tu!

MM akarejea kwenye kauli za danganya toto za Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini za kwamba ofisi yake imejipanga kuhakikisha ajali za barabarani zinakomeshwa, hasa wakati huu wa sikukuu za mwisho wa mwaka.

Anasema ni kauli za danganya toto kwa sababu wale matrafiki, tena wakiwamo ma-vehicle inspector wanachofanya si kukagua usalama wa basi, bali wanachofanya ni kukusanya rushwa kutoka katika kila basi.

Matukio yanayoendelea Kituo cha Mabasi, Maili Moja Kibaha ni aibu, si kwa Jeshi la Polisi tu, bali ni kwa Taifa zima. Ikumbukwe kuwa kuna wasafiri wengi ambao ni wageni wanaotoka au kwenda mataifa kama Zimbabwe, Zambia, Rwanda, Burundi, DRC, Kenya, Uganda nk.

Rushwa inayotolewa hapo Kibaha inadhihirisha kuwa vyombo vyote vyenye dhima ya kupambana na dhambi hii ni kama vimeshakufa na vinasubiri kuzikwa! Hakuna Takukuru, Polisi wenyewe wala Usalama wa Taifa walio tayari kuiondoa aibu hii.

Kama Kamanda Mpinga anadhani haya yanayosemwa na MM hapa ni chuki na uzushi, ajitahidi kesho asubuhi afike hapo kituoni akiwa amevaa kiraia. Kwa atakayoyaona, na kama kweli yeye ni mwadilifu, anaweza kuanguka kwa kihoro. Maili Moja ile siyo rushwa, bali ni mradi unaoonekana kupata baraka zote za wakubwa, hasa wa polisi.

Ukiyaona ya hapo hutasika kuamini kuwa huenda kweli wakubwa ndiyo wanaowatuma hawa matrafiki ili jioni wawasilishe hesabu. Lakini kubwa kuliko yote ni hili; kwanini hawa matrafiki wa Kibaha hawahamishwi? Kazi kwako Kamanda Mpinga maana inaelekea Pwani hakuna RPC na kama yupo, kashindwa!
 
Umenena Mkuu,kuna mengi ya kuangalia ndani ya jeshi la polisi.
 
Kova anaona wenyeviti waliojiteka kuisingiza chadema tu ila hawa wala rushwaa..aah!!macho yake yanaangalia kwingine...

Kova anaona wenyeviti waliojiteka kuisingiza chadema tu ila hawa wala rushwaa..aah!!macho yake yanaangalia kwingine...

yaani wewe hata dar es salaam ilipoishia ujui kazi kuropoka tu kama tobo lissu
 
Back
Top Bottom