Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Nadhani Polisi wanafanya mzaha kwenye mambo serious. Juzi Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, SACP Gilles Muroto alisema kwamba walipokamata Nabii Tito walimpeleka hospitali ya Mirembe na alipochunguzwa ilibainika kuwa na ugonjwa wa akili. Kama Medical report ilionesha hivyo nilitegemea polisi wanemrudisha Mirembe akapate matibabu. Lakini waliendelea kmshikilia.
Jana wamempeleka nyumbani kwake Nong'ona (nyuma ya UDOM) ili kwenda kumfanyia upekuzi. Taarifa kutoka mtandao wa [HASHTAG]#TanzaniaToday[/HASHTAG]zinaeleza kuwa Nabii huyo alipoingia ndani alifanya jaribio la kujiua kwa kujikata na tumboni na kitu chenye ncha kali, ambapo alikimbizwa hospitali na kushonwa nyuzi 21.
Najaribu kujiuliza ikiwa Nabii huyo angefanikiwa kujiua polisi wangeeleza nini jamii? Mmeshaambiwa mtu ni mgonjwa wa akili kwanini muendelee kumshikilia? Na mlipoenda kumpekua nyumbani kwake kwanini mlimpa uhuru wa kuwa peke yake wakati mnajua ni mgonjwa wa akili? Nadhani kuna uzembe mahali. Polisi wajitafakari.!
Jana wamempeleka nyumbani kwake Nong'ona (nyuma ya UDOM) ili kwenda kumfanyia upekuzi. Taarifa kutoka mtandao wa [HASHTAG]#TanzaniaToday[/HASHTAG]zinaeleza kuwa Nabii huyo alipoingia ndani alifanya jaribio la kujiua kwa kujikata na tumboni na kitu chenye ncha kali, ambapo alikimbizwa hospitali na kushonwa nyuzi 21.
Najaribu kujiuliza ikiwa Nabii huyo angefanikiwa kujiua polisi wangeeleza nini jamii? Mmeshaambiwa mtu ni mgonjwa wa akili kwanini muendelee kumshikilia? Na mlipoenda kumpekua nyumbani kwake kwanini mlimpa uhuru wa kuwa peke yake wakati mnajua ni mgonjwa wa akili? Nadhani kuna uzembe mahali. Polisi wajitafakari.!