Blessed Tajiri
JF-Expert Member
- Dec 16, 2023
- 221
- 659
Tutafika Oktoba tukiwa tumechoka sana!
====
WAWILI WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA MATUMIZI MABAYA YA MITANDAO.
Jeshi la Polisi Mkoani Arusha limetoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa inayosambaa kwenye baadhi ya mitandao ya kijamii ikieleza juu ya watu wawili kukamatwa na watu wasiojulikana huko katika maeneo ya Maji ya Chai, wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha.
Akitoa ufafanuzi kuhusiania na tukio hilo leo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Justine Masejo amesema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa na Jeshi la Polisi Juni 20 mwaka huu na kuwataja kuwa ni Jackson Kabalo (32) na Joseph Mrindoko (37) wote wakiwa ni wajasiriamali, wakazi wa Maji ya Chai wilayani Arumeru kwa tuhuma za matumizi mabaya ya mitandao.
Soma Pia: Kundi la “Wachokonozi” wamekamatwa na watu waliodai kuwa ni Askari Polisi katika eneo la Maji ya Chai, Arumeru, Arusha
Kamanda Masejo amebainisha kuwa upelelezi wa tukio hilo unaendelea na pindi utakapokamilika hatua zaidi za kisheria zitafuata.
Jeshi la Polisi Mkoani humo limetoa onyo kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii kuacha kusambaza taarifa ambazo hawana uhakika nazo zinazoleta taharuki katika jamii hasa zile za kuzusha kuwa watuhumiwa wamekamatwa na watu wasiojulikana jambo ambalo sio la kweli.
Pia soma: Polisi Arusha: Ni kweli tunawashikilia Wachokonozi kwa makosa mbalimbali
====
WAWILI WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA MATUMIZI MABAYA YA MITANDAO.
Jeshi la Polisi Mkoani Arusha limetoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa inayosambaa kwenye baadhi ya mitandao ya kijamii ikieleza juu ya watu wawili kukamatwa na watu wasiojulikana huko katika maeneo ya Maji ya Chai, wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha.
Akitoa ufafanuzi kuhusiania na tukio hilo leo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Justine Masejo amesema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa na Jeshi la Polisi Juni 20 mwaka huu na kuwataja kuwa ni Jackson Kabalo (32) na Joseph Mrindoko (37) wote wakiwa ni wajasiriamali, wakazi wa Maji ya Chai wilayani Arumeru kwa tuhuma za matumizi mabaya ya mitandao.
Soma Pia: Kundi la “Wachokonozi” wamekamatwa na watu waliodai kuwa ni Askari Polisi katika eneo la Maji ya Chai, Arumeru, Arusha
Kamanda Masejo amebainisha kuwa upelelezi wa tukio hilo unaendelea na pindi utakapokamilika hatua zaidi za kisheria zitafuata.
Jeshi la Polisi Mkoani humo limetoa onyo kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii kuacha kusambaza taarifa ambazo hawana uhakika nazo zinazoleta taharuki katika jamii hasa zile za kuzusha kuwa watuhumiwa wamekamatwa na watu wasiojulikana jambo ambalo sio la kweli.
Pia soma: Polisi Arusha: Ni kweli tunawashikilia Wachokonozi kwa makosa mbalimbali