Polisi wa Barabarani wanatuchanganya!

Tanzania Mpya

JF-Expert Member
Apr 11, 2012
253
144
Siwaelewi hawa polisi wanapoingia ktkt ya barabara na kuanza kuongoza magari wakati taa nazo bado zinawaka. Kuna siku nilikuja speed nawahi taa za kijani lkn nilipokaribia kuvuka ndipo nikamuona polisi yupo pale anaita magari ya upande mwingine. Kuna dada alimgonga polisi alipoingia ktk junction kwa kuruhusiwa na taa bila kujua kwamba pale ktk kulikuwa na polisi anaongoza magari!

Hivi hakuna namna ya wao kuzizima hizi taa kabla ya kuingia na kuongoza kwa mkono? Hii ni hatari sana, ni kutaka kuingizana ktk matatizo. Naomba Polisi waliangalio hilo, tunatuchanganya sana na wao pia wanajiweka hatarini. Kama taa zinawaka, waache tufuate taa, na kama wanataka kuongoza kwa mkono watafute namna ya kuzizima kwanza.
 
sawa mkuu. Mimi pia sipendi utaratibu wa polisi kuwa kwenye traffic lights kuongoza magari wakati huo taa zinafanyakazi.
 
Kwanza wakiongoza magari wanasababisha foleni tu,lakini nafikiri huwa wanafanya hivyo ili
wengine wazungukie kwenye magari yaliyosimama kwenye foleni.Si unajua mambo ya kupeleka
hesabu kwa wakuu.
 
Mie sikumoja pale Salender bridge muda wa saa moja na nusu usiku nilipita nikiwa gari la mwisho na taa zimekuwa nyekundu, polisi akiwa katikati ya barabara, tena amelewa. Akanisimamisha kwa nini napita na taa nyekundu, nikamjibu bwana, wewe unafanya nini hapa katikati kwenye taa kama huongozi na taa zinafanya kazi? Mie nilidhani tunaongozwa na wewe sio taa. Tukabishana, mwishowe akaniambia haya hebu niachie kitu kidogo uondoke!
 
jamani tuwapende polisi wetu kwani wao wanafanya kazi ngumu pia miundo mbinu ya barabara ni duni nchini mwetu so mazingira yao ya kazi ni magumu.....
 
Mie sikumoja pale Salender bridge muda wa saa moja na nusu usiku nilipita nikiwa gari la mwisho na taa zimekuwa nyekundu, polisi akiwa katikati ya barabara, tena amelewa. Akanisimamisha kwa nini napita na taa nyekundu, nikamjibu bwana, wewe unafanya nini hapa katikati kwenye taa kama huongozi na taa zinafanya kazi? Mie nilidhani tunaongozwa na wewe sio taa. Tukabishana, mwishowe akaniambia haya hebu niachie kitu kidogo uondoke!

Ni hatari sana! Wanapaswa kujirekebisha haraka.
 
jamani tuwapende polisi wetu kwani wao wanafanya kazi ngumu pia miundo mbinu ya barabara ni duni nchini mwetu so mazingira yao ya kazi ni magumu.....

Sio kwamba hatuwapendi, no. Tunachosema wafanye kazi kiusalama zaidi, wazime kwanza taa za barabarani ndipo waongoze kwa mkono, kwa kuwa mara nyingine hawaonekani watu wanaangalia taa.
 
Back
Top Bottom